< Yoshua 17 >

1 Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
This was the assignment of land for the tribe of Manasseh (who was the firstborn of Joseph)—that is, for Makir, who was Manasseh's firstborn and who himself was the father of Gilead. Makir's descendants were assigned the land of Gilead and Bashan, because Makir had been a man of war.
2 Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
Land was assigned to the rest of the tribe of Manasseh, given to their clans—Abiezer, Helek, Asriel, Shechem, Hepher, and Shemida. These were the male descendants of Manasseh son of Joseph, presented by their clans.
3 Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
Now Zelophehad son of Hepher son of Gilead son of Makir son of Manasseh had no sons, but only daughters. The names of his daughters were Mahlah, Noah, Hoglah, Milkah, and Tirzah.
4 Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
They approached Eleazar the priest, Joshua son of Nun, and the leaders, and they said, “Yahweh commanded Moses to give to us an inheritance along with our brothers.” So, following the commandment of Yahweh, he gave those women an inheritance among the brothers of their father.
5 Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
Ten parcels of land were assigned to Manasseh in Gilead and Bashan, which is on the other side of the Jordan,
6 kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
because the daughters of Manasseh received an inheritance along with his sons. The land of Gilead was assigned to the rest of the tribe of Manasseh.
7 Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
The territory of Manasseh reached from Asher to Mikmethath, which is east of Shechem. Then the border went southward to those living near the spring of Tappuah.
8 (Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
(The land of Tappuah belonged to Manasseh, but the town of Tappuah on the border of Manasseh belonged to the tribe of Ephraim.)
9 Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
The border went down to the brook of Kanah. These cities south of the brook among the towns of Manasseh belonged to Ephraim. The border of Manasseh was on the north side of the brook, and it ended at the sea.
10 Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
The land to the south belonged to Ephraim, and the land to the north was Manasseh's; the sea was the border. On the north side Asher can be reached, and to the east, Issachar.
11 Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
Also in Issachar and in Asher, Manasseh possessed Beth Shan and its villages, Ibleam and its villages, the inhabitants of Dor and its villages, the inhabitants of Endor and its villages, the inhabitants of Taanach and its villages, and the inhabitants of Megiddo and its villages (and the third city is Napheth).
12 Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
Yet the tribe of Manasseh could not take possession of those cities, for the Canaanites continued to live in this land.
13 Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
When the people of Israel grew strong, they put the Canaanites to forced labor, but did not completely drive them out.
14 Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
Then the descendants of Joseph said to Joshua, saying, “Why have you given us only one assignment of land and one portion for an inheritance, since we are a people great in number, and all along Yahweh has blessed us?”
15 Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
Joshua said to them, “If you are a people great in number, go up by yourselves to the forest and there clear the ground for yourselves in the land of the Perizzites and of the Rephaim. Do this, since the hill country of Ephraim is too small for you.”
16 Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
The descendants of Joseph said, “The hill country is not enough for us. But all the Canaanites who live in the valley have chariots of iron, both those who are in Beth Shan and its villages, and those who are in the Valley of Jezreel.”
17 Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
Then Joshua said to the house of Joseph—to Ephraim and Manasseh, “You are a people great in number, and you have great power. You must not have only one piece of land assigned to you.
18 bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”
The hill country will also be yours. Though it is a forest, you will clear it and take possession of it to its farthest borders. You will drive out the Canaanites, even though they have chariots of iron, and even though they are strong.”

< Yoshua 17 >