< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Und Jehova antwortete Hiob aus dem Sturme und sprach:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Wer ist es, der den Rat verdunkelt mit Worten ohne Erkenntnis?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Gürte doch wie ein Mann deine Lenden; so will ich dich fragen, und du belehre mich!
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Wo warst du, als ich die Erde gründete? Tue es kund, wenn du Einsicht besitzest!
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Wer hat ihre Maße bestimmt, wenn du es weißt? Oder wer hat über sie die Meßschnur gezogen?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
In was wurden ihre Grundfesten eingesenkt?
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
Oder wer hat ihren Eckstein gelegt, als die Morgensterne miteinander jubelten und alle Söhne Gottes jauchzten?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Und wer hat das Meer mit Toren verschlossen, als es ausbrach, hervorkam aus dem Mutterschoße,
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
als ich Gewölk zu seinem Gewande und Wolkendunkel zu seiner Windel machte,
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
und ich ihm meine Grenze bestimmte und Riegel und Tore setzte,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
und sprach: Bis hierher sollst du kommen und nicht weiter, und hier sei eine Schranke gesetzt dem Trotze deiner Wellen? -
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Hast du, seitdem du lebst, einem Morgen geboten? Hast du die Morgenröte ihre Stätte wissen lassen,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
daß sie erfasse die Säume der Erde, und die Gesetzlosen von ihr verscheucht werden?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
Sie verwandelt sich wie Siegelton, und alles steht da wie in einem Gewande;
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
und den Gesetzlosen wird ihr Licht entzogen, und der erhobene Arm wird zerbrochen.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Bist du gekommen bis zu den Quellen des Meeres, und hast du die Gründe der Tiefe durchwandelt?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Wurden dir die Pforten des Todes enthüllt, und sahest du die Pforten des Todesschattens?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Hast du Einsicht genommen in die Breiten der Erde? Sage an, wenn du es alles weißt!
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Welches ist der Weg zur Wohnung des Lichtes, und die Finsternis, wo ist ihre Stätte?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
Daß du sie hinbrächtest zu ihrer Grenze, und daß du der Pfade zu ihrem Hause kundig wärest.
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Du weißt es ja; denn damals wurdest du geboren, und die Zahl deiner Tage ist groß!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Bist du zu den Vorräten des Schnees gekommen, und hast du gesehen die Vorräte des Hagels,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
die ich aufgespart habe für die Zeit der Bedrängnis, für den Tag des Kampfes und der Schlacht?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Welches ist der Weg, auf dem das Licht sich verteilt, der Ostwind sich verbreitet über die Erde?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Wer teilt der Regenflut Kanäle ab und einen Weg dem Donnerstrahle,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
um regnen zu lassen auf ein Land ohne Menschen, auf die Wüste, in welcher kein Mensch ist,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
um zu sättigen die Öde und Verödung, und um hervorsprießen zu lassen die Triebe des Grases?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Hat der Regen einen Vater, oder wer zeugt die Tropfen des Taues?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
Aus wessen Schoße kommt das Eis hervor, und des Himmels Reif, wer gebiert ihn?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Wie das Gestein verdichten sich die Wasser, und die Fläche der Tiefe schließt sich zusammen.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Kannst du knüpfen das Gebinde des Siebengestirns, oder lösen die Fesseln des Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Kannst du die Bilder des Tierkreises hervortreten lassen zu ihrer Zeit, und den großen Bären leiten samt seinen Kindern?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Kennst du die Gesetze des Himmels, oder bestimmst du seine Herrschaft über die Erde?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Kannst du deine Stimme zum Gewölk erheben, daß eine Menge Wassers dich bedecke?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Kannst du Blitze entsenden, daß sie hinfahren, daß sie zu dir sagen: Hier sind wir? -
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Wer hat Weisheit in die Nieren gelegt, oder wer hat dem Geiste Verstand gegeben?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Wer zählt die Wolken mit Weisheit, und des Himmels Schläuche, wer gießt sie aus,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
wenn der Staub zu dichtem Gusse zusammenfließt und die Schollen aneinander kleben?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Erjagst du der Löwin den Raub, und stillst du die Gier der jungen Löwen,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
wenn sie in den Höhlen kauern, im Dickicht auf der Lauer sitzen?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Wer bereitet dem Raben seine Speise, wenn seine Jungen zu Gott schreien, umherirren ohne Nahrung?

< Ayubu 38 >