< Yoshua 11 >

1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
Dès que Jabin, roi de Hatsor, eut appris ces choses, il envoya vers Jobab roi de Madon, vers le roi de Shimron, vers le roi d'Acshaph,
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
Vers les rois qui étaient au nord dans la montagne et dans la plaine au midi de Kinnéreth, et dans la plaine, et sur les hauteurs de Dor, à l'occident,
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
Vers les Cananéens de l'orient et de l'occident, vers les Amoréens, les Héthiens, les Phéréziens, les Jébusiens dans la montagne, et les Héviens au pied de l'Hermon, dans le pays de Mitspa.
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
Alors ils sortirent, eux et toutes leurs armées avec eux, un peuple nombreux, égal en nombre au sable qui est sur le bord de la mer, ayant des chevaux et des chars en fort grand nombre.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
Tous ces rois se réunirent et vinrent camper ensemble près des eaux de Mérom, pour combattre contre Israël.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
Mais l'Éternel dit à Josué: Ne les crains point; car demain, environ ce temps-ci, je les livrerai tous blessés à mort devant Israël; tu couperas les jarrets à leurs chevaux, et tu brûleras leurs chars au feu.
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
Josué, avec tous ses gens de guerre, vint donc subitement contre eux, près des eaux de Mérom, et ils tombèrent sur eux;
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
Et l'Éternel les livra entre les mains d'Israël; ils les battirent et les poursuivirent jusqu'à Sidon la grande, et jusqu'à Misrephoth-Maïm, et jusqu'à la vallée de Mitspa, vers l'orient; ils les battirent au point de n'en laisser échapper aucun.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
Et Josué leur fit comme l'Éternel lui avait dit; il coupa les jarrets de leurs chevaux, et il brûla leurs chars au feu.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
Et comme Josué s'en retournait, en ce même temps, il prit Hatsor, et frappa son roi avec l'épée; car Hatsor était autrefois la capitale de tous ces royaumes.
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
Ils firent passer au fil de l'épée toutes les personnes qui y étaient, les vouant à l'interdit; il n'y resta rien de ce qui respirait, et on brûla Hatsor.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
Josué prit aussi toutes les villes de ces rois, et tous leurs rois, et les fit passer au fil de l'épée; il les voua à l'interdit, comme Moïse, serviteur de l'Éternel, l'avait commandé.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Mais Israël ne brûla aucune des villes situées sur une colline, excepté Hatsor seule, que Josué brûla.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
Et les enfants d'Israël pillèrent pour eux tout le butin de ces villes, et le bétail; mais ils firent passer au fil de l'épée tous les hommes, jusqu'à ce qu'ils les eussent exterminés; ils n'y laissèrent rien de ce qui respirait.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
Comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse son serviteur, Moïse le commanda à Josué; et Josué fit ainsi; il n'omit rien de ce que l'Éternel avait commandé à Moïse.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
Josué prit donc tout ce pays, la montagne, tout le midi, tout le pays de Gossen, la plaine et la campagne, la montagne d'Israël et sa plaine,
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
Depuis la montagne nue, qui monte vers Séir, jusqu'à Baal-Gad, dans la vallée du Liban, au pied de la montagne d'Hermon. Et il prit tous leurs rois, les frappa, et les fit mourir.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
Josué fit longtemps la guerre contre tous ces rois.
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
Il n'y eut aucune ville qui fît la paix avec les enfants d'Israël, excepté les Héviens qui habitaient Gabaon. Ils les prirent toutes par la guerre;
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Car cela venait de l'Éternel, qu'ils endurcissent leur cœur pour sortir en bataille contre Israël; afin de les vouer à l'interdit sans qu'il y eût pour eux de merci, mais afin de les exterminer, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
En ce temps-là Josué vint et extermina les Anakim de la montagne d'Hébron, de Débir, d'Anab, de toute la montagne de Juda et de toute la montagne d'Israël; Josué les voua à l'interdit, avec leurs villes.
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
Il ne resta point d'Anakim dans le pays des enfants d'Israël, il n'en resta qu'à Gaza, à Gath et à Asdod.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
Josué prit donc tout le pays, selon tout ce que l'Éternel avait dit à Moïse, et Josué le donna en héritage à Israël, selon leurs divisions, d'après leurs tribus. Alors le pays fut tranquille et sans guerre.

< Yoshua 11 >