< Waamuzi 1 >

1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
And it came to pass after the death of Joshua that the children of Israel asked Jehovah, saying, Which of us shall go up against the Canaanites first, to fight against them?
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
And Jehovah said, Judah shall go up: behold, I have delivered the land into his hand.
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
And Judah said to Simeon his brother, Come up with me into my lot, and let us fight against the Canaanites, and I likewise will go with thee into thy lot; and Simeon went with him.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
And Judah went up; and Jehovah delivered the Canaanites and the Perizzites into their hand, and they smote them in Bezek, ten thousand men.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
And they found Adoni-Bezek in Bezek, and fought against him, and they smote the Canaanites and the Perizzites.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
And Adoni-Bezek fled, and they pursued after him, and caught him, and cut off his thumbs and his great toes.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
And Adoni-Bezek said, Seventy kings, with their thumbs and their great toes cut off, gleaned under my table: as I have done, so God has requited me. And they brought him to Jerusalem, and there he died.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
And the children of Judah fought against Jerusalem, and took it, and smote it with the edge of the sword, and set the city on fire.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
And afterwards the children of Judah went down to fight against the Canaanites, that dwelt in the hill-country, and in the south, and in the lowland.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
And Judah went against the Canaanites that dwelt in Hebron — the name of Hebron before was Kirjath-Arba; and they slew Sheshai and Ahiman and Talmai.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
And from there he went against the inhabitants of Debir; now the name of Debir before was Kirjath-sepher.
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
And Caleb said, He that smites Kirjath-sepher and takes it, to him will I give Achsah my daughter as wife.
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
And Othniel the son of Kenaz, Caleb's younger brother, took it; and he gave him Achsah his daughter as wife.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
And it came to pass as she came, that she urged him to ask of her father the field; and she sprang down from the ass. And Caleb said to her, What wouldest thou?
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
And she said to him, Give me a blessing; for thou hast given me a southern land; give me also springs of water. And Caleb gave her the upper springs and the lower springs.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
And the children of the Kenite, Moses' father-in-law, had gone up out of the city of palm-trees with the children of Judah into the wilderness of Judah, which is in the south of Arad; and they went and dwelt with the people.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
And Judah went with Simeon his brother, and they slew the Canaanites that inhabited Zephath, and utterly destroyed it; and they called the name of the city Hormah.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
And Judah took Gazah and its border, and Ashkelon and its border, and Ekron and its border.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
And Jehovah was with Judah; and he took possession of the hill-country, for he did not dispossess the inhabitants of the valley, because they had chariots of iron.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
And they gave to Caleb Hebron, as Moses had said; and he dispossessed from thence the three sons of Anak.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
And the children of Benjamin did not dispossess the Jebusites, the inhabitants of Jerusalem; but the Jebusites dwell with the children of Benjamin in Jerusalem to this day.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
And the house of Joseph, they also went up against Bethel; and Jehovah was with them.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
And the house of Joseph sent to search out Bethel; now the name of the city before was Luz.
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
And the guards saw a man come forth out of the city, and said unto him, Shew us, we pray thee, how [we] may enter into the city, and we will shew thee kindness.
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
And he shewed them how to enter into the city. And they smote the city with the edge of the sword; but they let go the man and all his family.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
And the man went into the land of the Hittites, and built a city, and called its name Luz, which is its name to this day.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
And Manasseh did not dispossess Beth-shean and its dependent villages, nor Taanach and its dependent villages, nor the inhabitants of Dor and its dependent villages, nor the inhabitants of Ibleam and its dependent villages, nor the inhabitants of Megiddo and its dependent villages; and the Canaanites would dwell in that land.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
And it came to pass when Israel became strong, that they made the Canaanites tributary; but they did not utterly dispossess them.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
And Ephraim did not dispossess the Canaanites that dwelt in Gezer; but the Canaanites dwelt among them in Gezer.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
Zebulun did not dispossess the inhabitants of Kitron, nor the inhabitants of Nahalol; but the Canaanites dwelt among them, and became tributaries.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
Asher did not dispossess the inhabitants of Accho, nor the inhabitants of Zidon, nor Ahlab, nor Achzib, nor Helbah, nor Aphik, nor Rehob;
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
and the Asherites dwelt among the Canaanites, the inhabitants of the land; for they did not dispossess them.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
Naphtali did not dispossess the inhabitants of Beth-shemesh, nor the inhabitants of Beth-anath; and he dwelt among the Canaanites, the inhabitants of the land, but the inhabitants of Beth-shemesh and of Beth-anath became tributaries to them.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
And the Amorites forced the children of Dan into the hill-country, for they would not suffer them to come down to the valley.
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
And the Amorites would dwell on mount Heres, in Ajalon and in Shaalbim; but the hand of the house of Joseph prevailed, and they became tributaries.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
And the border of the Amorites was from the ascent of Akrabbim, from the rock, and upwards.

< Waamuzi 1 >