< Waamuzi 9 >

1 Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu ya mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake,
And Abimelech the son of Jerubbaal went to Shechem to his mother's brethren, and communed with them, and with all the family of the house of his mother's father, saying,
2 “Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa wenu nyama yenu hasa.”
Speak, I pray you, in the ears of all the men of Shechem, Which [is] better for you, either that all the sons of Jerubbaal, [which are] seventy persons, should reign over you, or that one should reign over you? remember also that I [am] your bone and your flesh.
3 Ndugu za mama yake walipowaeleza watu wote wa Shekemu, wakaelekea kumkubali Abimeleki, kwa kuwa walisema, “Yeye ni ndugu yetu.”
And his mother's brethren spoke of him in the ears of all the men of Shechem all these words: and their hearts inclined to follow Abimelech; for they said, He [is] our brother.
4 Wakampa shekeli sabini za fedha kutoka hekalu la Baal-Berithi, naye Abimeleki akaitumia kuajiri watu ovyo wasiojali, wakawa ndio wafuasi wake.
And they gave him seventy [pieces] of silver out of the house of Baal-berith, with which Abimelech hired vain and light persons, who followed him.
5 Akaenda nyumbani kwa baba yake huko Ofra, na juu ya jiwe moja wakawaua ndugu zake sabini, ambao ni wana wa Yerub-Baali. Lakini Yothamu, mwana mdogo wa wote wa Yerub-Baali, akaokoka kwa kujificha.
And he went to his father's house at Ophrah, and slew his brethren the sons of Jerubbaal, [being] seventy persons, upon one stone; notwithstanding, yet Jotham the youngest son of Jerubbaal was left; for he hid himself.
6 Ndipo watu wote wa Shekemu na Beth-Milo wakakusanyika pamoja chini ya mti mkubwa wa mwaloni penye nguzo iliyoko Shekemu wakamvika Abimeleki taji kuwa mfalme.
And all the men of Shechem assembled, and all the house of Millo, and went and made Abimelech king, by the plain of the pillar that [was] in Shechem.
7 Yothamu alipoambiwa hayo, akapanda juu ya kilele cha mlima Gerizimu, akawapazia sauti yake akawaambia, “Nisikilizeni enyi watu wa Shekemu, ili Mungu naye apate kuwasikiliza ninyi.
And when they told [it] to Jotham, he went and stood in the top of mount Gerizim, and lifted up his voice and cried, and said to them, Hearken to me, ye men of Shechem, that God may hearken to you.
8 Siku moja miti ilitoka ili kwenda kujitawazia mfalme. Ikauambia mzeituni, ‘Wewe uwe mfalme wetu.’
The trees went forth [on a time] to anoint a king over them; and they said to the olive-tree, Reign thou over us.
9 “Lakini mzeituni ukaijibu, ‘Je, niache kutoa mafuta yangu ambayo kwake miungu na wanadamu huheshimiwa, ili nikawe juu ya miti?’
But the olive-tree said to them, Should I leave my fatness, with which by me they honor God and man, and go to be promoted over the trees?
10 “Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo na uwe mfalme wetu!’
And the trees said to the fig-tree, Come thou, [and] reign over us.
11 “Lakini mtini ukaijibu, ‘Je, niache kutoa matunda yangu mazuri na matamu, ili niende nikawe juu ya miti?’
But the fig-tree said to them, Should I forsake my sweetness, and my good fruit, and go to be promoted over the trees?
12 “Ndipo miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
Then said the trees to the vine, Come thou, [and] reign over us.
13 “Lakini mzabibu ukaijibu, ‘Je, niache kutoa divai yangu inayofurahisha miungu na wanadamu ili nikawe juu ya miti?’
And the vine said to them, Should I leave my wine, which cheereth God and man, and go to be promoted over the trees?
14 “Mwishoni miti yote ikauambia mti wa miiba, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
Then said all the trees to the bramble, Come thou, [and] reign over us.
15 “Nao mti wa miiba ukaijibu, ‘Kama kweli mnataka niwe mfalme wenu, basi njooni mpate kupumzika chini ya kivuli changu. Lakini kama sivyo, moto na utoke kwenye mti wa miiba ukateketeze mierezi ya Lebanoni!’
And the bramble said to the trees, If in truth ye anoint me king over you, [then] come [and] put your trust in my shadow: and if not, let fire come out of the bramble, and devour the cedars of Lebanon.
