< Mika 1 >

1 Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
This is the word of Yahweh that came to Micah the Morashtite in the days of Jotham, Ahaz, and Hezekiah, kings of Judah, which he saw concerning Samaria and Jerusalem.
2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
Listen, all you peoples. Listen, earth, and all that is in you. Let the Lord Yahweh be a witness against you, the Lord from his holy temple.
3 Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
Look, Yahweh comes out of his place; he will come down and tread on the high places of the earth.
4 Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
The mountains will melt under him; the valleys will break apart, like wax before fire, like waters that are poured down a steep place.
5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
All this is because of the Jacob's transgression, and because of the sins of the house of Israel. What is Jacob's transgression? Is it not Samaria? What is Judah's high place? Is it not Jerusalem?
6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
“I will make Samaria a heap of ruins in the field, a place for planting vineyards, and I will pour her stones down into the valley and I will uncover her foundations.
7 Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
All her carved figures will be broken to pieces, and all her gifts that she received will be burned with fire, and I will destroy all her idols. Since she gathered her gifts from the wages of prostitutes, they will become the wages of prostitutes again.”
8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
For this reason I will lament and wail; I will go barefoot and naked; I will wail like the jackals and mourn like owls.
9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
For her wound is incurable, for it has come to Judah. It has reached the gate of my people, to Jerusalem.
10 Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
Do not tell about it in Gath; do not weep at all. At Beth Leaphrah I roll myself in the dust.
11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
Pass by, inhabitants of Shaphir, in nakedness and shame. The inhabitants of Zaanan do not come out. Beth Ezel mourns, for their protection is taken away.
12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
For the inhabitants of Maroth wait anxiously for good news, because disaster has come down from Yahweh to the gates of Jerusalem.
13 Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
Harness the chariot to the team of horses, inhabitants of Lachish. You, Lachish, were the beginning of sin for the daughter of Zion, for the transgressions of Israel were found in you.
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
So you will give a parting gift to Moresheth Gath; the town of Akzib will disappoint the kings of Israel.
15 Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
I will again bring a conqueror to you, inhabitants of Mareshah; the splendor of Israel will come to Adullam.
16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.
Shave your head and cut off your hair for the children in whom you delight. Make yourself as bald as eagles, for your children will go into exile from you.

< Mika 1 >