< Waamuzi 7 >

1 Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More.
Then Jerubbaal, who is Gideon, and all the people who were with him, rose up early, and camped beside the spring of Harod. And the camp of Midian was on the north side of them, by the hill of Moreh, in the valley.
2 Bwana akamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. Ili kwamba Israeli asije akajisifu juu yangu akisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa,
Jehovah said to Gideon, "The people who are with you are too many for me to give the Midianites into their hand, lest Israel vaunt themselves against me, saying, 'My own hand has saved me.'
3 kwa hiyo sasa tangaza jeshi lote likiwa linasikia, kwamba: Yeyote anayeogopa na kutetemeka, yeye na arudi nyumbani, aondoke katika Mlima Gileadi.’” Hivyo watu 22,000 walirudi, wakabaki 10,000.
Now therefore proclaim in the ears of the people, saying, 'Whoever is fearful and trembling, let him return and depart from Mount Gilead.' There returned of the people twenty-two thousand; but ten thousand remained.
4 Lakini Bwana akamwambia Gideoni, “Idadi ya jeshi bado ni kubwa. Wapeleke chini katika maji nami nitawajaribu huko kwa ajili yako. Kama nikikuambia, ‘Huyu atakwenda pamoja nawe,’ yeye atakwenda; lakini kama nikisema, ‘Huyu hatakwenda pamoja nawe,’ yeye hatakwenda.”
Jehovah said to Gideon, "The people are yet too many; bring them down to the water, and I will try them for you there: and it shall be, that of whom I tell you, This shall go with you, the same shall go with you; and of whoever I tell you, This shall not go with you, the same shall not go.
5 Hivyo Gideoni akalileta lile jeshi chini kwenye maji naye Bwana akamwambia Gideoni, “Watenge upande mmoja wale wote wanywao maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”
So he brought down the people to the water. And Jehovah said to Gideon, "Everyone who laps of the water with his tongue, as a dog laps, you shall put to one side; and everyone who gets down on his knees to drink with hand to mouth shall be on the other side."
6 Idadi ya wale waliokunywa kwa kuramba ramba walikuwa 300, lakini wengine wote katika jeshi walipiga magoti ili kunywa.
The number of those who lapped with their tongues was three hundred men, but all the rest of the people got down on their knees to drink water.
7 Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa hao watu 300 walioramba maji nitawaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mkononi mwako. Waache hao watu wengine wote warudi kila mmoja nyumbani mwake.”
Jehovah said to Gideon, "By the three hundred men who lapped will I save you, and deliver the Midianites into your hand; and let all the people go every man to his home."
8 Hivyo Gideoni akawaacha wale Waisraeli wengine kila mmoja aende kwenye hema yake. Akabakia na wale 300, ambao walichukua vyakula na tarumbeta za wale wenzao. Basi kambi ya Wamidiani ilikuwa chini yake bondeni.
So the people took food in their hand, and their trumpets; and he sent all the men of Israel every man to his tent, but retained the three hundred men. And the camp of Midian was beneath him in the valley.
9 Usiku ule ule Bwana akamwambia Gideoni, “Ondoka, ushuke kambini, kwa kuwa nimeitia mkononi mwako.
It happened the same night, that Jehovah said to him, "Arise, get down into the camp; for I have delivered it into your hand.
10 Lakini kama unaogopa kushambulia, shuka kambini pamoja na mtumishi wako Pura,
But if you fear to go down, go with Purah your servant down to the camp:
11 nawe sikiliza wanayosema. Hatimaye, utatiwa moyo kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mtumishi wake wakashuka na kufikia walinzi wa mbele wenye silaha waliokuwa mle kambini.
and you shall hear what they say; and afterward will your hands be strengthened to go down into the camp." Then he went down with Purah his servant to the outermost part of the armed men who were in the camp.
12 Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine yote ya mashariki walikaa bondeni, nao walikuwa mfano wa nzige kwa wingi wao. Ngamia zao hazikuhesabika, wingi wao ulikuwa kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.
And Midian, Amalek, and all the Kedemites lay along in the valley as numerous as locusts; and their camels were without number, as numerous as the sand which is on the seashore.
13 Gideoni alifika wakati huo huo kukiwa na mtu mmoja aliyekuwa anamweleza mwenzake ndoto yake, akisema, “Niliota ndoto: Tazama mkate wa shayiri ulioviringana ulianguka katika kambi moja ya Wamidiani, ukaipiga na ikaanguka nao ukaipindua juu chini na hema ikaporomoka chini.”
When Gideon had come, look, there was a man telling a dream to his friend; and he said, "Look, I had a dream, and look, a cake of barley bread tumbled into the camp of Midian, and came to the tent, and struck it so that it fell, and turned it upside down, so that the tent collapsed."