16 “Basi ikiwa mmetenda kwa uaminifu na heshima kumfanya Abimeleki kuwa mfalme, na kama mmetendea vyema Yerub-Baali na jamaa yake kama ilivyostahili:
Now therefore, if ye have done truly and sincerely, in that ye have made Abimelech king, and if ye have dealt well with Jerubbaal and his house, and have done to him according to the deserving of his hands:
17 kwa kuwa baba yangu aliwapigania ninyi na kuhatarisha nafsi yake na kuwaokoa ninyi kutoka mikononi mwa Wamidiani
(For my father fought for you, and adventured his life far, and delivered you from the hand of Midian:
18 (lakini leo mmeasi dhidi ya jamaa ya baba yangu, na kuwaua wanawe sabini juu ya jiwe moja, nanyi mkamfanya Abimeleki mwana wa mwanamke mtumwa kuwa mfalme juu ya Shekemu, kwa kuwa yeye ni ndugu yenu),
And ye have risen up against my father's house this day, and have slain his sons, seventy persons, upon one stone, and have made Abimelech, the son of his maid-servant, king over the men of Shechem, because he [is] your brother: )
19 nanyi kama basi mmemtendea Yerub-Baali na jamaa yake kwa heshima na uaminifu, basi Abimeleki na awe furaha yenu, nanyi mwe furaha yake pia!
If ye then have dealt truly and sincerely with Jerubbaal and with his house this day, [then] rejoice ye in Abimelech, and let him also rejoice in you:
20 Lakini kama sivyo, moto na utoke kwa Abimeleki na uwateketeze, ninyi watu wa Shekemu na Beth-Milo, nao moto utoke kwenu, watu wa Shekemu na Beth-Milo umteketeze Abimeleki!”
But if not, let fire come out from Abimelech, and devour the men of Shechem, and the house of Millo; and let fire come out from the men of Shechem, and from the house of Millo, and devour Abimelech.
21 Ndipo Yothamu akakimbia, akatoroka akaenda Beeri, akaishi huko, kwa sababu alimwogopa ndugu yake Abimeleki.
And Jotham ran away, and fled, and went to Beer, and dwelt there, for fear of Abimelech his brother.
22 Baada ya Abimeleki kutawala Israeli kwa muda wa miaka mitatu,
When Abimelech had reigned three years over Israel,
23 Mungu akaruhusu roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu, nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa hila.
Then God sent an evil spirit between Abimelech and the men of Shechem; and the men of Shechem dealt treacherously with Abimelech:
24 Hili lilitokea ili ule ukatili waliotendewa hao wana sabini wa Yerub-Baali upatilizwe, na damu yao iwe juu ya Abimeleki ndugu yao aliyewaua, na pia iwe juu ya watu wa Shekemu, ambao walimsaidia kuua ndugu zake.
That the cruelty [done] to the seventy sons of Jerubbaal might come, and their blood be laid upon Abimelech their brother who slew them, and upon the men of Shechem who aided him in the killing of his brethren.
25 Hivyo, kutokana na uadui juu yake watu wa Shekemu wakaweka watu wa kumvizia katika vilele vya milima. Wakawanyangʼanya watu wote waliopita karibu nao, nayo haya yakaarifiwa kwa Abimeleki.
And the men of Shechem set liers in wait for him on the top of the mountains, and they robbed all that came along that way by them: and it was told Abimelech.
26 Basi Gaali mwana wa Ebedi akaenda pamoja na ndugu zake wakaingia Shekemu, nao watu wa huko wakamtumainia yeye.
And Gaal the son of Ebed came with his brethren, and went over to Shechem: and the men of Shechem put their confidence in him.
27 Wakaenda mashambani mwao kuvuna zabibu na kuzisindika hizo zabibu, wakafanya sikukuu katika hekalu la mungu wao. Wakati wakila na kunywa, wakamlaani Abimeleki.
And they went out into the fields, and gathered their vineyards, and trod [the grapes], and made merry, and went into the house of their god, and ate and drank, and cursed Abimelech.
28 Gaali mwana wa Ebedi akasema, “Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerub-Baali? Naye Zebuli si ndiye msaidizi wake? Basi watumikieni watu wa Hamori, babaye Shekemu. Kwa nini tumtumikie Abimeleki?
And Gaal the son of Ebed said, Who [is] Abimelech, and who [is] Shechem, that we should serve him; [is] not [he] the son of Jerubbaal? and Zebul his officer? Serve the men of Hamor the father of Shechem: for why should we serve him?
29 Laiti watu hawa wangekuwa chini ya amri yangu! Basi mimi ningemwondoa huyo Abimeleki. Ningemwambia Abimeleki, ‘Ondoa jeshi lako lote.’”
