< Mambo ya Walawi 21 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
And the Lord said vnto Moses, Speake vnto the Priestes the sonnes of Aaron, and say vnto them, Let none be defiled by the dead among his people,
2 isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
But by his kinseman that is neere vnto him: to wit, by his mother, or by his father, or by his sonne, or by his daughter, or by his brother,
3 au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
Or by his sister a maid, that is neere vnto him, which hath not had a husband: for her he may lament.
4 Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
He shall not lament for the Prince among his people, to pollute him selfe.
5 “‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
They shall not make balde partes vpon their head, nor shaue off the locks of their beard, nor make any cuttings in their flesh.
6 Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
They shalbe holy vnto their God, and not pollute the name of their God: for the sacrifices of the Lord made by fire, and the bread of their God they doe offer: therefore they shalbe holie.
7 “‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
They shall not take to wife an whore, or one polluted, neither shall they marrie a woman diuorced from her husband: for such one is holy vnto his God.
8 Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
Thou shalt sanctifie him therefore, for he offereth the bread of thy God: he shall be holy vnto thee: for I the Lord, which sanctifie you, am holy.
9 “‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
If a Priestes daughter fall to play the whore, she polluteth her father: therefore shall she be burnt with fire.
10 “‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
Also ye hie Priest among his brethren, (vpon whose head the anointing oyle was powred, and hath consecrated his hand to put on the garments) shall not vncouer his head, nor rent his clothes,
11 Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
Neither shall he goe to any dead bodie, nor make him selfe vncleane by his father or by his mother,
12 wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
Neither shall he goe out of the Sanctuarie, nor pollute the holy place of his God: for the crowne of the anoynting oyle of his God is vpon him: I am the Lord.
13 “‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
Also he shall take a maide vnto his wife:
14 Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
But a widowe, or a diuorced woman, or a polluted, or an harlot, these shall he not marrie, but shall take a maide of his owne people to wife:
15 na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
Neyther shall he defile his seede among his people: for I am the Lord which sanctifie him.
16 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spake vnto Moses, saying,
17 “Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
Speake vnto Aaron, and say, Whosoeuer of thy seede in their generations hath any blemishes, shall not prease to offer the bread of his God:
18 Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
For whosoeuer hath any blemish, shall not come neere: as a man blinde or lame, or that hath a flat nose, or that hath any misshapen member,
19 hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
Or a man that hath a broken foote, or a broken hande,
20 au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
Or is crooke backt, or bleare eyed, or hath a blemish in his eye, or be skiruie, or skabbed, or haue his stones broken.
21 Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
None of the seede of Aaron the Priest that hath a blemish, shall come neere to offer the sacrifices of the Lord made by fire, hauing a blemish: he shall not prease to offer the bread of his God.
22 Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
The bread of his God, euen of the most holie, and of the holy shall he eate:
23 Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
But he shall not goe in vnto the vaile, nor come neere the altar, because hee hath a blemish, least he pollute my Sanctuaries: for I am the Lord that sanctifie them.
24 Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.
Thus spake Moses vnto Aaron, and to his sonnes, and to all the children of Israel.

< Mambo ya Walawi 21 >