< Waamuzi 16 >

1 Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona mwanamke kahaba, naye akaingia kwake.
And Samson went from there to Gaza, and saw a prostitute there, and went in to her.
2 Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja huku!” Hivyo wakapazingira mahali pale nao wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji. Wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, “Tumvizie hadi mapambazuko, ndipo tutamuua.”
And it was reported to the Gazites, saying, "Samson is here." They surrounded him, and lay in wait for him all night at the gate of the city, and were quiet all night, saying, "Wait until morning light, then we will kill him."
3 Samsoni akalala mpaka usiku wa manane. Akaondoka katikati ya usiku, akashika milango ya lango la mji pamoja na miimo yake miwili, akaingʼoa, makomeo yake na vyote. Akaviweka mabegani mwake na kuvipeleka mpaka kwenye kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.
Now Samson rested until midnight, but got up at midnight and took hold of the doors of the gate of the city, and the two posts, and pulled them up, bar and all, and put them on his shoulders, and carried them up to the top of the mountain that is overlooking Hebron, and set them down there.
4 Baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika Bonde la Soreki aliyeitwa Delila.
It came to pass afterward, that he fell in love with a woman in the Valley of Sorek, whose name was Delilah.
5 Viongozi wa Wafilisti wakamwendea yule mwanamke na kumwambia, “Umbembeleze ili upate kujua siri za nguvu zake zilizo nyingi na jinsi tutakavyoweza kumshinda ili tuweze kumfunga na kumtiisha. Nasi kila mmoja wetu tutakupa shekeli 1,100 za fedha.”
The lords of the Philistines came up to her, and said to her, "Entice him, and see in which his great strength lies, and by what means we may prevail against him, that we may bind him to afflict him; and we will each give you eleven hundred pieces of silver."
6 Hivyo Delila akamwambia Samsoni, “Naomba niambie siri ya hizi nguvu zako nyingi na jinsi utakavyoweza kufungwa ili kukutiisha.”
Delilah said to Samson, "Please tell me where your great strength lies, and how you can be bound and subdued."
7 Samsoni akamjibu, “Kama wakinifunga kwa kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakapokuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
Samson said to her, "If they bind me with seven green cords that were never dried, then shall I become weak, and be as another man."
8 Viongozi wa Wafilisti wakamletea yule mwanamke kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, akamfunga nazo Samsoni.
Then the lords of the Philistines brought up to her seven green cords which had not been dried, and she bound him with them.
9 Wakati watu wakiwa wanamvizia katika chumba cha ndani, yule mwanamke akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini yeye akazikata zile kamba za upinde, kama vile uzi wa pamba unapoguswa na moto. Hivyo siri ya nguvu zake haikujulikana.
Now she had an ambush waiting in the inner room. She said to him, "The Philistines are on you, Samson." He broke the cords, as a string of tow is broken when it touches the fire. So his strength was not known.
10 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Tafadhali niambie waweza kufungwa kwa kitu gani?”
Delilah said to Samson, "Look, you have mocked me, and told me lies: now please tell me with which you might be bound."
11 Akamwambia, “Wakinifunga kwa uthabiti kwa kamba mpya ambazo hazijatumika, basi nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
He said to her, "If they only bind me with new ropes with which no work has been done, then shall I become weak, and be as another man."
12 Hivyo Delila akachukua kamba mpya na kumfunga nazo. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Wale watu waliokuwa wanamvizia walikuwa katika chumba cha ndani. Lakini akazikata zile kamba zilizokuwa zimefunga mikono yake kama akatavyo uzi.
So Delilah took new ropes, and bound him therewith, and said to him, "The Philistines are on you, Samson." The ambush was waiting in the inner room. He broke them off his arms like a thread.
13 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa, umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Nieleze ni jinsi gani utakavyoweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, “Kama ukivisuka hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo na kukaza kwa msumari, ndipo nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.” Hivyo Samsoni alipokuwa amelala, Delila akachukua vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake na kuvifunga kwenye mtande wa nguo,
Delilah said to Samson, "Until now, you have mocked me and told me lies. Tell me how you might be bound." He said to her, "If you weave the seven braids on my head with the fabric and fasten them with the pin, then I will be weak as another man."
14 na kuvikaza kwa msumari. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini akaamka kutoka usingizini na kuungʼoa ule msumari na ule mtande.
So while he slept, Delilah took the seven braids on his head, and wove them with the fabric, and she fastened it with the pin, and said to him, "The Philistines are upon you, Samson." And he awoke from his sleep, and pulled away the pin of the loom and the fabric.
15 Ndipo Delila akamwambia, “Wawezaje kusema, ‘Nakupenda,’ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenifanyia mzaha mara hizi tatu na hujaniambia siri ya hizi nguvu zako nyingi.”
She said to him, "How can you say, 'I love you,' when your heart is not with me? You have mocked me these three times, and have not told me where your great strength lies."
16 Hatimaye, baada ya kuwa anamsumbua kwa maneno siku kwa siku na kumuudhi, roho yake ikataabika hata kufa.
It happened, when she pressed him daily with her words, and urged him, that his soul was troubled to death.
17 Hivyo akamwambia yule mwanamke siri yake yote, akamwambia, “Wembe haujapita kamwe kichwani mwangu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu. Kama nywele za kichwa changu zikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, na nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote!”
