< Yona 2 >

1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
Then Jonah prayed to Jehovah, his God, out of the fish's belly.
2 Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
He said, "I called because of my affliction to Jehovah. He answered me. Out of the belly of Sheol I cried. You heard my voice. (Sheol h7585)
3 Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
For you threw me into the depths, in the heart of the seas. The flood was all around me. All your breakers and waves passed over me.
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
I said, 'I have been banished from your sight; yet I will look again toward your holy temple.'
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
The waters surrounded me, threatening my life. The deep was around me. The end is upon my head.
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
I went down to the bottoms of the mountains. The earth barred me in forever: yet have you brought up my life from the pit, Jehovah my God.
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
"When my soul fainted within me, I remembered Jehovah. My prayer came in to you, into your holy temple.
8 “Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
Those who regard worthless things forsake their faithfulness.
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
But I will sacrifice to you with the voice of thanksgiving. I will pay that which I have vowed. Salvation belongs to Jehovah."
10 Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
Jehovah spoke to the fish, and it vomited out Jonah on the dry land.

< Yona 2 >