< Luka 22 >

1 Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia.
בהתקרב חג הפסח חיפשו ראשי הכוהנים והסופרים דרך להיפטר מישוע בלי לעורר מהומות בעם – דבר שפחדו ממנו מאוד.
2 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu.
3 Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili.
אז נכנס השטן ביהודה איש קריות, שהיה אחד משנים־עשר תלמידי ישוע.
4 Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu.
יהודה הלך אל ראשי הכוהנים ואל מפקדי משמר בית־המקדש כדי להתייעץ איתם כיצד להסגיר את ישוע לידיהם.
5 Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha.
ראשי הכוהנים ומפקדי משמר בית־המקדש שמחו מאוד על העזרה שהציע להם יהודה, והבטיחו לו כסף.
6 Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.
מאותה עת חיפש יהודה הזדמנות להסגיר את ישוע לידיהם, כשלא יהיה בחברת אנשים רבים.
7 Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.
בהגיע חג הפסח, ביום שבו מקריבים זבח,
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”
שלח ישוע את פטרוס ויוחנן להכין את הסדר.
9 Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”
”היכן אתה רוצה שנכין את הסעודה?“שאלו את ישוע.
10 Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.
”בכניסה לירושלים תפגשו אדם נושא כד מים“, השיב ישוע.”לכו אחריו, היכנסו אל הבית שאליו יכנס
11 Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
ואמרו לבעל הבית:’רבנו ביקש שתראה לנו את חדר האורחים אשר הכנת לו ולתלמידיו בשביל הסדר‘.
12 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”
הוא יוביל אתכם אל הקומה השנייה ויראה לכם חדר גדול שהכין למעננו. שם תכינו את הסעודה.“
13 Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
פטרוס ויוחנן הלכו העירה; הכול התרחש בדיוק כפי שאמר ישוע, והם הכינו את הסדר.
14 Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.
מאוחר יותר הגיעו ישוע ושאר התלמידים, וכשהגיעה השעה התיישבו כולם סביב השולחן.
15 Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
”נכספתי לאכול עמכם את סעודת הפסח לפני שאתייסר“, פתח ישוע ואמר:
16 Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”
”אני אומר לכם ששוב לא אוכל את סעודת הפסח, עד אשר תתקיים במלוא משמעותה במלכות האלוהים.“
17 Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.
לאחר מכן לקח ישוע כוס יין, ברך ואמר:”קחו את היין ושתו ממנו כולכם.
18 Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
”דעו לכם ששוב לא אשתה יין עד אשר תבוא מלכות האלוהים.“
19 Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
לאחר מכן הוא לקח כיכר לחם (מצה), הודה לאלוהים עליו, פרס את הלחם לפרוסות, נתן לתלמידיו ואמר:”זהו גופי הניתן בעדכם. עשו זאת לזיכרוני.“
20 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.
בתום הסעודה הגיש להם ישוע עוד כוס יין ואמר:”כוס זאת מסמלת את הברית החדשה בין אלוהים לביניכם – ברית שנחתמה בדמי.
21 Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.
אולם ליד השולחן יושב האיש שיסגיר אותי.
22 Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”
בן־האדם הולך למות כפי שנגזר עליו, אולם אני אומר לכם: אוי לו לאיש שיסגיר אותו!“
23 Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.
התלמידים החלו לשאול זה את זה מי מהם עלול לעשות מעשה נורא שכזה.
24 Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.
בין התלמידים התעורר ויכוח: מי מהם החשוב ביותר.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’
אמר להם ישוע:”בעולמנו רודים המלכים והשליטים בנתיניהם, ובכל זאת אלה נחשבים לדורשים בטוב נתיניהם.
26 Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.
אולם אצלכם המצב שונה; מי שמרבה לשרת אתכם הוא יהיה הגדול מביניכם, והמנהיג יהיה משרת.
27 Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.
ומי נחשב גדול, מי שיושב בשולחן או מי שמשרת את מי שבשולחן? כמובן שהיושב בשולחן. ואילו אני ביניכם כמשרת.
28 Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.
”מאחר ששמרתם לי אמונים על־אף הצרות והקשיים,
29 Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,
ומאחר שאבי הנחיל לי מלכות, הריני מעניק לכם בזאת את הזכות
30 ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”
לאכול ולשתות על שולחני במלכותי, ולשבת על כסאות לשפוט את שנים־עשר שבטי ישראל.“
31 Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano.
”שמעון, שמעון, “המשיך האדון,”השטן דורש את כולכם, לסנן אתכם כמו חיטה.
32 Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”
אבל התפללתי בעדך שלא תאבד את אמונתך. לאחר שתחזור בתשובה חזק את אחיך.“
33 Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”
”אדוני, “קרא שמעון פטרוס,”אני מוכן ללכת איתך לבית־הסוהר ואף למות איתך!“
34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”
אולם ישוע ענה:”פטרוס, אני אומר לך שעוד היום, לפני קריאת התרנגול, תתכחש לי שלוש פעמים ותאמר שאינך מכיר אותי כלל.
35 Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?” Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”
”כאשר שלחתי אתכם לבשר את הבשורה בלי כסף, בלי תרמיל ובלי נעליים האם חסרתם משהו?“המשיך ישוע.”לא חסר לנו דבר“, השיבו.
36 Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja.
