< Mika 2 >

1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Wo to you, that thenken vnprofitable thing, and worchen yuele in youre beddis; in the morewtid liyt thei don it, for the hond of hem is ayenus God.
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
Thei coueitiden feeldis, and tooken violentli; and rauyschiden housis, and falsli calengiden a man and his hous, a man and his eritage.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
Therfor the Lord seith these thingis, Lo! Y thenke on this meynee yuel, fro which ye schulen not take awei youre neckis; and ye schulen not walke proude, for the worste tyme is.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
In that dai a parable schal be takun on you, and a song schal be songun with swetnesse of men, seiynge, Bi robbyng we ben distried; a part of my puple is chaungid; hou schal he go awei fro me, whanne he turneth ayen that schal departe youre cuntreis?
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
For this thing `noon schal be to thee sendynge a litil corde of sort in cumpeny of the Lord.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
A! thou Israel, speke ye not spekyng; it schal not droppe on these men, confusioun schal not catche,
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
seith the hous of Jacob. Whether the Spirit of the Lord is abreggid, either siche ben the thouytis of hym? Whether my wordis ben not gode, with hym that goith riytli?
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
And ayenward my puple roos togidere in to an aduersarie; ye token awei the mantil aboue the coote, and ye turneden in to batel hem that wenten sympli.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
Ye castiden the wymmen of my puple out of the hous of her delices; fro the litle children of hem ye token awei myn heriyng with outen ende.
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Rise ye, and go, for here ye han not reste; for the vnclennesse therof it schal be corrupt with the worst rot.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
Y wolde that Y were not a man hauynge spirit, and rathere Y spak a leesyng. Y schal droppe to thee in to wyn, and in to drunkenesse; and this puple schal be, on whom it is droppid.
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
With gaderyng Y schal gadere Jacob; Y schal lede togidere thee al in to oon, the relifs of Israel. Y schal put hym togidere, as a floc in folde; as scheep in the myddil of fooldis thei schulen make noise, of multitude of men.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
For he schal stie schewynge weie bifore hem; thei schulen departe, and passe the yate, and schulen go out therbi; and the kyng of hem schal passe bifore hem, and the Lord in the heed of hem.

< Mika 2 >