< Luka 1 >

1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
如你所知,很多人都曾试图用文字记录我们参与的成就。
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
他们所记录的证据,来自最早见证和传递上帝讯息之人。
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
由于我从始至终都参与其中,所以应该可以准确无误地撰写所发生的一切。
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
敬爱的提阿非罗们,我之所以这么做,是为了让你们确认自己所学之道完全值得信赖。
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
希律担任犹太王的那段时间,亚比雅班里有一位名叫撒迦利亚的祭司,他妻子以利沙伯是亚伦的后人。
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
他们的一举一动都遵循上帝正道,严格遵守主所立下的一切诫命规条。
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
但他们没有孩子,因为以利沙伯无法生育,而且二人都年岁已高。。
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
有一天,撒迦利亚按照排班的时间履行作为上帝祭司的职责,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
照惯例抽签后,他被选中进入主的神庙上香。
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
在烧香的过程,众人都在外面祈祷。
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
这时天使向撒迦利亚显化,立于香坛的右侧。
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
撒迦利亚见状颇感惊慌,非常害怕。
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
天使说:“撒迦利亚,别害怕,上帝听到了你的祈求。你妻子以利沙伯将为你生下一子,你将为他起名为约翰。
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
这孩子会为你带来欢喜和快乐,许多人都会来庆祝他的降生。
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
他将成为主面前的尊者,滴酒不沾,未降生之前便有圣灵附体。
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
他将带领众多以色列人,回到主、也就是他们的上帝身边。
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
他将以以利亚的圣灵和力量走在前,劝说父亲们关爱自己的儿女,规劝悖逆之人走正道,让民众准备好迎接主。”
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
撒迦利亚问天使:“我要如何相信这一切?我老了,我妻子也是一把年纪。”
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
天使回答:“我是上帝面前的加百列,奉命向你传话,告诉你这个好消息。
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
但你并不相信我所说的一切,所以你会失语,直到我所言之事成真,你才能开口说话。”
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
众人正在外面等候撒迦利亚,见他迟迟未从神庙出来,很是奇怪。
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
但他出来时却真的失语了,无法讲话,只能打手势。于是众人意识到刚才在神庙中出现了神迹。
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
他完成自己的职责后便回了家。
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
几天后,他妻子以利沙伯果真怀孕,在家中待了五个月。
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
她说:“这一切是主的旨意,他这样待我,便是要让我不再在世人面前感到羞辱。”
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
在怀孕的第六个月,上帝派天使加百列来到加利利的拿撒勒镇,现身在一个名叫玛利亚的少女面前。
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
玛利亚当时已与一位名叫约瑟夫的男人订婚。
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
天使向她问候,然后对她说“你很幸运,主与你同在。”
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
玛利亚对此颇感困惑,不知道这问候到底意味着什么。
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
天使说:“玛利亚,不要怕!因为上帝已对你施以恩典。
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
你将怀孕生子,那婴儿将起名叫耶稣。
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
他将成为一位伟人,被称为至高上帝之子,上帝将把向其赐予祖先大卫的王位,
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
他将永远统治雅各的家园,他的王国将永续存在。” (aiōn g165)
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
玛利亚问天使:“但这怎能可能?我还是处女。”
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
天使回答:“圣灵将降临于你,至高上帝将笼罩于你。那即将诞下的婴儿生而神圣,将被称为上帝之子。
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
甚至连你的亲戚以利沙伯都怀孕了,人们说那女人无法生育,现在怀胎已有六个月。
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
对于上帝而言,一切皆有可能。”
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
玛利亚说:“我听你的,随时准备服侍上帝,愿你所言的事情发生在我身上。”于是天使便离开了。
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
稍后,玛利亚准备了一下便急忙赶去犹太山地的一座城市,
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
来到撒迦利亚的家。她走进屋向以利沙伯问安。
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
听见玛利亚的问候,以利沙伯腹中的婴儿立刻开始跳动,表达着喜悦。圣灵注入了以利沙伯的体内,
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
于是她高声说:“你是一位如此有福的女人,你腹中的婴儿能由你诞下,也是一种福气!
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
我太荣幸了,我主之母能够造访我的寒舍。
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
听到你问候的那一刻,我腹中的婴儿就欢喜跳跃。
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
你真荣幸,因为你已确信,主将把对你的承诺变为现实!”
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
玛利亚说:“赞美主!
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
上帝救世主让我如此欢喜,
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
因为我作为他的仆人,尽管身世卑微,他却决定垂青于我。今后万代都会认为我是获得赐福之人。
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
全能上帝对我做出伟大之举,他的名字如此神圣。
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
他的怜悯将在尊敬他的世界中传递。
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
他凭借其力量,击败了那些自作聪明之人。
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
他能够让位高权重之人跌落王位,让谦卑之人获得升华,
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
他让饥肠辘辘之人饱餐美食,也让富足之人两手空空。
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
在他的帮助下,他的仆人以色列将永记他的怜悯, (aiōn g165)
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
正如他向我们先父、亚伯拉罕及其后裔所做的承诺。”
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
玛利亚和以利沙伯同住了三个月,然后便返回自己的家。
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
以利沙伯终于诞下一名男婴。
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
邻居和亲戚们得知主向她施以如此善意,便和她一同庆祝。
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
到了第八天,他们前来为孩子行割礼,打算让他随父亲的名字叫撒迦利亚。
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
但以利沙伯说:“不要,他应该叫做约翰。”
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
众人回答:“但你的亲戚中并没有这样的名字。”
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
他们通过手势询问孩子的父亲撒迦利亚,询问他的意见。
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
撒迦利亚示意要写字。令众人诧异的是,他写下的是:“他就叫约翰。”
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
忽然他再次开口说话了,开始赞美上帝。
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
这一切让住在周围的人心生敬畏,这个消息很快就传遍整个犹太山地。
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
众人听闻此事便思量它的含义:“这孩子将会成为怎样的人?”因为很显然,他对上帝而言非常特别。
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
婴儿的父亲撒迦利亚体内充满了圣灵,他预言道:
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
“主就是以色列的上帝,他如此伟大,因为他降临到子民之中,为其赋予自由,
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
他向其仆人大卫的家族赐予伟大的救赎,
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
正如他自古以来借由其神圣先知所传达的预言。 (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
他承诺拯救我们摆脱敌人,远离那些憎恨我们的人。
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
他怜悯我们的祖先,记得他的圣约,
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
那是他向我们的祖先亚伯拉罕所发誓言。
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
他让我们摆脱恐惧,从敌人手中拯救我们,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
这让我们可以毕生遵循正道并服侍于他。
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
尽管你现在只是一个婴儿,但却会被称为至高上帝的先知,因你将先于主之前,为他铺好道路,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
通过宽恕其子民的罪,传播救赎的讯息。
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
蒙上帝对我们的关爱怜悯,天堂的黎明将降临照耀我们,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
照亮那些活在黑暗中、笼罩在死亡阴影中的人,引导我们走上平安之路。”
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
这个叫做约翰的男孩逐渐长大,精神变得很强大。他一直住在荒野之中,等待在以色列人中公开露面的时机。

< Luka 1 >