< Mambo ya Walawi 6 >

1 Bwana akamwambia Mose:
L'Eternel parla aussi à Moïse, en disant:
2 “Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
Quand quelque personne aura péché, et aura commis un crime contre l'Eternel, en mentant à son prochain pour un dépôt, ou pour une chose qu'on aura mise entre ses mains, soit qu'il l'ait ravie, soit qu'il ait trompé son prochain.
3 au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
Ou s'il a trouvé quelque chose perdue, et qu'il mente à ce sujet; ou s'il jure faussement sur quelqu'une de toutes les choses qu'il arrive à l'homme de faire, en péchant à leur égard;
4 wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
S'il arrive donc qu'il ait péché, et qu'il soit trouvé coupable, il rendra la chose qu'il aura ravie, ou ce qu'il aura usurpé par tromperie, ou le dépôt qui lui aura été donné en garde, ou la chose perdue qu'il aura trouvée;
5 au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
Ou tout ce dont il aura juré faussement; il restituera le principal, et il ajoutera un cinquième par dessus à celui-là qui il appartenait; il le donnera le jour qu'il aura été déclaré coupable.
6 Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
Et il amènera pour l'Eternel au Sacrificateur [la victime de] son péché, [savoir] un bélier sans tare, [pris] du troupeau, avec l'estimation que tu feras de la faute.
7 Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
Et le Sacrificateur fera propitiation pour lui devant l'Eternel; et il lui sera pardonné, pour tout ce qu'il aura fait en quoi il se sera rendu coupable.
8 Bwana akamwambia Mose:
L'Eternel parla aussi à Moïse, en disant:
9 “Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
Commande à Aaron et à ses fils, et leur dis: C'est ici la Loi de l'holocauste; l'holocauste [demeurera] sur le feu qui est sur l'autel, toute la nuit jusqu'au matin, et le feu de l'autel y sera tenu allumé.
10 Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
Et le Sacrificateur, vêtu de sa robe de lin, mettra ses caleçons de lin sur sa chair, et il lèvera les cendres après que le feu aura consumé l'holocauste sur l'autel; puis il les mettra près de l'autel.
11 Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
Alors il dépouillera ses vêtements, et s'étant vêtu d'autres habits, il transportera les cendres hors du camp, en un lieu net.
12 Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
Et quant au feu qui est sur l'autel, on l'y tiendra allumé, [et] on ne le laissera point éteindre. Le Sacrificateur allumera du bois au feu tous les matins, il arrangera l'holocauste sur le bois, et y fera fumer les graisses des offrandes de prospérités.
13 Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
On tiendra le feu continuellement allumé sur l'autel, [et] on ne le laissera point éteindre.
14 “‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
Et c'est ici la Loi de l'offrande du gâteau; les fils d'Aaron l'offriront devant l'Eternel sur l'autel.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Et on lèvera une poignée de la fleur de farine du gâteau, et de son huile, avec tout l'encens qui est sur le gâteau, et on le fera fumer en bonne odeur sur l'autel pour mémorial à l'Eternel.
16 Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
Et Aaron et ses fils mangeront ce qui en restera; on le mangera sans levain dans un lieu saint, on le mangera dans le parvis du Tabernacle d'assignation.
17 Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
On n'en cuira point qui soit fait avec du levain; je leur ai donné cela pour leur portion d'entre mes offrandes faites par feu; c'est une chose très-sainte, comme [la victime pour] le péché, et [la victime pour] le délit.
18 Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
Tout mâle d'entre les fils d'Aaron en mangera; c'est une ordonnance perpétuelle en vos âges touchant les offrandes faites par feu à l'Eternel; quiconque les touchera sera sanctifié.
19 Tena Bwana akamwambia Mose,
L'Eternel parla aussi à Moïse, en disant:
20 “Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
C'est ici l'offrande d'Aaron et de ses fils, laquelle ils offriront à l'Eternel le jour qu'il sera oint, [savoir] la dixième partie d'un Epha de fine farine, pour offrande perpétuelle; une moitié le matin, [et] l'autre moitié le soir.
21 Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Elle sera apprêtée sur une plaque avec de l'huile, tu l'apporteras ainsi rissolée, et tu offriras les pièces cuites du gâteau en bonne odeur à l'Eternel.
22 Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
Et le Sacrificateur d'entre ses fils qui [sera] oint en sa place, fera cela par ordonnance perpétuelle; on le fera fumer tout entier à l'Eternel.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
Et tout le gâteau du Sacrificateur sera consumé, sans en manger.
24 Bwana akamwambia Mose,
L'Eternel parla aussi à Moïse, en disant:
25 “Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
Parle à Aaron et à ses fils, et leur dis: C'est ici la Loi [de la victime pour] le péché; [la victime] pour le péché sera égorgée devant l'Eternel, dans le [même] lieu où l'holocauste sera égorgé; [car] c'est une chose très-sainte.
26 Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
Le Sacrificateur qui offrira [la victime] pour le péché, la mangera; elle se mangera dans un lieu saint, dans le parvis du Tabernacle d'assignation.
27 Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
Quiconque touchera sa chair sera saint, et s'il en rejaillit quelque sang sur le vêtement, ce sur quoi le sang sera tombé sera lavé dans le lieu saint.
28 Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
Et le vaisseau de terre dans lequel on l'aura fait bouillir, sera cassé; mais si on l'a fait bouillir dans un vaisseau d'airain, il sera écuré, et lavé dans l'eau.
29 Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
Tout mâle d'entre les Sacrificateurs en mangera; c'est une chose très-sainte.
30 Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.
Nulle [victime pour] le péché dont on portera du sang dans le Tabernacle d'assignation, pour faire la propitiation dans le Sanctuaire, ne sera mangée, mais elle sera brûlée au feu.

< Mambo ya Walawi 6 >