< Waamuzi 7 >

1 Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More.
Jérubbaal, qui est Gédéon, et tout le peuple qui était avec lui, s'étant donc levés de bon matin, campèrent près de la fontaine de Harod; et le camp de Madian était au nord, vers le coteau de Moré, dans la vallée.
2 Bwana akamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. Ili kwamba Israeli asije akajisifu juu yangu akisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa,
Or, l'Éternel dit à Gédéon: Le peuple qui est avec toi, est trop nombreux pour que je livre Madian en ses mains; Israël se glorifierait contre moi, en disant: C'est ma main qui m'a délivré.
3 kwa hiyo sasa tangaza jeshi lote likiwa linasikia, kwamba: Yeyote anayeogopa na kutetemeka, yeye na arudi nyumbani, aondoke katika Mlima Gileadi.’” Hivyo watu 22,000 walirudi, wakabaki 10,000.
Maintenant donc, publie ceci aux oreilles du peuple, et qu'on dise: Que celui qui est timide et qui a peur, s'en retourne et s'éloigne librement de la montagne de Galaad. Et vingt-deux mille hommes d'entre le peuple s'en retournèrent, et il en resta dix mille.
4 Lakini Bwana akamwambia Gideoni, “Idadi ya jeshi bado ni kubwa. Wapeleke chini katika maji nami nitawajaribu huko kwa ajili yako. Kama nikikuambia, ‘Huyu atakwenda pamoja nawe,’ yeye atakwenda; lakini kama nikisema, ‘Huyu hatakwenda pamoja nawe,’ yeye hatakwenda.”
Et l'Éternel dit à Gédéon: Le peuple est encore trop nombreux; fais-les descendre vers l'eau, et là je les mettrai à l'épreuve; et celui dont je te dirai: Celui-ci ira avec toi, ira; et celui duquel je te dirai: Celui-ci n'ira point avec toi, n'ira point.
5 Hivyo Gideoni akalileta lile jeshi chini kwenye maji naye Bwana akamwambia Gideoni, “Watenge upande mmoja wale wote wanywao maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”
Il fit donc descendre le peuple vers l'eau, et l'Éternel dit à Gédéon: Quiconque lapera l'eau avec sa langue, comme le chien lape, tu le mettras à part; et tu les sépareras de tous ceux qui se courberont sur leurs genoux pour boire.
6 Idadi ya wale waliokunywa kwa kuramba ramba walikuwa 300, lakini wengine wote katika jeshi walipiga magoti ili kunywa.
Et le nombre de ceux qui lapèrent l'eau dans leurs mains, la portant à leur bouche, fut de trois cents hommes; mais tout le reste du peuple se courba sur ses genoux pour boire de l'eau.
7 Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa hao watu 300 walioramba maji nitawaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mkononi mwako. Waache hao watu wengine wote warudi kila mmoja nyumbani mwake.”
Alors l'Éternel dit à Gédéon: Je vous délivrerai par ces trois cents hommes, qui ont lapé l'eau, et je livrerai Madian entre tes mains. Que tout le peuple s'en aille, chacun chez soi.
8 Hivyo Gideoni akawaacha wale Waisraeli wengine kila mmoja aende kwenye hema yake. Akabakia na wale 300, ambao walichukua vyakula na tarumbeta za wale wenzao. Basi kambi ya Wamidiani ilikuwa chini yake bondeni.
On garda les vivres du peuple et ses trompettes. Et Gédéon renvoya tous les hommes d'Israël, chacun en sa tente, mais il retint les trois cents hommes. Or, le camp de Madian était au-dessous de lui, dans la vallée.
9 Usiku ule ule Bwana akamwambia Gideoni, “Ondoka, ushuke kambini, kwa kuwa nimeitia mkononi mwako.
Et l'Éternel dit à Gédéon pendant la nuit: Lève-toi, descends au camp, car je l'ai livré entre tes mains.
10 Lakini kama unaogopa kushambulia, shuka kambini pamoja na mtumishi wako Pura,
Et si tu crains d'y descendre seul, descends au camp avec Pura ton serviteur,
11 nawe sikiliza wanayosema. Hatimaye, utatiwa moyo kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mtumishi wake wakashuka na kufikia walinzi wa mbele wenye silaha waliokuwa mle kambini.
Et tu entendras ce qu'ils diront, et tes mains seront fortifiées; descends au camp. Il descendit donc, avec Pura son serviteur, jusqu'aux avant-postes du camp.
12 Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine yote ya mashariki walikaa bondeni, nao walikuwa mfano wa nzige kwa wingi wao. Ngamia zao hazikuhesabika, wingi wao ulikuwa kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.
Or, les Madianites, les Amalécites et tous les fils de l'Orient étaient répandus dans la vallée, nombreux comme des sauterelles, et leurs chameaux étaient sans nombre, comme le sable qui est sur le bord de la mer, tant il y en avait.
13 Gideoni alifika wakati huo huo kukiwa na mtu mmoja aliyekuwa anamweleza mwenzake ndoto yake, akisema, “Niliota ndoto: Tazama mkate wa shayiri ulioviringana ulianguka katika kambi moja ya Wamidiani, ukaipiga na ikaanguka nao ukaipindua juu chini na hema ikaporomoka chini.”
Et Gédéon arriva; et voici un homme contait à son compagnon un songe, et il disait: Voici, j'ai fait un songe; il me semblait qu'un gâteau de pain d'orge roulait dans le camp des Madianites, et qu'étant venu jusqu'à la tente, il l'a frappée, de sorte qu'elle est tombée; et il l'a retournée sens dessus dessous, et elle a été renversée.