And would that this people were under my hand! then would I remove Abimelech. And he said to Abimelech, Increase thy army, and come out.
30 Zebuli aliyekuwa mtawala wa mji aliposikia aliyosema Gaali mwana wa Ebedi, akakasirika sana.
And when Zebul the ruler of the city heard the words of Gaal the son of Ebed, his anger was kindled.
31 Akatuma ujumbe uende kwa Abimeleki kwa siri na kusema, “Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wamekuja Shekemu, na wanauchochea mji huu kinyume chako.
And he sent messengers to Abimelech privately, saying, Behold, Gaal the son of Ebed, and his brethren, are come to Shechem; and behold, they fortify the city against thee.
32 Sasa, basi, usiku huu wewe uondoke na watu wako ili mje kuwavizia mashambani.
Now therefore rise by night, thou, and the people that [are] with thee, and lie in wait in the field:
33 Kisha asubuhi wakati wa kuchomoza jua, amka mapema na ujipange dhidi ya huo mji. Wakati yeye na jeshi lililo pamoja naye watakapotoka kukabiliana nanyi, mwaweza kuwatendea kwa kadiri mnavyoweza.”
And it shall be, [that] in the morning, as soon as the sun hath risen, thou shalt rise early, and attack the city: and behold, [when] he and the people that [are] with him come out against thee, then mayest thou do to them as thou shalt find occasion.
34 Kwa hiyo Abimeleki pamoja na jeshi lake lote wakaondoka usiku na kujificha karibu na Shekemu wakiwa vikosi vinne.
And Abimelech rose, and all the people that [were] with him, by night, and they laid wait against Shechem in four companies.
35 Basi Gaali mwana wa Ebedi alikuwa ametoka nje akawa amesimama katika ingilio la mji wakati ule ule ambao Abimeleki na watu wake walipokuwa wanatoka sehemu zao za maficho.
And Gaal the son of Ebed went out, and stood in the entrance of the gate of the city: and Abimelech rose, and the people that [were] with him, from lying in wait.
36 Gaali alipowaona, akamwambia Zebuli, “Tazama, watu wanashuka kutoka kwenye vilele vya milima!” Zebuli akajibu, “Wewe unaona vivuli vya milima kana kwamba ni watu.”
And when Gaal saw the people, he said to Zebul, Behold, there come people down from the top of the mountains. And Zebul said to him, Thou seest the shadow of the mountains as [if they were] men.
37 Lakini Gaali akasema tena, “Tazama, watu wanashuka kutoka katikati ya nchi na kikosi kimoja kinakuja kutoka Tabur-Ezeri na kikosi kingine kutoka upande wa Elon-Meonenimu.”
And Gaal spoke again, and said, See, there come people down by the middle of the land, and another company come along by the plain of Meonenim.
38 Ndipo Zebuli akamwambia, “Kuko wapi kujivuna kwako sasa, wewe uliyesema, ‘Huyo Abimeleki ni nani hata tumtumikie?’ Hawa si wale watu uliowadharau? Toka nje sasa ukapigane nao!”
Then said Zebul to him, Where [is] now thy mouth, with which thou saidst, Who [is] Abimelech, that we should serve him? [are] not these the people that thou hast despised? go out, I pray now, and fight with them.
39 Basi Gaali akatoka akawaongoza watu wa Shekemu kupigana na Abimeleki.
And Gaal went out before the men of Shechem, and fought with Abimelech.
40 Abimeleki akamfukuza, watu wengi wakajeruhiwa katika kukimbia huko, njia nzima hadi kwenye ingilio la lango.
And Abimelech chased him, and he fled before him, and many were overthrown [and] wounded, [even] to the entrance of the gate.
41 Abimeleki akakaa Aruma, naye Zebuli akawafukuza Gaali na ndugu zake watoke Shekemu.
And Abimelech dwelt at Arumah: and Zebul thrust out Gaal and his brethren, that they should not dwell in Shechem.
42 Kesho yake watu wa Shekemu wakatoka wakaenda mashambani, Abimeleki akaambiwa juu ya jambo hili.
And it came to pass on the morrow, that the people went out into the field; and they told Abimelech.
43 Hivyo akawachukua watu wake, akawagawanya katika vikosi vitatu na kuwaweka waviziao huko mashambani. Alipowaona watu wanatoka kwenda nje ya mji, akainuka dhidi yao na kuwashambulia.
And he took the people, and divided them into three companies, and laid wait in the field, and looked, and behold, the people [had] come out of the city; and he rose up against them, and smote them.
