< Mika 2 >

1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Malheur à ceux qui méditent l’iniquité et préparent le mal sur leurs couches, pour l’accomplir dès la pointe du jour autant que cela est en leur pouvoir!
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
Ils convoitent des champs et les volent, des maisons et s’en emparent. Ils usent de violence envers les hommes et leurs demeures, envers les propriétaires et leurs domaines.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
Eh bien! dit l’Eternel, voici je médite, moi, contre cette engeance une calamité où vous enfoncerez jusqu’au cou: vous ne marcherez plus la tête haute, car ce sera un temps de malheur.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
En ce jour, on chantera à votre propos une satire, on soupirera une complainte; on dira: "Nous sommes totalement ruinés! L’Héritage de mon peuple passe à d’autres mains. Hélas! Comme on m’en expulse pour le répartir entre les ravisseurs de notre champ!"
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
En vérité il n’y aura personne pour toi qui puisse jeter le cordeau sur un lot de terre dans la Communauté du Seigneur.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
"Ne pérorez pas, ainsi pérorent-ils; on ne débite pas de pareils discours; les avanies n’ont pas de fin!"
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
Est-il permis de parler ainsi, maison de Jacob? L’Eternel manque-t-il de patience? Sont-ce là ses œuvres? Mes paroles ne sont-elles pas bienveillantes pour celui qui marche droit?
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
Mais depuis longtemps mon peuple s’érige en ennemi; ceux qui passent en sécurité, comme s’ils revenaient du combat, vous les dépouillez du manteau qui couvre leur vêtement.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
Les femmes de mon peuple, vous les chassez de leurs maisons de plaisance; à leurs enfants vous enlevez pour toujours le lustre qu’ils me doivent.
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Debout et en route! car ce n’est plus ici une terre de repos: parce qu’elle a été souillée, elle sera une cause de souffrances, de cruelles souffrances.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
Qu’un homme se présente, se nourrissant de vent, inventant des mensonges, et qu’il dise: "Je vais te tenir des discours sur le vin et les boissons fortes," voilà un prédicateur pour ce peuple!
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
J’Aurai soin de te rassembler tout entier, ô Jacob, de te réunir, ô reste d’Israël! Comme les brebis dans un parc, comme un troupeau dans le pâturage, je les mettrai ensemble: ce sera une multitude bruyante d’hommes.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
Devant eux marche celui qui brise la clôture; ils la renversent, se précipitent par l’ouverture et sortent: leur roi les précède et l’Eternel est à leur tête.

< Mika 2 >