< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
A ESTO también se espanta mi corazón, y salta de su lugar.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Oid atentamente su voz terrible, y el sonido que sale de su boca.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Debajo de todos los cielos lo dirige, y su luz hasta los fines de la tierra.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Después de ella bramará el sonido, tronará él con la voz de su magnificencia; y aunque sea oída su voz, no los detiene.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
Tronará Dios maravillosamente con su voz; él hace grandes cosas, que nosotros no entendemos.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
Porque á la nieve dice: Desciende á la tierra; también á la llovizna, y á los aguaceros de su fortaleza.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Así hace retirarse á todo hombre, para que los hombres todos reconozcan su obra.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
La bestia se entrará en su escondrijo, y estaráse en sus moradas.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Del mediodía viene el torbellino, y el frío de los vientos del norte.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Por el soplo de Dios se da el hielo, y las anchas aguas son constreñidas.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Regando también llega á disipar la densa nube, y con su luz esparce la niebla.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Asimismo por sus designios se revuelven las nubes en derredor, para hacer sobre la haz del mundo, en la tierra, lo que él les mandara.
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Unas veces por azote, otras por causa de su tierra, otras por misericordia las hará parecer.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Escucha esto, Job; repósate, y considera las maravillas de Dios.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
¿Supiste tú cuándo Dios las ponía en concierto, y hacía levantar la luz de su nube?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
¿Has tú conocido las diferencias de las nubes, las maravillas del Perfecto en sabiduría?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
¿Por qué están calientes tus vestidos cuando se fija el [viento del] mediodía sobre la tierra?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
¿Extendiste tú con él los cielos, firmes como un espejo sólido?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Muéstranos qué le hemos de decir; [porque] nosotros no podemos componer [las ideas] á causa de las tinieblas.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
¿Será preciso contarle cuando yo hablaré? Por más que el hombre razone, quedará como abismado.
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
He aquí aún: no se puede mirar la luz esplendente en los cielos, luego que pasa el viento y los limpia,
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Viniendo de la parte del norte la dorada claridad. En Dios hay una majestad terrible.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
El [es] Todopoderoso, al cual no alcanzamos, grande en potencia; y en juicio y en multitud de justicia no afligirá.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Temerlo han por tanto los hombres: él no mira á los sabios de corazón.

< Ayubu 37 >