< Mambo ya Walawi 14 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Ja Herra puhui Mosekselle, sanoen:
2 “Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
Ja tämä on spitalisen sääty: koska hän puhdistetaan, hän pitää tuotaman papin tykö.
3 Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
Ja papin pitää käymän ulos leiristä, katselemaan häntä, jos spitalin haava on parantunut spitalisesta.
4 kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
Ja pappi käskekään sen, joka puhdistetaan, ottaa kaksi elävää puhdasta lintua, ja sedripuuta, ja tulipunaiseksi painettua villaa, ja isoppia.
5 Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
Ja pappi käskekään sen teurastaa yhden linnun saviastiassa, vuotavan veden tykönä.
6 Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
Ja ottakaan elävän linnun sedripuun kanssa, tulipunalla painetun villan ja isopin, ja kastakaan tapetun linnun vereen, vuotavan veden tykönä.
7 Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
Ja priiskottakaan spitalista puhdistettavan päälle seitsemän kertaa: ja niin puhdistakaan hänen, ja antakaan elävän linnun lentää kedolle.
8 “Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
Mutta puhdistettu peskään vaatteensa, ja ajelkaan kaikki hiuksensa, ja peskään itsensä vedessä ja niin on hän puhdas. Menkään sitte leiriin, kuitenkin asukaan ulkona majastansa seitsemän päivää.
9 Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
Ja seitsemäntenä päivänä pitää hänen ajeleman kaikki hiukset päästänsä, ja partansa ja karvat silmäkulmistansa, niin että kaikki karvat ovat ajellut, ja pitää pesemän vaatteensa, ja pesemän ihonsa vedellä, niin on hän puhdas.
10 “Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
Ja kahdeksantena päivänä pitää hänen ottaman kaksi virheetöintä karitsaa, ja virheettömän vuosikuntaisen lampaan, niin myös kolme kymmenestä sämpyläjauhoja ruokauhriksi, öljyllä sekoitettuja, ja yhden login öljyä.
11 Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
Niin pitää papin, joka puhdisti, asettaman puhdistetun ja tämän kalun, Herran eteen seurakunnan majan oven edessä.
12 “Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
Ja papin pitää ottaman yhden karitsan, ja uhraaman vikauhriksi, öljylogin kanssa, ja pitää ne häälyttämäm häälytykseksi Herran edessä.
13 Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
Ja sitte teurastaman karitsan sillä paikalla, kussa rikosuhri ja polttouhri teurastetaan, pyhässä siassa; sillä niinkuin rikosuhri, niin myös vikauhrikin on papin oma; sillä se on kaikkein pyhin.
14 Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
Ja papin pitää ottaman vikauhrin verta ja sivuman puhdistetun oikian korvan lehteen, niin myös oikian käden peukaloon, ja oikian jalan isoon varpaaseen.
15 Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
Ja papin pitää ottaman öljylogista ja vuodattaman papin vasempaan käteen.
16 na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
Ja papin pitää kastaman oikian kätensä sormen öljyyn, joka hänen vasemmassa kädessänsä on, ja priiskottaman öljyä sormellansa seitsemän kertaa Herran edessä.
17 Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
Vaan käteensä jääneestä öljystä pitää papin paneman puhdistetun oikian korvan lehteen, ja oikiaan peukaloon, ja oikian jalan isoon varpaaseen, vikauhrin veren päälle.
18 Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
Käteensä jääneen öljyn, pitää papin paneman puhdistetun pään päälle, ja papin pitää sovittaman häntä Herran edessä.
19 “Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
Ja papin pitää tekemän rikosuhrin, ja sovittaman puhdistetun hänen saastaisuudestansa, ja sen jälkeen teurastaman polttouhrin.
20 na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
Ja papin pitää uhraaman polttouhrin ja ruokauhrin alttarilla, ja papin pitää sovittaman häntä, niin hän on puhdas.
21 “Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
Jos hän on köyhä eikä ole hänellä varaa, niin ottakaan karitsan vikauhrinsa edestä häälytykseksi, sovittaakseen häntä, ja yhden kymmeneksen sämpyläjauhoja, sekoitetun öljyllä, ruokauhriksi, ja login öljyä,
22 na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
Ja kaksi mettistä eli kaksi kyyhkyläisen poikaa, jotka hän voi saada: toinen olkoon rikosuhriksi, ja toinen polttouhriksi.
23 “Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
Ja kantakaan sen papille kahdeksantena päivänä puhdistukseksensa, seurakunnan majan oven eteen, Herran edessä.
24 Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
Niin pitää papin ottaman vikauhrin karitsan, ja login öljyä, ja papin pitää ne häälyttämän häälytykseksi Herran edessä,
25 Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
Ja teurastaman vikauhrin karitsan, ja papin pitää ottaman vikauhrin verta, ja sivuman puhdistetun oikian korvan lehteen, niin myös oikian käden peukaloon, ja oikian jalan isoon varpaaseen.
26 Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
Ja papin pitää vuodattaman öljyä papin vasempaan käteen.
