< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
Forasmuch as many haue taken in hand to set foorth the storie of those things, whereof we are fully persuaded,
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
As they haue deliuered them vnto vs, which from the beginning saw them their selues, and were ministers of ye word,
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
It seemed good also to me (most noble Theophilus) assoone as I had searched out perfectly all things from the beginning, to write vnto thee thereof from point to point,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
That thou mightest acknowledge the certaintie of those things, whereof thou hast bene instructed.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
In the time of Herod King of Iudea, there was a certaine Priest named Zacharias, of the course of Abia: and his wife was of the daughters of Aaron, and her name was Elisabet.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
Both were iust before God, and walked in all the commandements and ordinances of the Lord, without reproofe.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
And they had no childe, because that Elisabet was barren: and both were well stricken in age.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
And it came to passe, as he executed the Priestes office before God, as his course came in order,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
According to the custome of the Priests office, his lot was to burne incense, when he went into the Temple of the Lord.
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
And the whole multitude of the people were without in prayer, while the incense was burning.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
Then appeared vnto him an Angel of the Lord standing at the right side of the altar of incense.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
And when Zacharias sawe him, he was troubled, and feare fell vpon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
But the Angel saide vnto him, Feare not, Zacharias: for thy prayer is heard, and thy wise Elisabet shall beare thee a sonne, and thou shalt call his name Iohn.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
And thou shalt haue ioy and gladnes, and many shall reioyce at his birth.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
For he shalbe great in the sight of the Lord, and shall neither drinke wine, nor strong drinke: and he shalbe filled with the holy Ghost, euen from his mothers wombe.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
And many of the children of Israel shall he turne to their Lord God.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
For he shall goe before him in the spirite and power of Elias, to turne the hearts of the fathers to the children, and the disobedient to the wisedome of the iust men, to make ready a people prepared for the Lord.
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
Then Zacharias said vnto ye Angel, Whereby shall I knowe this? for I am an olde man, and my wife is of a great age.
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
And the Angell answered, and sayde vnto him, I am Gabriel that stand in the presence of God, and am sent to speake vnto thee, and to shew thee these good tidings.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
And beholde, thou shalt be domme, and not be able to speake, vntill the day that these things be done, because thou beleeuedst not my words, which shalbe fulfilled in their season.
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
Now the people waited for Zacharias, and marueiled that he taried so long in the Temple.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
And when hee came out, hee coulde not speake vnto them: then they perceiued that hee had seene a vision in the Temple: For he made signes vnto them, and remained domme.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
And it came to passe, when the daies of his office were fulfilled, that he departed to his owne house.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
And after those daies, his wife Elisabet conceiued, and hid her selfe fiue moneths, saying,
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
Thus hath the Lord dealt with me, in the daies wherein he looked on me, to take from me my rebuke among men.
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
And in the sixth moneth, the Angell Gabriel was sent from God vnto a citie of Galile, named Nazareth,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
To a virgin affianced to a man whose name was Ioseph, of the house of Dauid, and the virgins name was Marie.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
And the Angel went in vnto her, and said, Haile thou that art freely beloued: the Lord is with thee: blessed art thou among women.
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
And when she saw him, she was troubled at his saying, and thought what maner of salutation that should be.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
Then the Angel saide vnto her, Feare not, Marie: for thou hast found fauour with God.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
For loe, thou shalt conceiue in thy wobe, and beare a sonne, and shalt call his name Iesus.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
He shall be great, and shall be called the Sonne of the most High, and the Lord God shall giue vnto him the throne of his father Dauid.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
And hee shall reigne ouer the house of Iacob for euer, and of his kingdome shall bee none ende. (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Then sayde Marie vnto the Angel, How shall this be, seeing I knowe not man?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
And the Angel answered, and said vnto her, The holy Ghost shall come vpon thee, and the power of the most High shall ouershadowe thee: therefore also that holy thing which shall bee borne of thee, shall be called the Sonne of God.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
And behold, thy cousin Elisabet, she hath also conceiued a sonne in her olde age: and this is her sixt moneth, which was called barren.
