< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
prathamatO yE sAkSiNO vAkyapracArakAzcAsan tE'smAkaM madhyE yadyat sapramANaM vAkyamarpayanti sma
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
tadanusAratO'nyEpi bahavastadvRttAntaM racayituM pravRttAH|
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
ataEva hE mahAmahimathiyaphil tvaM yA yAH kathA azikSyathAstAsAM dRPhapramANAni yathA prApnOSi
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
tadarthaM prathamamArabhya tAni sarvvANi jnjAtvAhamapi anukramAt sarvvavRttAntAn tubhyaM lEkhituM matimakArSam|
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
yihUdAdEzIyahErOdnAmakE rAjatvaM kurvvati abIyayAjakasya paryyAyAdhikArI sikhariyanAmaka EkO yAjakO hArONavaMzOdbhavA ilIzEvAkhyA
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
tasya jAyA dvAvimau nirdOSau prabhOH sarvvAjnjA vyavasthAzca saMmanya IzvaradRSTau dhArmmikAvAstAm|
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
tayOH santAna EkOpi nAsIt, yata ilIzEvA bandhyA tau dvAvEva vRddhAvabhavatAm|
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
yadA svaparyyAnukramENa sikhariya IzvAsya samakSaM yAjakIyaM karmma karOti
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
tadA yajnjasya dinaparipAyyA paramEzvarasya mandirE pravEzakAlE dhUpajvAlanaM karmma tasya karaNIyamAsIt|
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
taddhUpajvAlanakAlE lOkanivahE prArthanAM kartuM bahistiSThati
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
sati sikhariyO yasyAM vEdyAM dhUpaM jvAlayati taddakSiNapArzvE paramEzvarasya dUta Eka upasthitO darzanaM dadau|
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
taM dRSTvA sikhariya udvivijE zazagkE ca|
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
tadA sa dUtastaM babhASE hE sikhariya mA bhaistava prArthanA grAhyA jAtA tava bhAryyA ilIzEvA putraM prasOSyatE tasya nAma yOhan iti kariSyasi|
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
kinjca tvaM sAnandaH saharSazca bhaviSyasi tasya janmani bahava AnandiSyanti ca|
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
yatO hEtOH sa paramEzvarasya gOcarE mahAn bhaviSyati tathA drAkSArasaM surAM vA kimapi na pAsyati, aparaM janmArabhya pavitrENAtmanA paripUrNaH
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
san isrAyElvaMzIyAn anEkAn prabhOH paramEzvarasya mArgamAnESyati|
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
santAnAn prati pitRNAM manAMsi dharmmajnjAnaM pratyanAjnjAgrAhiNazca parAvarttayituM, prabhOH paramEzvarasya sEvArtham EkAM sajjitajAtiM vidhAtunjca sa EliyarUpAtmazaktiprAptastasyAgrE gamiSyati|
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
tadA sikhariyO dUtamavAdIt kathamEtad vEtsyAmi? yatOhaM vRddhO mama bhAryyA ca vRddhA|
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
tatO dUtaH pratyuvAca pazyEzvarasya sAkSAdvarttI jibrAyElnAmA dUtOhaM tvayA saha kathAM gadituM tubhyamimAM zubhavArttAM dAtunjca prESitaH|
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
kintu madIyaM vAkyaM kAlE phaliSyati tat tvayA na pratItam ataH kAraNAd yAvadEva tAni na sEtsyanti tAvat tvaM vaktuMmazaktO mUkO bhava|
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
tadAnIM yE yE lOkAH sikhariyamapaikSanta tE madhyEmandiraM tasya bahuvilambAd AzcaryyaM mEnirE|
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
sa bahirAgatO yadA kimapi vAkyaM vaktumazaktaH sagkEtaM kRtvA niHzabdastasyau tadA madhyEmandiraM kasyacid darzanaM tEna prAptam iti sarvvE bubudhirE|
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
anantaraM tasya sEvanaparyyAyE sampUrNE sati sa nijagEhaM jagAma|
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
katipayadinESu gatESu tasya bhAryyA ilIzEvA garbbhavatI babhUva
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
pazcAt sA panjcamAsAn saMgOpyAkathayat lOkAnAM samakSaM mamApamAnaM khaNPayituM paramEzvarO mayi dRSTiM pAtayitvA karmmEdRzaM kRtavAn|
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
aparanjca tasyA garbbhasya SaSThE mAsE jAtE gAlIlpradEzIyanAsaratpurE
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
dAyUdO vaMzIyAya yUSaphnAmnE puruSAya yA mariyamnAmakumArI vAgdattAsIt tasyAH samIpaM jibrAyEl dUta IzvarENa prahitaH|
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
sa gatvA jagAda hE IzvarAnugRhItakanyE tava zubhaM bhUyAt prabhuH paramEzvarastava sahAyOsti nArINAM madhyE tvamEva dhanyA|
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
tadAnIM sA taM dRSTvA tasya vAkyata udvijya kIdRzaM bhASaNamidam iti manasA cintayAmAsa|
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
tatO dUtO'vadat hE mariyam bhayaM mAkArSIH, tvayi paramEzvarasyAnugrahOsti|
