< Nehemia 11 >

1 Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
And the princes of the people dwelt in Jerusalem; the rest of the people also cast lots, to bring one of ten to dwell in Jerusalem the holy city, and nine parts in the other cities.
2 Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
And the people blessed all the men that willingly offered themselves to dwell in Jerusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
Now these are the chiefs of the province that dwelt in Jerusalem; but in the cities of Judah dwelt every one in his possession in their cities, to wit, Israelites, the priests, and the Levites, and the Nethinim, and the children of Solomon's servants.
4 ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
And in Jerusalem dwelt certain of the children of Judah, and of the children of Benjamin. Of the children of Judah: Athaiah the son of Uzziah, the son of Zechariah, the son of Amariah, the son of Shephatiah, the son of Mahalalel, of the children of Perez;
5 Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
and Maaseiah the son of Baruch, the son of Colhozeh, the son of Hazaiah, the son of Adaiah, the son of Joiarib, the son of Zechariah, the son of the Shilonite.
6 Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
All the sons of Perez that dwelt in Jerusalem were four hundred threescore and eight valiant men.
7 Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
And these are the sons of Benjamin: Sallu the son of Meshullam, the son of Joed, the son of Pedaiah, the son of Kolaiah, the son of Maaseiah, the son of Ithiel, the son of Jeshaiah.
8 na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
And after him Gabbai, Sallai, nine hundred twenty and eight.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
And Joel the son of Zichri was their overseer; and Judah the son of Hassenuah was second over the city.
10 Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
Of the priests: Jedaiah the son of Joiarib, Jachin,
11 Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
Seraiah the son of Hilkiah, the son of Meshullam, the son of Zadok, the son of Meraioth, the son of Ahitub, the ruler of the house of God,
12 pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
and their brethren that did the work of the house, eight hundred twenty and two; and Adaiah the son of Jeroham, the son of Pelaliah, the son of Amzi, the son of Zechariah, the son of Pashhur, the son of Malchijah,
13 na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
and his brethren, chiefs of fathers' houses, two hundred forty and two; and Amashsai the son of Azarel, the son of Ahzai, the son of Meshillemoth, the son of Immer,
14 na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
and their brethren, mighty men of valour, a hundred twenty and eight; and their overseer was Zabdiel, the son of Haggedolim.
15 Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
And of the Levites: Shemaiah the son of Hasshub, the son of Azrikam, the son of Hashabiah, the son of Bunni;
16 Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
and Shabbethai and Jozabad, of the chiefs of the Levites, who had the oversight of the outward business of the house of God;
17 Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
and Mattaniah the son of Mica, the son of Zabdi, the son of Asaph, who was the chief to begin the thanksgiving in prayer, and Bakbukiah, the second among his brethren; and Abda the son of Shammua, the son of Galal, the son of Jeduthun.
18 Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
All the Levites in the holy city were two hundred fourscore and four.
19 Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
Moreover the porters, Akkub, Talmon, and their brethren, that kept watch at the gates, were a hundred seventy and two.
20 Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
And the residue of Israel, of the priests, the Levites, were in all the cities of Judah, every one in his inheritance.
21 Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
But the Nethinim dwelt in Ophel; and Ziha and Gishpa were over the Nethinim.
22 Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
The overseer also of the Levites at Jerusalem was Uzzi the son of Bani, the son of Hashabiah, the son of Mattaniah, the son of Mica, of the sons of Asaph, the singers, over the business of the house of God.
23 Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
For there was a commandment from the king concerning them, and a sure ordinance concerning the singers, as every day required.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
And Pethahiah the son of Meshezabel, of the children of Zerah the son of Judah, was at the king's hand in all matters concerning the people.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
And for the villages, with their fields, some of the children of Judah dwelt in Kiriath-arba and the towns thereof, and in Dibon and the towns thereof, and in Jekabzeel and the villages thereof;
26 katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
and in Jeshua, and in Moladah, and Beth-pelet;
27 katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
and in Hazar-shual, and in Beer-sheba and the towns thereof;
28 katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
and in Ziklag, and in Meconah and in the towns thereof;
29 katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
and in En-rimmon, and in Zorah, and in Jarmuth;
30 Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
Zanoah, Adullam, and their villages, Lachish and the fields thereof, Azekah and the towns thereof. So they encamped from Beer-sheba unto the valley of Hinnom.
31 Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
And the children of Benjamin from Geba onward, at Michmas and Aijah, and at Beth-el and the towns thereof;
32 katika Anathothi, Nobu na Anania,
at Anathoth, Nob, Ananiah;
33 katika Hazori, Rama na Gitaimu,
Hazor, Ramah, Gittaim;
34 katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
Hadid, Zeboim, Neballat;
35 katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
Lod, and Ono, Ge-harashim.
36 Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.
And of the Levites, certain courses in Judah were joined to Benjamin.

< Nehemia 11 >