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
For with God shall nothing be vnpossible.
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
Then Marie said, Behold the seruant of the Lord: be it vnto me according to thy woorde. So the Angel departed from her.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
And Marie arose in those daies, and went into ye hil countrey with hast to a citie of Iuda,
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
And entred into the house of Zacharias, and saluted Elisabet.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
And it came to passe, as Elisabet heard the salutation of Marie, the babe sprang in her bellie, and Elisabet was filled with the holy Ghost.
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
And she cried with a loud voice, and saide, Blessed art thou among women, because the fruit of thy wombe is blessed.
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
And whence commeth this to mee, that the mother of my Lord should come to me?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
For loe, assoone as the voice of thy salutation sounded in mine eares, the babe sprang in my bellie for ioye,
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
And blessed is shee that beleeued: for those things shall be perfourmed, which were tolde her from the Lord.
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
Then Marie sayde, My soule magnifieth the Lord,
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
And my spirite reioyceth in God my Sauiour.
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
For hee hath looked on the poore degree of his seruaunt: for beholde, from henceforth shall all ages call me blessed,
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
Because hee that is mightie, hath done for me great things, and holy is his Name.
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
And his mercie is from generation to generation on them that feare him.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
Hee hath shewed strength with his arme: hee hath scattered the proude in the imagination of their hearts.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
Hee hath put downe the mighty from their seates, and exalted them of lowe degree.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
Hee hath filled the hungrie with good things, and sent away the rich emptie.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
Hee hath vpholden Israel his seruaunt to be mindefull of his mercie
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
(As hee hath spoken to our fathers, to wit, to Abraham, and his seede) for euer. (aiōn g165)
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
And Marie abode with her about three moneths: after, shee returned to her owne house.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Nowe Elisabets time was fulfilled, that shee should be deliuered, and shee brought foorth a sonne.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
And her neighbours, and cousins heard tell howe the Lord had shewed his great mercie vpon her, and they reioyced with her.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
And it was so that on the eight day they came to circumcise the babe, and called him Zacharias after the name of his father.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
But his mother answered, and saide, Not so, but he shalbe called Iohn.
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
And they saide vnto her, There is none of thy kindred, that is named with this name.
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
Then they made signes to his father, howe he would haue him called.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
So hee asked for writing tables, and wrote, saying, His name is Iohn, and they marueiled all.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
And his mouth was opened immediately, and his tongue, and he spake and praised God.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
Then feare came on all them that dwelt neere vnto them, and all these woordes were noised abroade throughout all the hill countrey of Iudea.
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
And al they that heard them, laid them vp in their hearts, saying, What maner childe shall this be! and the hand of the Lord was with him.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
Then his father Zacharias was filled with the holy Ghost, and prophesied, saying,
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
Blessed be the Lord God of Israel, because he hath visited and redeemed his people,
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
And hath raised vp the horne of saluation vnto vs, in the house of his seruant Dauid,
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
As he spake by ye mouth of his holy Prophets, which were since the world began, saying, (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
That he would sende vs deliuerance from our enemies, and from the hands of all that hate vs,
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
That he might shewe mercie towards our fathers, and remember his holy couenant,
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
And the othe which he sware to our father Abraham.
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
Which was, that he would graunt vnto vs, that we being deliuered out of the handes of our enemies, should serue him without feare,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
All the daies of our life, in holinesse and righteousnesse before him.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
And thou, babe, shalt be called the Prophet of the most High: for thou shalt goe before the face of the Lord, to prepare his waies,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
And to giue knowledge of saluation vnto his people, by the remission of their sinnes,
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
Through ye tender mercy of our God, wherby the day spring from an hie hath visited vs,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
To giue light to them that sit in darknes, and in the shadow of death, and to guide our feete into the way of peace.
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
And the childe grewe, and waxed strong in spirit, and was in the wildernesse, til the day came that he should shewe him selfe vnto Israel.

< Luka 1 >