< Ayubu 42 >

1 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Alors Job répondit à l'Eternel, et dit:
2 “Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
Je sais que tu peux tout, et qu'on ne te saurait empêcher de faire ce que tu penses.
3 Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
Qui est celui-ci, [as-tu dit], qui étant sans science, [entreprend] d'obscurcir [mon] conseil? J'ai donc parlé, et je n'y entendais rien; ces choses sont trop merveilleuses pour moi, et je n'[y] connais rien.
4 “Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
Ecoute maintenant, et je parlerai; je t'interrogerai, et tu m'enseigneras.
5 Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
J'avais ouï de mes oreilles parler de toi; mais maintenant mon œil t'a vu.
6 Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
C'est pourquoi j'ai horreur [d'avoir ainsi parlé], et je m'en repens sur la poudre et sur la cendre.
7 Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.
Or après que l'Eternel eut dit ces paroles à Job, il dit à Eliphas Témanite: Ma fureur est embrasée contre toi, et contre tes deux compagnons; parce que vous n'avez pas parlé droitement de moi comme Job mon serviteur.
8 Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”
C'est pourquoi prenez maintenant sept taureaux, et sept béliers, et allez vers Job mon serviteur, et offrez un holocauste pour vous, et Job mon serviteur priera pour vous; (car certainement j'exaucerai sa prière, ) afin que je ne vous traite pas selon votre folie; parce que vous n'avez pas parlé droitement devant moi, comme a fait Job mon serviteur.
9 Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.
Ainsi Eliphas Témanite, et Bildad Suhite, [et] Tsophar Nahamathite vinrent, et firent ce que l'Eternel leur avait commandé; et l'Eternel exauça la prière de Job.
10 Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.
Et l'Eternel tira Job de sa captivité quand il eut prié pour ses amis; et il rendit à Job le double de tout ce qu'il avait eu.
11 Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
Aussi tous ses frères, et toutes ses sœurs, et tous ceux qui l'avaient connu auparavant, vinrent vers lui, et mangèrent avec lui dans sa maison, et lui ayant témoigné qu'ils compatissaient à son état, ils le consolèrent de tout le mal, que l'Eternel avait fait venir sur lui; et chacun d'eux lui donna une pièce d'argent, et chacun une bague d'or.
12 Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja.
Ainsi l'Eternel bénit le dernier état de Job plus que le premier, tellement qu'il eut quatorze mille brebis, et six mille chameaux, et mille couples de bœufs, et mille ânesses.
13 Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.
Il eut aussi sept fils, et trois filles.
14 Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki.
Et il appela le nom de l'une Jémina, et le nom de l'autre Ketsiha, et le nom de la troisième Kéren-happuch.
15 Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.
Et il ne se trouva point dans tout le pays de si belles femmes, que les filles de Job; et leur père leur donna héritage entre leurs frères.
16 Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.
Et Job vécut après ces choses-là cent quarante ans, et il vit ses fils, et les fils de ses fils, jusqu'à la quatrième génération.
17 Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.
Puis il mourut âgé et rassasié de jours.

< Ayubu 42 >