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
pazya tvaM garbbhaM dhRtvA putraM prasOSyasE tasya nAma yIzuriti kariSyasi|
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
sa mahAn bhaviSyati tathA sarvvEbhyaH zrESThasya putra iti khyAsyati; aparaM prabhuH paramEzvarastasya piturdAyUdaH siMhAsanaM tasmai dAsyati;
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
tathA sa yAkUbO vaMzOpari sarvvadA rAjatvaM kariSyati, tasya rAjatvasyAntO na bhaviSyati| (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
tadA mariyam taM dUtaM babhASE nAhaM puruSasaggaM karOmi tarhi kathamEtat sambhaviSyati?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
tatO dUtO'kathayat pavitra AtmA tvAmAzrAyiSyati tathA sarvvazrESThasya zaktistavOpari chAyAM kariSyati tatO hEtOstava garbbhAd yaH pavitrabAlakO janiSyatE sa Izvaraputra iti khyAtiM prApsyati|
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
aparanjca pazya tava jnjAtirilIzEvA yAM sarvvE bandhyAmavadan idAnIM sA vArddhakyE santAnamEkaM garbbhE'dhArayat tasya SaSThamAsObhUt|
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
kimapi karmma nAsAdhyam Izvarasya|
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
tadA mariyam jagAda, pazya prabhErahaM dAsI mahyaM tava vAkyAnusArENa sarvvamEtad ghaTatAm; ananataraM dUtastasyAH samIpAt pratasthE|
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
atha katipayadinAt paraM mariyam tasmAt parvvatamayapradEzIyayihUdAyA nagaramEkaM zIghraM gatvA
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
sikhariyayAjakasya gRhaM pravizya tasya jAyAm ilIzEvAM sambOdhyAvadat|
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
tatO mariyamaH sambOdhanavAkyE ilIzEvAyAH karNayOH praviSTamAtrE sati tasyA garbbhasthabAlakO nanartta| tata ilIzEvA pavitrENAtmanA paripUrNA satI
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
prOccairgaditumArEbhE, yOSitAM madhyE tvamEva dhanyA, tava garbbhasthaH zizuzca dhanyaH|
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
tvaM prabhOrmAtA, mama nivEzanE tvayA caraNAvarpitau, mamAdya saubhAgyamEtat|
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
pazya tava vAkyE mama karNayOH praviSTamAtrE sati mamOdarasthaH zizurAnandAn nanartta|
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
yA strI vyazvasIt sA dhanyA, yatO hEtOstAM prati paramEzvarOktaM vAkyaM sarvvaM siddhaM bhaviSyati|
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
tadAnIM mariyam jagAda| dhanyavAdaM parEzasya karOti mAmakaM manaH|
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
mamAtmA tArakEzE ca samullAsaM pragacchati|
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
akarOt sa prabhu rduSTiM svadAsyA durgatiM prati| pazyAdyArabhya mAM dhanyAM vakSyanti puruSAH sadA|
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
yaH sarvvazaktimAn yasya nAmApi ca pavitrakaM| sa Eva sumahatkarmma kRtavAn mannimittakaM|
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
yE bibhyati janAstasmAt tESAM santAnapaMktiSu| anukampA tadIyA ca sarvvadaiva sutiSThati|
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
svabAhubalatastEna prAkAzyata parAkramaH| manaHkumantraNAsArddhaM vikIryyantE'bhimAninaH|
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
siMhAsanagatAllOkAn balinazcAvarOhya saH| padESUccESu lOkAMstu kSudrAn saMsthApayatyapi|
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
kSudhitAn mAnavAn dravyairuttamaiH paritarpya saH| sakalAn dhaninO lOkAn visRjEd riktahastakAn|
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
ibrAhImi ca tadvaMzE yA dayAsti sadaiva tAM| smRtvA purA pitRNAM nO yathA sAkSAt pratizrutaM| (aiōn g165)
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
isrAyElsEvakastEna tathOpakriyatE svayaM||
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
anantaraM mariyam prAyENa mAsatrayam ilIzEvayA sahOSitvA vyAghuyya nijanivEzanaM yayau|
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
tadanantaram ilIzEvAyAH prasavakAla upasthitE sati sA putraM prAsOSTa|
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
tataH paramEzvarastasyAM mahAnugrahaM kRtavAn Etat zrutvA samIpavAsinaH kuTumbAzcAgatya tayA saha mumudirE|
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
tathASTamE dinE tE bAlakasya tvacaM chEttum Etya tasya pitRnAmAnurUpaM tannAma sikhariya iti karttumISuH|
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
kintu tasya mAtAkathayat tanna, nAmAsya yOhan iti karttavyam|
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
tadA tE vyAharan tava vaMzamadhyE nAmEdRzaM kasyApi nAsti|
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
tataH paraM tasya pitaraM sikhariyaM prati sagkEtya papracchuH zizOH kiM nAma kAriSyatE?
