< Yoshua 13 >

1 Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
Now Joshua was very old when Yahweh said to him, “You are very old, but there is still very much land to capture.
2 “Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
This is the land that still remains: All the regions of the Philistines, and all those of the Geshurites,
3 kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
from Shihor, which is east of Egypt, and northward to the border of Ekron, which is considered property of the Canaanites; the five rulers of the Philistines, those of Gaza, Ashdod, Ashkelon, Gath, and Ekron—the territory of the Avvites.
4 kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
In the south (the territory of the Avvites); all the lands of the Canaanites, from Arah that belongs to the Sidonians, as far as Aphek which is on the border of the Amorites;
5 eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
the land of the Gebalites, all of Lebanon toward the east, from Baal Gad below Mount Hermon to Lebo Hamath.
6 “Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
Also, all the inhabitants of the hill country from Lebanon as far as Misrephoth Maim, including all the people of Sidon. I will drive them out before the army of Israel. Be sure to assign the land to Israel as an inheritance, as I commanded you.
7 sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
Divide this land as an inheritance to the nine tribes and to the half tribe of Manasseh.”
8 Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
With the other half of the tribe of Manasseh, the Reubenites and the Gadites had received their inheritance that Moses gave them on the east side of the Jordan,
9 Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
from Aroer, which is on the edge of the Arnon river gorge (including the city that is in the middle of the gorge), to all the plateau of Medeba as far as Dibon;
10 nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
all the cities of Sihon, king of the Amorites, who ruled in Heshbon, to the border of the Ammonites;
11 Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
Gilead, and the region of the Geshurites and Maacathites, all of Mount Hermon, all Bashan to Salekah;
12 yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
all the kingdom of Og in Bashan, who reigned in Ashtaroth and Edrei—these are what was left of the remnant of the Rephaim—Moses struck them and drove them out.
13 Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
But the people of Israel did not drive out the Geshurites or the Maacathites. Instead, Geshur and Maacath live among Israel to this day.
14 Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
To the tribe of Levi alone Moses gave no inheritance. The offerings of Yahweh, the God of Israel, made by fire, are their inheritance, as God said to Moses.
15 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
Moses gave an inheritance to the tribe of Reuben, clan by clan.
16 Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
Their territory was from Aroer, on the edge of the Arnon River gorge, and the city that is in the middle of the valley, and all the plateau by Medeba.
17 hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
Reuben also received Heshbon and all its cities that are in the plateau, Dibon, and Bamoth Baal, and Beth Baal Meon,
18 Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
and Jahaz, and Kedemoth, and Mephaath,
19 Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
and Kiriathaim, and Sibmah, and Zereth Shahar on the hill of the valley.
20 Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
Reuben also received Beth Peor, the slopes of Pisgah, Beth Jeshimoth,
21 miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
all the cities of the plateau, and all the kingdom of Sihon king of the Amorites, who had reigned in Heshbon, whom Moses had defeated together with the leaders of Midian, Evi, Rekem, Zur, Hur and Reba, the princes of Sihon, who had lived in the land.
22 Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
The people of Israel also killed with the sword Balaam son of Beor, who practiced divination, among the rest of those they had killed.
23 Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
The border of the tribe of Reuben is the Jordan River; this is their boundary. This was the inheritance of the tribe of Reuben, given to each of their clans, with their cities and villages.
24 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
This is what Moses gave to the tribe of Gad, clan by clan:
25 Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
Their territory was Jazer, all the cities of Gilead and half the land of the Ammonites, to Aroer, which is east of Rabbah,
26 na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
from Heshbon to Ramath Mizpah and Betonim, from Mahanaim to the territory of Debir.
27 na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
In the valley, Moses gave them Beth Haram, Beth Nimrah, Succoth, and Zaphon, the rest of the kingdom of Sihon king of Heshbon, with the Jordan as a border, to the lower end of the Sea of Kinnereth, eastward beyond the Jordan.
28 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
This is the inheritance of the tribe of Gad, clan by clan, with their cities and villages.
29 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
Moses gave an inheritance to the half tribe of Manasseh. It was assigned to the half tribe of the people of Manasseh, clan by clan.
30 Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
Their territory was from Mahanaim, all Bashan, all the kingdom of Og king of Bashan, and all the towns of Jair, which are in Bashan, sixty cities;
31 nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
half of Gilead, and Ashtaroth and Edrei (the royal cities of Og in Bashan). These were assigned to the clan of Machir son of Manasseh—half of the people of Machir, clan by clan.
32 Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
This is the inheritance that Moses assigned to them on the plains of Moab, beyond the Jordan east of Jericho.
33 Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
Moses did not give an inheritance to the tribe of Levi. Yahweh, the God of Israel, is their inheritance, just as he said to them.

< Yoshua 13 >