< Marko 15 >

1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
And as soon as ever it was light the chief priests holding a consultation with the elders and scribes, they and the whole sanhedrim, bound Jesus, and carried Him away, and delivered Him to Pilate.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
And Pilate asked Him, Art thou the king of the Jews? and He answered It is as thou sayst.
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
And the chief priests accused Him of many things: but he answered nothing.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
So Pilate asked Him again, saying, Dost thou answer nothing? See how many things they witness against thee:
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
but Jesus still answered nothing, so that Pilate was amazed.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
Now at the feast he used to release to them one prisoner, whomsoever they desired:
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
and there was one Barabbas under confinement with some of his accomplices in sedition, who had committed murder in the insurrection.
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
And the people clamoured and desired him to do as he always used to do for them.
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
But Pilate answered them, saying, Would ye have me release to you the king of the Jews?
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
(for he knew that the chief priests had delivered Him up to him out of envy: )
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
but the chief priests incited the people to desire that he would rather release Barabbas to them.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
And Pilate answered, and said to them again, What then would you have me do with Him, whom ye call king of the Jews?
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
And they cried out again, Crucify Him.
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
But Pilate said unto them, Why, what ill has He done? And they cried out the more vehemently, Crucify Him.
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
So Pilate being willing to ingratiate with the multitude, released Barabbas to them, and having scourged Jesus, delivered Him up to be crucified.
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
And the soldiers led Him away into the hall, which is called the Pretorium; and gathered their whole company together:
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
and they clad Him in purple, and platted a crown of thorns and put it on his head,
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
and saluted Him, saying, Hail king of the Jews;
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
and struck Him on the head with a reed, and spit upon Him, and bowed their knees, and did Him homage.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
And when they had thus abused Him, they took off the purple from Him, and put his own clothes on Him, and brought Him out to crucify Him.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
And they compel one Simon a Cyrenian, the father of Alexander and Rufus, as he was passing by, coming out of the country, to carry his cross:
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
and they brought Him to a place called Golgotha, which is, being interpreted, the place of a scull.
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
And they offered Him wine mingled with myrrh to drink, but He would not take it.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
And when they had fastened Him to the cross, they parted his garments, casting lots upon them, what each of them should take.
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
And it was the third hour, when they fixed Him on the cross:
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
and the title of his charge was written over Him, THE KING OF THE JEWS.
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
And they crucified two thieves with Him, one on his right hand and one on his left:
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
so that the scripture was fulfilled, which saith, "And He was numbered with the transgressors."
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
And they that passed by reviled Him, shaking their heads and saying, Ah, thou that destroyest, the temple,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
and buildest it in three days, save thyself and come down from the cross.
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
And the chief priests likewise scoffing at Him among themselves, with the scribes, said, He saved others, Himself He cannot save: let Christ,
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
the king of Israel, come down now from the cross, that we may see and believe in Him. And even they that were crucified with Him, reviled Him.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
Now at the sixth hour there was darkness over the whole land, until the ninth hour.
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
And at the ninth hour Jesus cried out with a loud voice, saying, "Eloi, Eloi, lama sabachthani," which is being interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me?
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
And some of them that stood by hearing it, said, Behold He calleth upon Elias.
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
And there ran one, and filled a spunge with vinegar, and putting it on a reed offered it Him to drink, saying, Let Him alone, let us see whether Elias will come to take Him down.
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
But Jesus cried with a loud voice and expired.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
And the veil of the temple was rent in two from the top to the bottom.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
And when the centurion, that stood over against Him, saw that He expired with such a cry, he said, Truly this man was the Son of God.
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
There were also women at a distance looking on: among whom was Mary Magdalene, and Mary the mother of James the less and of Joses, and Salome;
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
who also when He was in Galilee, followed Him and waited on Him: and several others who came up to Jerusalem with Him.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
And the evening being now come, (because it was the preparation,
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
or the day before the sabbath, ) Joseph of Arimathea, an honorable counsellor, who also was expecting the kingdom of God, came and went in boldly to Pilate, and begged the body of Jesus.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
But Pilate wondered that He was dead already, and therefore calling for the centurion he asked him if He had been dead any time:
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
and when he heard it from the centurion, he granted the body to Joseph.
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
And he bought fine linen, and took Him down, and wrapped Him in the linen, and laid Him in a sepulchre which was hewn out of a rock; and rolled a stone to the door of the sepulchre.
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
And Mary Magdalene, and Mary the mother of Joses observed where He was laid.

< Marko 15 >