He told her all his heart, and said to her, "No razor has ever come on my head; for I have been a Nazirite to God from my mother's womb. If I am shaved, then my strength will go from me, and I will become weak, and be like any other man."
18 Delila alipoona kuwa amemweleza siri yake yote, akatuma ujumbe kwa viongozi wa Wafilisti na kusema, “Njooni tena mara nyingine, maana amenieleza siri yake yote.” Basi viongozi wa Wafilisti wakaja kwa Delila, wakiwa na fedha mikononi mwao.
When Delilah saw that he had told her all his heart, she sent and called for the lords of the Philistines, saying, "Come up this once, for he has told me all his heart." Then the lords of the Philistines went up to her, and brought the money in their hands.
19 Delila akamfanya alale usingizi magotini pake, akamwita mtu akamnyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake. Akaanza kumsumbua ili aamke nazo nguvu zake zikamtoka.
She made him sleep on her knees; and she called for a man, and shaved off the seven locks of his head; and he began to weaken, and his strength went from him.
20 Yule mwanamke akamwita, “Samsoni, hao Wafilisti wanakujia!” Akaamka toka usingizini akasema, “Nitatoka nje kama hapo awali, nitawakungʼutia mbali na kuwa huru.” Lakini hakujua kuwa Bwana amemwacha.
She said, "The Philistines are upon you, Samson." He awoke out of his sleep, and said, "I will go out as at other times, and shake myself free." But he didn't know that Jehovah had departed from him.
21 Basi Wafilisti wakamkamata, wakamngʼoa macho yake, wakamchukua wakamteremsha mpaka Gaza. Wakiwa wamemfunga kwa pingu za shaba, wakamweka ili asage ngano huko gerezani.
The Philistines seized him, and gouged out his eyes. And they brought him down to Gaza, and bound him with bronze shackles, and he ground at the mill in the prison.
22 Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.
However the hair of his head began to grow again after he was shaved.
23 Basi viongozi wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa kafara kwa mungu wao Dagoni na kufanya karamu, wakisema, “Mungu wetu amemtia adui yetu Samsoni mikononi mwetu.”
The lords of the Philistines gathered them together to offer a great sacrifice to their god Dagon, and to celebrate; for they said, "Our god has delivered Samson our enemy into our hand."
24 Watu walipomwona Samsoni wakamsifu mungu wao, wakisema: “Sasa mungu wetu amemtia adui yetu mikononi mwetu, yule aliyeharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.”
When the people saw him, they praised their god; for they said, "Our god has delivered our enemy and the destroyer of our country, who has slain many of us, into our hand."
25 Mioyo yao ilipokuwa imefurahishwa wakasema, “Mleteni Samsoni aje acheze ili tufurahi.” Basi wakamleta Samsoni kutoka mle gerezani naye akacheza mbele yao. Wakamweka kati ya nguzo mbili.
And it happened, when their hearts were merry, that they said, "Call for Samson, that he may entertain us." So they called for Samson out of the prison; and he performed before them. And they were striking him. And they set him between the pillars;
26 Samsoni akamwambia mtumishi aliyeshika mkono wake, “Niweke mahali ambapo ninaweza kuzigusa nguzo ambazo zinategemeza jengo ili nipate kuziegemea.”
and Samson said to the boy who held him by the hand, "Allow me to feel the pillars whereupon the house rests, that I may lean on them." And the boy did so.
27 Basi lile jengo lilikuwa na wingi wa watu waume kwa wake; viongozi wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na kwenye sakafu ya juu walikuwepo watu 3,000 waume kwa wake, waliokuwa wakimtazama Samsoni wakati anacheza.
Now the house was full of men and women; and all the lords of the Philistines were there. And there were on the roof about three thousand men and women watching while Samson performed.
28 Ndipo Samsoni akamwomba Bwana, akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, unikumbuke. Ee Mungu, nakusihi ukanitie nguvu mara hii moja tena, ili kwa tendo hili nipate kulipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.”
Samson called to Jehovah, and said, "Lord Jehovah, please remember me, and please strengthen me only this once, God, that I may be at once avenged of the Philistines for my two eyes."
29 Ndipo Samsoni akazikaribia zile nguzo mbili za katikati ambazo lile jengo lilikuwa linazitegemea. Akazishika moja kwa mkono wa kuume na nyingine mkono wa kushoto.
Samson took hold of the two middle pillars on which the house rested, and leaned on them, the one with his right hand, and the other with his left.
30 Samsoni akasema, “Nife pamoja na Wafilisti!” Ndipo akazisukuma zile nguzo kwa nguvu zake zote, lile jengo likaanguka juu ya viongozi na watu wote waliokuwamo mle ndani yake. Hivyo akawaua watu wengi wakati wa kufa kwake kuliko siku za uhai wake.
Samson said, "Let me die with the Philistines." He bowed himself with all his might; and the house fell on the lords, and on all the people who were in it. So the dead that he killed at his death were more than those who he killed in his life.
31 Basi ndugu zake na jamaa yote ya baba yake wakateremka kwenda kumchukua. Wakampandisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli kwenye kaburi la Manoa baba yake. Naye Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.
Then his brothers and all the house of his father came down, and took him, and brought him up, and buried him between Zorah and Eshtaol in the burial site of Manoah his father. He judged Israel twenty years.

< Waamuzi 16 >