< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
Ker so že mnogi vzeli v roko, da po vrsti uredijo izjavo o teh stvareh, ki se najbolj gotovo verjamejo med nami,
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
celo kakor so nam jih izročili [tisti], ki so bili od začetka priče in služabniki besede,
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
se je tudi meni zdelo dobro, od samega začetka imeti popolno razumevanje o vseh stvareh, da tebi, nadvse odlični Teófil, napišem po vrsti,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
da lahko spoznaš zanesljivost o teh besedah, o katerih si bil poučen.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
V dneh Heroda, judejskega kralja, je bil nek duhovnik, imenovan Zaharija, iz Abíjeve skupine, in njegova žena je bila izmed Aronovih hčera in njeno ime je bilo Elizabeta.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
Oba sta bila pravična pred Bogom in sta brez krivde živela po vseh Gospodovih zapovedih in odredbah.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
Ker je bila Elizabeta jalova nista imela nobenega otroka in oba sta bila zelo zvrhana v letih.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
In pripetilo se je, medtem ko je pred Bogom opravljal duhovniško službo, po vrstnem redu svoje skupine,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
glede na navado duhovniške službe, je bil na njem žreb, da zažge kadilo, ko je odšel v Gospodov tempelj.
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
Celotna množica ljudi pa je ob času zažiganja kadila zunaj molila.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
In prikazal se mu je Gospodov angel, stoječ na desni strani kadilnega oltarja.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
Ko pa ga je Zaharija zagledal, se je vznemiril in strah ga je spreletel.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
Toda angel mu je rekel: »Ne boj se, Zaharija, kajti tvoja molitev je uslišana in tvoja žena Elizabeta ti bo rodila sina in ti boš klical njegovo ime Janez.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
Imel boš radost in veselje in mnogi se bodo veselili ob njegovem rojstvu.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
Kajti velik bo v Gospodovih očeh in ne bo pil niti vina niti močne pijače in celó od maternice svoje matere bo izpolnjen s Svetim Duhom.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
In mnoge izmed Izraelovih otrok bo obrnil h Gospodu, njihovemu Bogu.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
Pred njim bo šel z Elijevim duhom in močjo, da obrne srca očetov k otrokom in neposlušne k modrosti pravičnih; da pripravi ljudstvo, pripravljeno za Gospoda.«
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
Zaharija je angelu rekel: »Po čem bom to spoznal? Kajti starec sem in moja žena je zelo zvrhana v letih.«
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
Angel mu odgovori in reče: »Jaz sem Gabriel, ki stojim v prisotnosti Boga in poslan sem, da ti govorim in da ti pokažem te vesele novice.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
Glej, ker nisi verjel mojim besedam, ki se bodo uresničile ob njihovem pravem času, boš postal nem in ne boš mogel govoriti do dne, ko se bodo te besede izpolnile.«
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
In ljudje so čakali na Zaharija in se čudili, da se je tako dolgo mudil v templju.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
Ko pa je prišel ven, jim ni mogel spregovoriti, in zaznali so, da je videl v templju videnje, kajti dajal jim je znamenja, ostal pa je brez besed.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
Pripetilo se je, kakor hitro so bili dnevi njegovega služenja dovršeni, da se je odpravil k svoji lastni hiši.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
Po teh dneh je njegova žena Elizabeta spočela in se pet mesecev skrivala, rekoč:
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
»Tako je Gospod ravnal z menoj v dneh, v katerih je pogledal name, da odvzame mojo grajo izmed ljudi.«
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
V šestem mesecu pa je bil od Boga poslan angel Gabriel v galilejsko mesto, imenovano Nazaret,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
k devici, zaročeni z možem, katerega ime je bilo Jožef, iz Davidove hiše; in devici je bilo ime Marija.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
Angel je vstopil k njej in rekel: »Pozdravljena, ti, ki si zelo spoštovana, Gospod je s teboj, blagoslovljena si med ženskami.«
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
Ko pa ga je zagledala, je bila ob njegovem govoru zaskrbljena in v svojih mislih preudarjala, kakšne vrste pozdrav naj bi to bil.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
Angel ji je rekel: »Ne boj se, Marija, kajti pri Bogu si našla naklonjenost.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
Glej, v svoji maternici boš spočela in rodila sina in njegovo ime boš klicala JEZUS.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
Velik bo in imenovan bo Sin Najvišjega; in Gospod Bog mu bo dal prestol njegovega očeta Davida
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
in nad Jakobovo hišo bo vladal večno in njegovemu kraljestvu ne bo konca.« (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Potem je Marija rekla angelu: »Kako se bo to zgodilo, glede na to, da ne poznam moškega?«
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
Angel je odgovoril in ji rekel: »Sveti Duh bo prišel nadte in moč Najvišjega te bo obsenčila, zato bo tudi ta sveta oseba, ki bo rojena od tebe, imenovana Božji Sin.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
Glej, tvoja sestrična Elizabeta je prav tako v svoji visoki starosti spočela sina, in to je šesti mesec z njo, ki je bila imenovana jalova.
