< Yoshua 20 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Yoshua,
Puis l'Eternel parla à Josué en disant:
2 “Waambie Waisraeli, watenge miji mikubwa ya kukimbilia, kama nilivyokuagiza kupitia Mose,
Parle aux enfants d'Israël, et [leur] dis: Etablissez-vous les villes de refuge desquelles je vous ai parlé par le moyen de Moïse.
3 ili mtu yeyote atakayemuua mtu kwa bahati mbaya na pasipo kukusudia aweze kukimbilia huko na kujiepusha na mlipiza kisasi wa damu.
Afin que le meurtrier qui aura tué quelqu'un par ignorance, sans y penser, s'y enfuie, et elles vous seront pour refuge devant celui qui a le droit de venger le sang.
4 “Anapokimbilia mojawapo ya hii miji mikubwa atasimama kwenye maingilio ya lango la mji mkuu na kueleza wazee wa mji kuhusu shauri lake. Kisha watampokea katika mji wao na kumpa mahali pa kuishi nao.
Et le [meurtrier] s'enfuira dans l'une de ces villes-là, et s'arrêtera à l'entrée de la porte de la ville, et il dira ses raisons aux Anciens de cette ville-là, lesquels l'écouteront, [et] le recevront chez eux dans la ville, et lui donneront un lieu, afin qu'il demeure avec eux.
5 Kama mlipiza kisasi wa damu akimfuatilia, wasimkabidhi yule mshtakiwa, kwa sababu alimuua jirani yake bila kukusudia, na bila kuwa na nia ya kudhuru.
Et quand celui qui a le droit de venger le sang le poursuivra, ils ne le livreront point en sa main; puisque c'est sans y penser qu'il a tué son prochain, et qu'il ne le haïssait point auparavant;
6 Huyu aliyeua atakaa kwenye mji mkubwa huo mpaka awe amesimama kukabili mashtaka yake mbele ya kusanyiko na mpaka kuhani mkuu anayehudumu kwa wakati huo atakapokufa. Ndipo atakapoweza kurudi nyumbani kwake katika mji ambao aliukimbia.”
Mais il demeurera dans cette ville-là, jusqu'à ce qu'il comparaisse devant l'assemblée en jugement, [même] jusqu'à la mort du souverain Sacrificateur qui sera en ce temps-là; alors le meurtrier retournera, et viendra dans sa ville et dans sa maison, à la ville dont il s'en sera fui.
7 Basi wakatenga Kedeshi katika Galilaya kwenye nchi ya vilima ya Naftali, Shekemu katika nchi ya vilima ya Efraimu, na Kiriath-Arba (yaani Hebroni) kwenye nchi ya vilima ya Yuda.
Ils consacrèrent donc Kédès dans la Galilée en la montagne de Nephthali; et Sichem en la montagne d'Ephraïm, et Kirjath-Arbah, qui est Hébron, en la montagne de Juda.
8 Katika upande wa mashariki mwa Yordani ya Yeriko wakatenga Bezeri katika jangwa katika uwanda wa juu katika kabila la Reubeni, Ramothi katika Gileadi katika kabila la Gadi, na Golani huko Bashani katika kabila la Manase.
Et au delà du Jourdain de Jérico vers le Levant ils ordonnèrent de la Tribu de Ruben, Betser au désert dans le plat pays, et Ramoth en Galaad, de la Tribu de Gad, et Golan en Basan, de la Tribu de Manassé.
9 Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote aishiye miongoni mwao aliyemuua mtu kwa bahati mbaya, angeweza kukimbilia katika miji mikubwa hiyo iliyotengwa na asiuawe na mlipiza kisasi wa damu kabla hajasimama kukabili mashtaka mbele ya kusanyiko.
Ce furent là les villes assignées à tous les enfants d'Israël, et à l'étranger demeurant parmi eux, afin que quiconque aurait tué quelqu'un par ignorance s'enfuît là, et ne mourût point de la main de celui qui a le droit de venger le sang, jusqu'à ce qu'il comparût devant l'assemblée.

< Yoshua 20 >