14 Rafiki yake akamjibu, “Habari hii si kitu kingine zaidi ya upanga wa Gideoni mwana wa Yoashi, Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote mkononi mwake.”
His friend answered, "This is nothing less than the sword of Gideon the son of Joash, a man of Israel. Into his hand God has delivered Midian, and all the army."
15 Gideoni alipoisikia hiyo ndoto na tafsiri yake, akamwabudu Mungu. Akarudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Inukeni! Bwana amelitia jeshi la Wamidiani mikononi mwenu.”
It was so, when Gideon heard the telling of the dream, and its interpretation, that he worshiped, and he returned into the camp of Israel, and said, "Get up, for Jehovah has delivered into your hand the army of Midian."
16 Akawagawa wale watu 300 katika makundi matatu, akawakabidhi tarumbeta mikononi mwao wote na mitungi isiyokuwa na maji yenye mienge ndani yake.
He divided the three hundred men into three companies, and he put into the hands of all of them trumpets, and empty pitchers, with torches within the pitchers.
17 Akawaambia, “Nitazameni, fanyeni kama nitakavyofanya, nitakapofika mwisho wa kambi mfanye kama nitakavyofanya.
He said to them, "Look at me, and do likewise. And look, when I come to the outermost part of the camp, it shall be that, as I do, so you shall do.
18 Wakati mimi na wale walio pamoja nami wote, tutakapopiga tarumbeta zetu, ninyi nanyi pigeni tarumbeta pande zote za kambi na mpige kelele, mseme, ‘Upanga wa Bwana na wa Gideoni.’”
When I blow the trumpet, I and all who are with me, then you blow the trumpets also on every side of all the camp, and say, "For Jehovah and for Gideon."
19 Gideoni na wale watu 100 waliokuwa pamoja naye wakafika mwisho wa kambi usiku mwanzoni mwa zamu ya kati, mara tu walipokuwa wamebadili zamu. Wakapiga zile tarumbeta zao na kuvunja ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
So Gideon and the hundred men who were with him came to the outermost part of the camp in the beginning of the middle watch, when they had but newly set the watch: and they blew the trumpets, and broke in pieces the pitchers that were in their hands.
20 Yale makundi matatu yakapiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na katika mikono yao ya kuume tarumbeta ili kuzipiga, wakapaza sauti zao, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni!”
The three companies blew the trumpets, and broke the pitchers, and held the torches in their left hands, and the trumpets in their right hands with which to blow; and they called out, "The sword of Jehovah and of Gideon.'"
21 Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka kambi pande zote, Wamidiani wote wakakimbia, huku wakipiga kelele.
They each stood in his place every man around the camp; and all the army ran; and they shouted, and put them to flight.
22 Walipozipiga zile tarumbeta 300, Bwana akafanya watu katika kambi yote kugeuziana upanga kila mmoja na mwenziwe. Jeshi likakimbia mpaka Beth-Shita kuelekea Serera hadi mpakani mwa Abel-Mehola karibu na Tabathi.
They blew the three hundred trumpets, and Jehovah set every man's sword against each other throughout the camp; and the army fled as far as Beth Shittah toward Zererah, as far as the border of Abel Meholah, by Tabbath.
23 Watu wa Israeli wakaitwa kutoka Naftali, Asheri na Manase, wakawafuatia Wamidiani.
The men of Israel were gathered together out of Naphtali, and out of Asher, and out of all Manasseh, and pursued after Midian.
24 Gideoni akatuma wajumbe katika nchi yote ya vilima vya Efraimu akisema, “Teremkeni dhidi ya Wamidiani na mkazuie vivuko vya maji mbele yao hadi Beth-Bara na pia Yordani.” Hivyo watu wote wa Efraimu wakakutanika pamoja na kuzingira mto wa Yordani hadi Beth-Bara.
Gideon sent messengers throughout all the hill country of Ephraim, saying, "Come down against Midian, and capture the waters, as far as Beth Barah, even the Jordan." So all the men of Ephraim were gathered together, and seized the waters as far as Beth Barah, even the Jordan.
25 Wakawakamata wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamuulia Orebu pale penye mwamba wa Orebu, na Zeebu wakamuulia penye shinikizo la kukamulia divai la Zeebu. Wakawafuatia Wamidiani na kuleta vichwa vya Orebu na Zeebu kwa Gideoni, huko ngʼambo ya Yordani.
They took the two princes of Midian, Oreb and Zeeb; and they killed Oreb at the rock of Oreb, and Zeeb they killed at the winepress of Zeeb, and pursued Midian. Then they brought the heads of Oreb and Zeeb to Gideon beyond the Jordan.

< Waamuzi 7 >