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
tataH sa phalakamEkaM yAcitvA lilEkha tasya nAma yOhan bhaviSyati| tasmAt sarvvE AzcaryyaM mEnirE|
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
tatkSaNaM sikhariyasya jihvAjAPyE'pagatE sa mukhaM vyAdAya spaSTavarNamuccAryya Izvarasya guNAnuvAdaM cakAra|
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
tasmAccaturdiksthAH samIpavAsilOkA bhItA EvamEtAH sarvvAH kathA yihUdAyAH parvvatamayapradEzasya sarvvatra pracAritAH|
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
tasmAt zrOtArO manaHsu sthApayitvA kathayAmbabhUvuH kIdRzOyaM bAlO bhaviSyati? atha paramEzvarastasya sahAyObhUt|
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
tadA yOhanaH pitA sikhariyaH pavitrENAtmanA paripUrNaH san EtAdRzaM bhaviSyadvAkyaM kathayAmAsa|
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
isrAyElaH prabhu ryastu sa dhanyaH paramEzvaraH| anugRhya nijAllOkAn sa Eva parimOcayEt|
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
vipakSajanahastEbhyO yathA mOcyAmahE vayaM| yAvajjIvanjca dharmmENa sAralyEna ca nirbhayAH|
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
sEvAmahai tamEvaikam EtatkAraNamEva ca| svakIyaM supavitranjca saMsmRtya niyamaM sadA|
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
kRpayA puruSAn pUrvvAn nikaSArthAttu naH pituH| ibrAhImaH samIpE yaM zapathaM kRtavAn purA|
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
tamEva saphalaM karttaM tathA zatrugaNasya ca| RtIyAkAriNazcaiva karEbhyO rakSaNAya naH|
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
sRSTEH prathamataH svIyaiH pavitrai rbhAvivAdibhiH| (aiōn g165)
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
yathOktavAn tathA svasya dAyUdaH sEvakasya tu|
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
vaMzE trAtAramEkaM sa samutpAditavAn svayam|
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
atO hE bAlaka tvantu sarvvEbhyaH zrESTha Eva yaH| tasyaiva bhAvivAdIti pravikhyAtO bhaviSyasi| asmAkaM caraNAn kSEmE mArgE cAlayituM sadA| EvaM dhvAntE'rthatO mRtyOzchAyAyAM yE tu mAnavAH|
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
upaviSTAstu tAnEva prakAzayitumEva hi| kRtvA mahAnukampAM hi yAmEva paramEzvaraH|
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
UrdvvAt sUryyamudAyyaivAsmabhyaM prAdAttu darzanaM| tayAnukampayA svasya lOkAnAM pApamOcanE|
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
paritrANasya tEbhyO hi jnjAnavizrANanAya ca| prabhO rmArgaM pariSkarttuM tasyAgrAyI bhaviSyasi||
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
atha bAlakaH zarIrENa buddhyA ca varddhitumArEbhE; aparanjca sa isrAyElO vaMzIyalOkAnAM samIpE yAvanna prakaTIbhUtastAstAvat prAntarE nyavasat|

< Luka 1 >