< Waamuzi 12 >

1 Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
Les hommes d'Éphraïm, s'étant rassemblés, partirent pour le nord, et dirent à Jephthé: Pourquoi es-tu allé combattre contre les enfants d'Ammon, sans nous avoir appelés à marcher avec toi? Nous brûlerons ta maison, et nous te brûlerons aussi.
2 Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
Et Jephthé leur dit: Nous avons eu de grandes contestations avec les enfants d'Ammon, moi et mon peuple; et quand je vous ai appelés, vous ne m'avez pas délivré de leurs mains.
3 Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
Et voyant que vous ne me délivriez pas, j'ai exposé ma vie, et j'ai marché contre les enfants d'Ammon, et l'Éternel les a livrés en ma main. Pourquoi donc êtes-vous montés aujourd'hui contre moi, pour me faire la guerre?
4 Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
Puis Jephthé, ayant rassemblé tous les gens de Galaad, combattit contre Éphraïm; et les hommes de Galaad battirent ceux d'Éphraïm, parce que ceux-ci avaient dit: Vous êtes des fugitifs d'Éphraïm! Galaad est au milieu d'Éphraïm, au milieu de Manassé!
5 Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
Et Galaad s'empara des gués du Jourdain, avant que ceux d'Éphraïm n'y arrivassent. Et quand un des fugitifs d'Éphraïm disait: Laissez-moi passer; les gens de Galaad lui disaient: Es-tu Éphratien? et il répondait: Non.
6 walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
Alors ils lui disaient: Eh bien, dis: Shibboleth (fleuve); et il disait Sibboleth, sans faire attention à bien prononcer; alors, le saisissant, ils le mettaient à mort aux gués du Jourdain. Il périt en ce temps-là quarante-deux mille hommes d'Éphraïm.
7 Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
Jephthé jugea Israël six ans. Puis Jephthé, le Galaadite, mourut, et fut enseveli dans une des villes de Galaad.
8 Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
Après lui, Ibtsan de Bethléhem jugea Israël.
9 Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
Il eut trente fils, et il maria hors de sa maison trente filles. Il fit venir de dehors trente filles pour ses fils, et il jugea Israël sept ans.
10 Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
Puis Ibtsan mourut et fut enseveli à Bethléhem.
11 Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
Après lui, Élon, le Zabulonite, jugea Israël; il jugea Israël dix ans.
12 Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
Puis Élon, le Zabulonite, mourut, et fut enseveli à Ajalon, dans la terre de Zabulon.
13 Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
Après lui Abdon, fils d'Hillel, le Pirathonite, jugea Israël.
14 Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
Il eut quarante fils, et trente petits-fils, qui montaient sur soixante et dix ânons; et il jugea Israël huit ans.
15 Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.
Puis Abdon, fils d'Hillel, le Pirathonite, mourut, et fut enseveli à Pirathon, dans le pays d'Éphraïm, dans la montagne des Amalécites.

< Waamuzi 12 >