”אבל עכשיו, “אמר להם ישוע,”למי שיש כסף ותרמיל שייקח אותם איתו; ולמי שאין חרב – שימכור את מעילו ויקנה אחת.
37 Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”
כי הגיע המועד שתתקיים הנבואה הכתובה עלי:’הוא נימנה בין פושעים‘. כן, כל מה שכתבו עלי הנביאים יתקיים במלואו.“
38 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.” Akawajibu, “Inatosha.”
”אדון, “קראו התלמידים,”יש לנו כאן שתי חרבות.“”אלה מספיקות לכם“, השיב ישוע.
39 Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
לאחר מכן יצא ישוע מהעיר והלך אל הר הזיתים, כמנהגו מדי יום, והתלמידים הלכו בעקבותיו.
40 Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
בהגיעו אל המקום אמר ישוע לתלמידיו:”התפללו שלא תבואו לידי ניסיון.“
41 Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
ישוע התרחק מתלמידיו מרחק־מה, כרע על ברכיו והתפלל:
42 akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
”אבי, אם יש ברצונך, אנא, הרחק ממני את כוס הייסורים. אולם אני רוצה שייעשה רצונך ולא רצוני!“
43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
לאחר מכן נגלה אליו מלאך מן השמים וחיזק אותו.
44 Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.
בגלל סבלו הרב הוא התפלל בדבקות רבה, וזיעתו נפלה על הארץ כטיפות דם גדולות.
45 Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni.
כאשר סיים ישוע את תפילתו וחזר אל תלמידיו, מצא אותם ישנים מרוב צער ועייפות.
46 Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”
”מדוע אתם ישנים?“שאל ישוע.”קומו והתפללו שלא תבואו לידי ניסיון.“
47 Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu.
בעודו מדבר התקרב אליו קהל גדול של אנשים ובראשם צעד יהודה, שהיה אחד מתלמידיו. יהודה קרב אל ישוע כדי לנשקו,
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”
אולם ישוע אמר לו:”יהודה, האם בנשיקה אתה עומד להסגיר את בן־האדם?“
49 Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?”
כשראו התלמידים את העומד להתרחש שאלו את ישוע:”אדון, אתה רוצה שנכה אותם בחרבות שלנו?“
50 Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.
ואחד מהם קיצץ את אוזנו הימנית של עבד הכוהן הגדול.
51 Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.
ישוע עצר בעדם ואמר:”הניחו להם לעשות את שלהם.“לאחר מכן נגע באוזנו של העבד וריפא אותה.
52 Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
ישוע פנה אל ראשי הכוהנים, מפקדי משמר בית־המקדש והזקנים שבאו לאסרו:”מדוע אתם באים אלי בחרבות ובמקלות, האם אני גנב או שודד?
53 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”
מדוע לא אסרתם אותי בבית־המקדש? הרי הייתי שם כל יום. אבל זוהי שעתכם, ושעת שלטון החושך.“
54 Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali.
הם אסרו את ישוע והובילוהו אל בית הכוהן הגדול. פטרוס הלך אחריהם במרחק־מה,
55 Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao.
אולם הצטרף אליהם כשהדליקו מדורה בחצר והתיישבו סביבה.
56 Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”
משרתת אחת הבחינה בפטרוס לאור המדורה. היא נעצה בו מבט וקראה:”האיש הזה היה עם ישוע!“
57 Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”
פטרוס הכחיש בתוקף את דבריה:”אישה, איני מכיר אותו כלל!“
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”
כעבור זמן קצר הבחין מישהו אחר בפטרוס.”אתה ודאי אחד מהם!“אמר.”מה פתאום, “הכחיש פטרוס,”אינני אחד מהם!“
59 Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”
כעבור שעה בערך העיר אדם נוסף:”אין לי ספק שהאיש הזה היה עם ישוע, כי שניהם מהגליל.“
60 Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika.
פטרוס הכחיש שוב:”בן־אדם, איני יודע על מה אתה מדבר!“לפני שסיים פטרוס את דבריו נשמעה קריאת התרנגול.
61 Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”
באותו רגע פנה ישוע והביט בעיניו של פטרוס. אז נזכר פטרוס בדברי האדון:”לפני קריאת התרנגול תתכחש לי שלוש פעמים.“
62 Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
הוא יצא מהחצר ומירר בבכי.
63 Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga.
החיילים שהופקדו על שמירת ישוע לעגו לו, הכו אותו והתעללו בו.
64 Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?”
הם קשרו את עיניו, הכו אותו באגרופים וקראו בלעג:”נביא שכמוך, נחש מי הכה אותך?“
65 Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.
הם המשיכו לקלל ולהעליב אותו.
66 Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao.
למחרת בבוקר הובא ישוע לפני חברי הסנהדרין, ראשי הכוהנים, הסופרים וזקני העם.
67 Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo, tuambie.” Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini.
”האם אתה באמת המשיח?“שאלו אותו. אך ישוע השיב:”אם אגיד לכם, לא תאמינו לי,
68 Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.
ואם אשאל אתכם שאלות לא תשיבו לי.
69 Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”
אולם עוד מעט בן־האדם ישב לימין גבורת האלוהים.“
70 Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”
”אם כך, בן־אלוהים אתה?“”אתם אמרתם שאני הוא“השיב ישוע.
71 Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”
”איננו זקוקים לעדויות נוספות!“הם קראו.”במו אוזנינו שמענו אותו אומר דברים אלה!“

< Luka 22 >