14 Rafiki yake akamjibu, “Habari hii si kitu kingine zaidi ya upanga wa Gideoni mwana wa Yoashi, Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote mkononi mwake.”
Alors son compagnon répondit et dit: Ce songe ne signifie pas autre chose que l'épée de Gédéon, fils de Joas, homme d'Israël. Dieu a livré Madian et tout ce camp entre ses mains.
15 Gideoni alipoisikia hiyo ndoto na tafsiri yake, akamwabudu Mungu. Akarudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Inukeni! Bwana amelitia jeshi la Wamidiani mikononi mwenu.”
Et quand Gédéon eut entendu le récit du songe et son interprétation, il se prosterna, revint au camp d'Israël, et dit: Levez-vous, car l'Éternel a livré le camp de Madian entre vos mains.
16 Akawagawa wale watu 300 katika makundi matatu, akawakabidhi tarumbeta mikononi mwao wote na mitungi isiyokuwa na maji yenye mienge ndani yake.
Puis il divisa les trois cents hommes en trois bandes, et il leur remit à chacun des trompettes, et des cruches vides, et des flambeaux dans les cruches;
17 Akawaambia, “Nitazameni, fanyeni kama nitakavyofanya, nitakapofika mwisho wa kambi mfanye kama nitakavyofanya.
Et il leur dit: Regardez-moi, et faites comme je ferai; quand je serai arrivé à l'extrémité du camp, vous ferez ce que je ferai.
18 Wakati mimi na wale walio pamoja nami wote, tutakapopiga tarumbeta zetu, ninyi nanyi pigeni tarumbeta pande zote za kambi na mpige kelele, mseme, ‘Upanga wa Bwana na wa Gideoni.’”
Et quand je sonnerai de la trompette, moi et tous ceux qui seront avec moi, vous sonnerez aussi de la trompette autour de tout le camp, et vous direz: Pour l'Éternel et pour Gédéon!
19 Gideoni na wale watu 100 waliokuwa pamoja naye wakafika mwisho wa kambi usiku mwanzoni mwa zamu ya kati, mara tu walipokuwa wamebadili zamu. Wakapiga zile tarumbeta zao na kuvunja ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
Gédéon, et les cent hommes qui étaient avec lui, vinrent à l'extrémité du camp, au commencement de la veille de minuit, comme on venait de poser les gardes. Ils sonnèrent des trompettes et cassèrent les cruches qu'ils avaient en leurs mains.
20 Yale makundi matatu yakapiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na katika mikono yao ya kuume tarumbeta ili kuzipiga, wakapaza sauti zao, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni!”
Alors les trois bandes sonnèrent des trompettes, et cassèrent les cruches. Ils saisirent de leur main gauche les flambeaux, et de leur main droite les trompettes pour sonner; et ils crièrent: L'épée pour l'Éternel et pour Gédéon!
21 Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka kambi pande zote, Wamidiani wote wakakimbia, huku wakipiga kelele.
Et ils se tinrent, chacun à sa place, autour du camp; et tout le camp se mit à courir, à pousser des cris, et à fuir.
22 Walipozipiga zile tarumbeta 300, Bwana akafanya watu katika kambi yote kugeuziana upanga kila mmoja na mwenziwe. Jeshi likakimbia mpaka Beth-Shita kuelekea Serera hadi mpakani mwa Abel-Mehola karibu na Tabathi.
Les trois cents hommes sonnèrent encore des trompettes, et par tout le camp l'Éternel tourna l'épée de chacun contre son compagnon. Et le camp s'enfuit jusqu'à Beth-Shitta, vers Tseréra, jusqu'au bord d'Abel-Mehola, vers Tabbath.
23 Watu wa Israeli wakaitwa kutoka Naftali, Asheri na Manase, wakawafuatia Wamidiani.
Et les hommes d'Israël, ceux de Nephthali, et d'Asser, et de tout Manassé, s'assemblèrent et poursuivirent les Madianites.
24 Gideoni akatuma wajumbe katika nchi yote ya vilima vya Efraimu akisema, “Teremkeni dhidi ya Wamidiani na mkazuie vivuko vya maji mbele yao hadi Beth-Bara na pia Yordani.” Hivyo watu wote wa Efraimu wakakutanika pamoja na kuzingira mto wa Yordani hadi Beth-Bara.
Alors Gédéon envoya des messagers dans toute la montagne d'Éphraïm, disant: Descendez à la rencontre des Madianites, et emparez-vous du passage des eaux, jusqu'à Beth-Bara, et du Jourdain. Les hommes d'Éphraïm s'assemblèrent donc, se saisirent des eaux jusqu'à Beth-Bara, et du Jourdain.
25 Wakawakamata wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamuulia Orebu pale penye mwamba wa Orebu, na Zeebu wakamuulia penye shinikizo la kukamulia divai la Zeebu. Wakawafuatia Wamidiani na kuleta vichwa vya Orebu na Zeebu kwa Gideoni, huko ngʼambo ya Yordani.
Et ils prirent deux des chefs des Madianites: Oreb et Zéeb. Et ils tuèrent Oreb au rocher d'Oreb, et tuèrent Zéeb au pressoir de Zéeb. Puis ils poursuivirent les Madianites, et apportèrent les têtes d'Oreb et de Zéeb à Gédéon, de l'autre côté du Jourdain.

< Waamuzi 7 >