< Mathayo 18 >

1 Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?”
At that hour the disciples came to Jesus, and said: Who then is greatest in the kingdom of heaven?
2 Yesu akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao.
And Jesus called a little child to him, and placed him in the midst of them,
3 Naye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.
and said: Verily I say to you, Unless you turn and become as little children, you can not enter the kingdom of heaven.
4 Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni.
Whoever, therefore, humbles himself as this little child, is greatest in the kingdom of heaven.
5 “Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
And whoever receives one such little child on my account, receives me;
6 Lakini kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
but whoever ensnares one of these little ones that believe in me, it were better for him that a millstone were hung about his neck, and that he were drowned in the depth of the sea.
7 “Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya yale mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mtu yule ambaye huyasababisha.
Alas for the world because of snares! for it is necessary that snares come: but alas for that man by whom the snare comes!
8 Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
If, then, your hand or your foot ensnares you, cut it off, and throw it from you. It is better for you to enter into life lame or maimed, than, having two hands or two feet, to be thrown into the eternal fire. (aiōnios g166)
9 Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
And if your eye ensnares you, pull it out, and throw it from you. It is better to enter into life with one eye, than, having two eyes, to be thrown into hell-fire. (Geenna g1067)
10 “Angalia ili usimdharau mmojawapo wa hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni. [
Take heed that you despise not one of these little ones: for I say to you, That their angels in heaven do always behold the face of my Father who is in heaven.
11 Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.]
For the Son of man has come to save that which is lost.
12 “Mwaonaje? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je, hatawaacha wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta huyo mmoja aliyepotea?
What think you? If a man have a hundred sheep, and one of them go astray, does he not leave the ninety-nine, and go into the mountains, and seek for that which has gone astray?
13 Naye akishampata, amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
And if it so be that he find it, verily I say to you, he rejoices over it more than over the ninety-nine that did not go astray.
14 Vivyo hivyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.
Even so, it is not the will of your Father who is in heaven, that one of these little ones should be lost.
15 “Kama ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa umempata tena ndugu yako.
And if your brother sin against you, go and tell him of his fault between you and him alone; if he hear you, you have gained your brother.
16 Lakini kama hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja au wawili ili kila neno lithibitishwe kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.
But if he will not hear you, take with you one or two more, that, by the mouth of two or three witnesses, every word may be established.
17 Kama akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa. Naye kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi awe kwenu kama mtu asiyeamini au mtoza ushuru.
But if he refuse to hear them, tell it to the church; and if he also refuse to hear the church, let him be to you as a heathen man and a publican.
18 “Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
Verily, I say to you, my disciples, Whatever you bind on earth, shall be bound in heaven; and whatever you loose on earth, shall be loosed in heaven.
19 “Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu watakubaliana duniani kuhusu jambo lolote watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
Again, I say to you, that if two of you agree on earth about any thing for which they will ask, it shall be done for them by my Father who is in heaven.
20 Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa Jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.”
For where there are two or three that have come together for my sake, there I am in the midst of them.
21 Ndipo Petro akamjia Yesu na kumuuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
Then Peter came to him, and said: Lord, how often shall my brother sin against me, and I forgive him? Till seven times?
22 Yesu akamjibu, “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
Jesus said to him: I say to you, Not till seven times, but till seventy times seven.
23 “Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya hesabu zake za fedha na watumishi wake.
For this reason, the kingdom of heaven is likened to a king that wished to settle accounts with his servants.
24 Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja aliyekuwa anadaiwa talanta10,000, aliletwa kwake.
And when he began to make a settlement, there was brought to him one that owed him ten thou sand talents.
25 Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa navyo, ili lile deni lipate kulipwa.
But as he was not able to pay, his lord commanded him, and his wife, and children, and all that he had, to be sold, and payment to be made.
26 “Yule mtumishi akampigia magoti, akamsihi yule bwana akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
Therefore, the servant fell down and besought him, saying, Have patience with me, Lord, and I will pay you all.
27 Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha aende zake.
And the lord of that servant was moved with compassion, and let him go, and forgave him the debt.
28 “Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka nje, akakutana na mtumishi mwenzake aliyekuwa amemkopesha dinarimia moja. Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai!’
But that servant went out, and found one of his fellow-servants, who owed him a hundred denarii; and he laid hold of him, and took him by the throat, saying: Pay me what you owe.
29 “Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
Then his fellow-servant fell down at his feet, and besought him, saying: Have patience with me, and I will pay you all.
30 “Lakini akakataa. Badala yake, alienda akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni.
And he would not; but went and threw him into prison, till he should pay the debt.
31 Watumishi wenzake walipoona haya yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa kimetukia.
When his fellow-servants saw what was done, they were very sad, and went and made known to their lord all that was done.
32 “Yule bwana akamwita yule mtumishi akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi nilikusamehe deni lako lote uliponisihi.
Then his lord called him and said to him: Wicked servant! I forgave you all that debt, because you besought me.
33 Je, haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’
Ought you not to have had mercy on your fellow-servant, even as I had mercy on you?
34 Kwa hasira, yule bwana wake akamtia yule mtumishi mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
And his lord was angry, and delivered him to the jailers, till he should pay all that was due him.
35 “Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”
So also will my heavenly Father do to you, if, from your hearts, you forgive not every one his brother’s offenses.

< Mathayo 18 >