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
Kajti z Bogom nič ne bo nemogoče.«
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
Marija je rekla: »Glej, Gospodova pomočnica; naj se mi zgodi glede na tvojo besedo.« In angel je odšel od nje.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
Marija je v tistih dneh vstala in z naglico odšla v hribovito deželo, v Judovo mesto
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
in vstopila v Zaharijevo hišo ter pozdravila Elizabeto.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
In pripetilo se je, ko je Elizabeta zaslišala Marijin pozdrav, da je dete poskočilo v njeni maternici in Elizabeta je bila izpolnjena s Svetim Duhom
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
in zaklicala z močnim glasom ter rekla: »Blagoslovljena si ti med ženskami in blagoslovljen je sad tvoje maternice.
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
Od kod je meni to, da bi prišla k meni mati mojega Gospoda?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
Kajti glej, brž ko je glas tvojega pozdrava zazvenel v mojih ušesih, je dete v moji maternici od radosti poskočilo.
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
Blagoslovljena je tista, ki je verovala, kajti izpolnile se bodo te besede, ki so ji bile povedane od Gospoda.«
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
Marija je rekla: »Moja duša poveličuje Gospoda
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
in moj duh se veseli v Bogu, mojem Odrešeniku.
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
Kajti ozrl se je na nizek stan svoje pomočnice, kajti glej, odslej me bodo vsi rodovi imenovali blagoslovljeno.
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
Kajti tisti, ki je mogočen, mi je storil velike stvari in sveto je njegovo ime.
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
In njegovo usmiljenje je od roda do roda nad tistimi, ki se ga bojijo.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
S svojim laktom je pokazal moč, ponosne je razgnal v domišljiji njihovih src.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
Mogočne je odstranil z njihovih prestolov in povišal te z nizkim položajem.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
Lačne je napolnil z dobrinami, bogate pa je odpustil prazne.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
Pomagal je svojemu služabniku Izraelu, v spomin na svoje usmiljenje,
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
kakor je govoril našim očetom, Abrahamu in njegovemu semenu na veke.« (aiōn g165)
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
Marija je z njo ostala približno tri mesece in se vrnila v svojo lastno hišo.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Torej prišel je Elizabetin polni čas, ko naj bi rodila; in rodila je sina.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
Njeni sosedje in njeni sorodniki so slišali, kako je Gospod nad njo izkazal veliko usmiljenje in veselili so se z njo.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
Pripetilo pa se je, da so na osmi dan prišli, da obrežejo otroka in poimenovali so ga Zaharija, po imenu njegovega očeta.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
Njegova mati pa je odgovorila in rekla: »Ne tako, temveč se bo imenoval Janez.«
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
Oni pa so ji rekli: »Nikogar v tvojem sorodstvu ni, ki je poimenovan s tem imenom.«
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
In naredili so znamenja njegovemu očetu, kako bi ga on imenoval.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
In prosil je za pisalno deščico ter napisal, rekoč: »Njegovo ime je Janez.« In vsi so se čudili.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
In njegova usta so se takoj odprla in njegov jezik se je sprostil in spregovoril je ter hvalil Boga.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
In strah je prišel na vse, ki so prebivali naokoli njih; in vse te besede so se razglasile naokoli po vsej judejski hriboviti deželi.
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
In vsi, ki so jih slišali, so si jih položili v svoja srca, rekoč: »Kakšne vrste otrok bo to!« In Gospodova roka je bila z njim.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
In njegov oče Zaharija je bil izpolnjen s Svetim Duhom in prerokoval, rekoč:
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
»Blagoslovljen bodi Gospod, Izraelov Bog; kajti obiskal je in odkupil svoje ljudi
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
in za nas je dvignil rog rešitve duš v hiši svojega služabnika Davida,
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
kakor je govoril po ustih svojih svetih prerokov, ki so bili, odkar je svet nastal, (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
da bi bili mi lahko rešeni pred našimi sovražniki in iz roke vseh, ki nas sovražijo,
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
da opravi usmiljenje, obljubljeno našim očetom in se spomni svoje svete zaveze,
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
prisege, s katero je prisegel našemu očetu Abrahamu,
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
da nam bo zagotovil, da mu bomo osvobojeni iz roke svojih sovražnikov, lahko služili brez strahu,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
v svetosti in pravičnosti pred njim, vse dni našega življenja.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
Ti pa, otrok, boš imenovan prerok Najvišjega, kajti šel boš pred Gospodov obraz, da pripraviš njegove poti,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
da daš njegovim ljudem spoznanje o rešitvi duš z odpuščanjem njihovih grehov,
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
po nežnem usmiljenju našega Boga; po katerem nas je obiskalo svitanje od zgoraj,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
da da svetlobo tem, ki sedijo v temi in v smrtni senci, da vodi naša stopala na pot miru.«
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
Otrok pa je rasel in se krepil v duhu in bil je v puščavah do dneva njegove pojavitve Izraelu.

< Luka 1 >