< Marko 15 >

1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
Early in the morning, the chief priests met together with the elders and scribes and the entire Jewish council. Then they bound Jesus and led him away. They handed him over to Pilate.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
Pilate asked him, “Are you the King of the Jews?” He answered him, “You say so.”
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
The chief priests were presenting many charges against Jesus.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
Pilate again asked him, “Do you give no answer? See how many charges they are bringing against you!”
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
But Jesus no longer answered Pilate, and that amazed him.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
Now at the time of the feast, Pilate usually released to them one prisoner, a prisoner they requested.
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
There with the rebels in prison, among the murderers held for their part in the rebellion, was a man named Barabbas.
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
The crowd came to Pilate and began to ask him to do for them as he had done in the past.
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
Pilate answered them and said, “Do you want me to release to you the King of the Jews?”
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
For he knew that it was because of envy that the chief priests had handed Jesus over to him.
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
But the chief priests stirred up the crowd to cry out that Barabbas should be released instead.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
Pilate answered them again and said, “What then should I do with the King of the Jews?”
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
They shouted again, “Crucify him!”
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
Pilate said to them, “What wrong has he done?” But they shouted more and more, “Crucify him.”
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
Pilate wanted to satisfy the crowd, so he released Barabbas to them. He scourged Jesus and then handed him over to be crucified.
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
The soldiers led him inside the courtyard (which is the government headquarters), and they called together the whole cohort of soldiers.
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
They put a purple robe on Jesus, and they twisted together a crown of thorns and put it on him.
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
They began to salute him and say, “Hail, King of the Jews!”
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
They struck his head with a reed staff and they spat on him. They bent their knees before him to pretend to worship him.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
When they had mocked him, they took off of him the purple robe and put his own garments on him, and then led him out to crucify him.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
A certain man, Simon of Cyrene, was coming in from the country (he was the father of Alexander and Rufus), and they forced him to carry his cross.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
The soldiers brought Jesus to the place called Golgotha (which interpreted means, “Place of a Skull”).
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
They offered him wine mixed with myrrh, but he did not drink it.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
They crucified him and divided up his garments by casting lots to determine what piece each soldier would take.
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
It was the third hour when they crucified him.
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
On a sign they wrote the charge against him, “The king of the Jews.”
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
With him they crucified two robbers, one on the right of him and one on his left.
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
Those who passed by insulted him, shaking their heads and saying, “Aha! You who would destroy the temple and rebuild it in three days,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
save yourself and come down from the cross!”
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
In the same way the chief priests were mocking him with each other, along with the scribes, and said, “He saved others, but he cannot save himself.
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
Let the Christ, the King of Israel, come down now from the cross, that we may see and believe,” and those who were crucified with him also taunted him.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
At the sixth hour, darkness came over the whole land until the ninth hour.
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
At the ninth hour Jesus cried out with a loud voice, “Eloi, Eloi, lama sabachthani?” which is interpreted, “My God, my God, why have you forsaken me?”
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
Some of those standing by heard his words and said, “Look, he is calling for Elijah.”
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
Someone ran, put sour wine on a sponge, put it on a reed staff, and gave it to him to drink. The man said, “Let us see if Elijah comes to take him down.”
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
Then Jesus cried out with a loud voice and died.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
The curtain of the temple was split in two from the top to the bottom.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
When the centurion who stood and faced Jesus saw that he had died in this way, he said, “Truly this man was the Son of God.”
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
There were also women who looked on from a distance. Among them were Mary Magdalene, Mary (the mother of James the younger and of Joses), and Salome.
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
When he was in Galilee they followed him and served him. Many other women also came up with him to Jerusalem.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
When evening had come, because it was the Day of Preparation, that is, the day before the Sabbath,
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
Joseph of Arimathea came there. He was a respected member of the council, who was waiting for the kingdom of God. He boldly went in to Pilate and asked for the body of Jesus.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
Pilate was amazed that Jesus was already dead; he called the centurion and asked him if Jesus was dead.
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
When Pilate learned from the centurion that Jesus was dead, he gave the body to Joseph.
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
Joseph had bought a linen cloth. He took him down from the cross, wrapped him in the linen cloth, and laid him in a tomb that had been cut out of a rock. Then he rolled a stone against the entrance of the tomb.
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
Mary Magdalene and Mary the mother of Joses saw the place where Jesus was buried.

< Marko 15 >