< Yoshua 11 >

1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
Da Kong Jabin af Hazor hørte herom sendte han Bud til Kong Jobab af Madon og Kongerne af Sjimron og Aksjaf.
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
og til Kongerne nordpå i Bjergene, i Arabalavningen sønden for Kinnerot, i Lavlandet og på Højdedraget vestpå ved Dor,
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
til Kana'anæerne i Øst og Vest, Amoriterne, Hivviterne, Perizziterne og Jebusiterne i Bjergene og Hetiterne ved Foden af Hermon i Mizpas Land;
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
og de drog ud med alle deres Hære, Krigsfolk talrige som Sandet ved Havets Bred, og med en stor Mængde Heste og Stridsvogne.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
Alle disse Konger slog sig sammen og kom og lejrede sig i Forening ved Meroms Vand for at angribe Israel.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
Men HERREN sagde til Josua: "Frygt ikke for dem! Thi i Morgen ved denne Tid vil jeg lade dem ligge faldne foran Israel; deres Heste skal du lamme, og deres Vogne skal du brænde!"
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
Da kom Josua med hele Hæren uventet over dem ved Meroms Vand og kastede sig over dem,
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
og HERREN gav dem i Israels Hånd, så de slog dem og forfulgte dem til den store Stad Zidon, til, Misrefot Majim og Mizpes Lavning i Øst, og huggede dem ned, så ikke en eneste af dem blev tilbage.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
Josua gjorde derpå med dem, som HERREN havde sagt ham; deres Heste lammede han, og deres Vogne brændte han.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
Ved den Tid vendte Josua om og indtog Hazor, og Kongen huggede han ned med Sværdet; Hazor var nemlig fordum alle disse Kongerigers Hovedstad;
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
og de huggede hver levende Sjæl i den ned med Sværdet og lagde Band på dem, så ikke en levende Sjæl blev tilbage; og Hazor stak han i Brand.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
Alle hine Kongsbyer med deres Konger undertvang Josua, og han huggede dem ned med Sværdet og lagde Band på dem, som HERRENs Tjener Moses havde påbudt.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Men ingen af de Byer, som lå på deres Høje, stak Israel i Brand, alene med Undtagelse af Hazor; den stak Josua i Brand.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
Kvæget og alt det andet, der røvedes fra disse Byer, beholdt Israeliterne som Bytte; men alle Menneskene huggede de ned med Sværdet til sidste Mand uden at lade en eneste levende Sjæl blive tilbage.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
Hvad HERREN havde pålagt sin Tjener Moses, havde Moses pålagt Josua, og det gjorde Josua; han undlod intet som helst af, hvad HERREN havde pålagt Moses.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
Således indtog Josua hele dette Land, Bjerglandet, hele Sydlandet, hele Landskabet Gosjen, Lavlandet, Arabalavningen, Israels Bjergland og Lavland,
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
fra det nøgne Bjergdrag, som højner sig hen imod Seir, indtil Ba'al Gad i Libanons Dal ved Hermonbjergets Fod; og alle deres Konger tog han til Fange, huggede dem ned og dræbte dem.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
I lang Tid førte Josua Krig med disse Konger
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
Der var ingen By, som sluttede Overenskomst med Israeliterne, undtagen Hivviterne, som boede i Gibeon. Alt tog de i Kamp;
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
thi HERREN voldte, at de forhærdede deres Hjerter, så de drog i Kamp mod Israel, for at de skulde lægge Band på dem uden Skånsel og udrydde dem, som HERREN havde pålagt Moses.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
Ved den Tid drog Josua hen og udryddede Anakiterne af Bjerglandet, af Hebron, Debir og Anab, og af hele Judas og hele Israels Bjergland; på dem og deres Byer lagde Josua Band.
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
Der blev ingen Anakiter tilbage i Israeliternes Land, kun i Gaza, Gat og Asdod blev der Levninger tilbage.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
Således indtog Josua hele Landet, ganske som HERREN havde sagt til Moses, og Josua gav Israel det i Eje efter deres Afdelinger, Stamme for Stamme. Og Landet fik Ro efter Krigen.

< Yoshua 11 >