27 na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
Ja papin pitää priiskottaman oikian käden sormella öljyä, joka on hänen vasemmassa kädessänsä, seitsemän kertaa Herran edessä.
28 Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
Käteensä jääneestä öljystä pitää papin panenman puhdistetun oikian korvan lehteen, ja oikian käden peukaloon, ja oikian jalan isoon varpaaseen, vikauhrin veren päälle.
29 Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
Ja käteensä jääneen öljyn pankaan papin puhdistetun pään päälle, ja sovittakoon häntä Herran edessä.
30 Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
Ja valmistakaan mettisiä, taikka kyhkyläisen poikia, jotka hän on voinut saada,
31 mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
Nimittäin niitä, joita hän on voinut saada: yhden rikosuhriksi ja toisen polttouhriksi, ynnä ruokauhrin kanssa; ja niin pitää papin sovittaman puhdistetun Herran edessä,
32 Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
Tämä on sääty spitalisesta, joka ei voi saada sitä, mikä hänen puhdistukseensa tarvitaan.
33 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Ja Herra puhui Mosekselle ja Aaronille, sanoen:
34 “Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
Koska te tulette Kanaanin maalle, jonka minä annan teille omaisuudeksi, ja minä sen maan huoneesen spitalin haavan annan,
35 ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
Niin pitää sen tuleman, jonka huone on, ja ilmoittaman papille, sanoen: minun huoneessani näkyy niinkuin (spitalin) haava;
36 Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
Niin pitää papin käskemän heidän lakaista huoneen, ennenkuin pappi siihen menee katsomaan haavaa, ettei kaikki, jotka huoneessa ovat, saastutettaisi: sitte pitää papin menemän katselemaan huonetta.
37 Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
Koska hän näkee haavan, ja löytää, että huoneen seinissä viheriäiset ja punahtavat onnet ovat, ja ovat nähdä matalammat muuta seinää;
38 kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
Niin lähtekään pappi huoneen ovesta, ja sulkekaan huoneen kiinni seitsemäksi päiväksi.
39 Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
Ja koska pappi seitsemäntenä päivänä palajaa ja näkee haavan itsensä levittäneeksi huoneen seiniin;
40 ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
Niin pitää papin käskemän heidän kangottaa ulos kiviä, joissa haava on, ja heittää niitä kaupungista ulos, saastaiseen paikkaan.
41 Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
Ja huone pitää sisältä kaikki ympärinsä puhtaaksi kaavittaman, ja kaavittu savi heitettämän kaupungista ulos, saastaiseen paikkaan.
42 Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
Ja heidän pitää ottaman toiset kivet, ja paneman niiden kivein siaan, ja ottaman toisen saven, ja sivuman huoneen.
43 “Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
Jos siis haava jällensä tulee, ja pakahtuu ulos huoneessa sittekuin kivet ovat kangotetut ulos, ja huone vastuudesta sivuttu;
44 kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
Niin pitää papin menemän sen sisälle, ja koska hän näkee haavan laskeneeksi itsensä leviämmälle huoneessa, niin on tosin kuluttuvainen spitali siinä huoneessa, ja se on saastainen.
45 Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
Sentähden pitää se huone särjettämän, sekä kivet että puut, ja kaikki savi huoneesta, ja vietävä kaupungista ulos, saastaiseen paikkaan.
46 “Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
Ja se joka käy huoneessa niinkauvan kuin se teljetty on, hänen pitää oleman saastainen ehtoosen asti.
47 Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
Ja sen joka siinä huoneessa makaa, pitää vaatteensa pesemän, ja se joka syö siinä huoneessa, pitää vaatteensa pesemän.
48 “Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
Jos myös pappi menee ja näkee, ettei haava ole laskenut itseänsä leviämmelle huoneessa, sittekuin se sivuttu on, niin sanokaan sen puhtaaksi; sillä haava on parannut.
49 Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
Ja pitää ottaman huoneen puhdistamiseksi kaksi lintua, niin myös sedripuuta, ja tulipunalla painetuita villoja, ja isoppia,
50 Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
Ja teurastaman toisen linnun savisessa astiassa, vuotavan veden tykönä.
51 Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
Ja pitää ottaman sedripuun, ja isopin, ja tulipunalla painetuita villoja, ja elävän linnun, ja kastaman ne sen vereen, ja vuotavaan veteen, ja priiskottaman huoneen seitsemän kertaa,
52 Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
Ja puhdistaman huoneen linnun verellä, ja vuotavalla vedellä, niin myös elävällä linnulla, sedripuulla, isopilla ja tulipunalla painetulla villalla.
53 Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
Ja sitte päästäkään elävän linnun lentämään kaupungista kedolle, ja sovittakaan huoneen, niin se on puhdas.
54 Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
Tämä on kaikkinaisen spitalin ja syhelmän haavain sääty:
55 upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
Vaatteen ja huoneen spitalin,
56 kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
Paisumain, pisamain ja putkenpolttamien,
57 kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.
Että pitää tiedettämän, mikä puhdas eli saastainen kunakin päivänä oleman pitää. Tämä on sääty spitalista.

< Mambo ya Walawi 14 >