< Mika 7 >

1 Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
Misery is mine. Indeed, I am like one who gathers the summer fruits, as gleanings of the vineyard: There is no cluster of grapes to eat. My soul desires to eat the early fig.
2 Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
The faithful have vanished from the earth, and there is no one upright among men. They all lie in wait for blood; every man hunts his brother with a net.
3 Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
Their hands are on that which is evil to do it diligently. The ruler and judge ask for a bribe; and the powerful man dictates the evil desire of his soul. Thus they conspire together.
4 Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
The best of them is like a brier. The most upright is worse than a thorn hedge. The day of your watchmen, even your visitation, has come; now is the time of their confusion.
5 Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
Do not trust in a neighbor. Do not put confidence in a friend. With the woman lying in your embrace, be careful of the words of your mouth.
6 Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
For the son dishonors the father, the daughter rises up against her mother, the daughter-in-law against her mother-in-law; a man's enemies are the men of his own house.
7 Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
But as for me, I will look to Jehovah. I will wait for the God of my salvation. My God will hear me.
8 Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
Do not rejoice against me, my enemy. When I fall, I will arise. When I sit in darkness, Jehovah will be a light to me.
9 Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
I will bear the indignation of Jehovah, because I have sinned against him, until he pleads my case, and executes judgment for me. He will bring me forth to the light. I will see his righteousness.
10 Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
Then my enemy will see it, and shame will cover her who said to me, where is Jehovah your God? Then my enemy will see me and will cover her shame. Now she will be trodden down like the mire of the streets.
11 Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
A day to build your walls; in that day, he will extend your boundary.
12 Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
In that day they will come to you from Assyria and the cities of Egypt, and from Egypt even to the River, and from sea to sea, and mountain to mountain.
13 Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
Yet the land will be desolate because of those who dwell in it, for the fruit of their doings.
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
Shepherd your people with your staff, the flock of your heritage, who dwell by themselves in a forest, in the midst of fertile pasture land, let them feed; in Bashan and Gilead, as in the days of old.
15 “Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
"As in the days of your coming forth out of the land of Egypt, I will show them marvelous things."
16 Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
The nations will see and be ashamed of all their might. They will lay their hand on their mouth. Their ears will be deaf.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
They will lick the dust like a serpent. Like crawling creatures of the earth they shall come trembling out of their dens. They will come with fear to Jehovah our God, and will be afraid because of you.
18 Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
Who is a God like you, who pardons iniquity, and passes over the disobedience of the remnant of his heritage? He doesn't retain his anger forever, because he delights in loving kindness.
19 Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
He will again have compassion on us. He will tread our iniquities under foot; and you will cast all their sins into the depths of the sea.
20 Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.
You will give truth to Jacob, and mercy to Abraham, as you have sworn to our fathers from the days of old.

< Mika 7 >