44 Abimeleki pamoja na vile vikosi wakaharakisha kwenda mbele kwenye nafasi, mahali pa ingilio la lango la mji. Vile vikosi viwili vikawawahi wale waliokuwa mashambani na kuwaua.
And Abimelech, and the company that [was] with him, rushed forward, and stood in the entrance of the gate of the city: and the two [other] companies ran upon all [the people] that [were] in the fields, and slew them.
45 Siku hiyo nzima Abimeleki akazidisha mashambulizi yake dhidi ya mji hadi akawa ameuteka na kuwaua watu wa huo mji. Kisha akauangamiza mji na kusambaza chumvi juu yake.
And Abimelech fought against the city all that day; and he took the city, and slew the people that [were] in it, and beat down the city, and sowed it with salt.
46 Kwa kusikia jambo hili watu wote katika mnara wa Shekemu, wakaingia kwenye ngome ya hekalu la El-Berithi.
And when all the men of the tower of Shechem heard [that], they entered into a hold of the house of the god Berith.
47 Abimeleki aliposikia kuwa wamekusanyika huko,
And it was told to Abimelech, that all the men of the tower of Shechem were assembled.
48 yeye na watu wake wote wakakwea kwenye Mlima Salmoni. Abimeleki akachukua shoka, akakata baadhi ya matawi, ambayo aliyachukua mabegani. Akawaagiza wale watu waliokuwa pamoja naye kuwa, “Fanyeni kile mlichoona mimi nikifanya!”
And Abimelech ascended mount Zalmon, he and all the people that [were] with him; and Abimelech took an ax in his hand, and cut down a bough from the trees, and took it, and laid [it] on his shoulder, and said to the people that [were] with him, What ye have seen me do, make haste, [and] do as I [have done].
49 Basi watu wote wakakata matawi na kumfuata Abimeleki. Wakayakusanya hayo matawi juu ya ngome na kuitia moto ili kuwachoma wale watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo watu wote katika mnara wa Shekemu, karibia watu 1,000 waume kwa wake, pia wakafa.
And all the people likewise cut down every man his bough, and followed Abimelech, and put [them] to the hold, and set the hold on fire upon them: so that all the men of the tower of Shechem died also, about a thousand men and women.
50 Baadaye Abimeleki akaenda Thebesi na kuuzingira kwa jeshi na kuuteka.
Then went Abimelech to Thebez, and encamped against Thebez, and took it.
51 Hata hivyo, ndani ya huo mji kulikuwa na mnara imara, ambako watu wote wa mji wanaume na wanawake, watu wote wa mji, walikimbilia ndani yake. Wakajifungia ndani yake na kupanda juu ya paa la mnara.
But there was a strong tower within the city, and thither fled all the men and women, and all they of the city, and shut [it] after them, and ascended to the top of the tower.
52 Abimeleki akaja kwenye ule mnara na kuushambulia, lakini alipokaribia kwenye ingilio la mnara ili kuuchoma kwa moto,
And Abimelech came to the tower, and fought against it, and came near to the door of the tower to burn it with fire.
53 mwanamke mmoja akaangusha sehemu ya juu ya jiwe la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki, likapasua fuvu la kichwa chake.
And a certain woman cast a piece of of a millstone upon Abimelech's head, and broke his skull.
54 Akamwita kwa haraka kijana yule aliyechukua silaha zake, na kumwambia, “Chukua upanga wako na uniue, watu wasije wakasema kwamba, ‘Mwanamke amemuua.’” Basi yule kijana akamchoma upanga, naye akafa.
Then he called hastily to the young man his armor-bearer, and said to him, Draw thy sword, and slay me, that men say not of me, A woman slew him. And his young man thrust him through, and he died.
55 Waisraeli walipoona kuwa Abimeleki amekufa, kila mtu akaenda nyumbani kwake.
And when the men of Israel saw that Abimelech was dead, they departed every man to his place.
56 Hivyo ndivyo Mungu alivyolipiza uovu ule ambao Abimeleki alikuwa ameutenda kwa baba yake kwa kuwaua ndugu zake sabini.
Thus God rendered the wickedness of Abimelech, which he did to his father, in slaying his seventy brethren:
57 Mungu akawapatiliza watu wa Shekemu uovu wao juu ya vichwa vyao, na juu yao ikaja laana ya Yothamu mwana wa Yerub-Baali.
And all the evil of the men of Shechem did God render upon their heads: and upon them came the curse of Jotham the son of Jerubbaal.

< Waamuzi 9 >