< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Elihu mówił jeszcze:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Poczekaj trochę, a pouczę cię, bo jeszcze przemówię za Boga.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Z daleka przyniosę swą wiedzę i uznam sprawiedliwość mego Stwórcy.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Bo naprawdę moje słowa nie [są] kłamstwem, a [człowiek] z doskonałą wiedzą [stoi] przed tobą.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Oto Bóg [jest] potężny, a nie gardzi [nikim]. On jest potężny w sile serca.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
Nie pozostawia niegodziwych przy życiu, a ubogim przyznaje prawa.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
Nie odwraca swoich oczu od sprawiedliwego, ale sadza ich na wieki z królami na tronie – i są wywyższeni.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
A jeśli są związani okowami albo spętani powrozami utrapienia;
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
Wtedy oznajmia im ich czyny i przestępstwa – to, że się wzmogły.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Otwiera im ucho, aby [przyjęli] karę, i każe im odwrócić się od nieprawości.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
Jeśli będą posłuszni i będą [mu] służyć, dopełnią swoich dni w dobrobycie, a swoich lat w rozkoszach.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Ale jeśli nie usłuchają, zginą od miecza, umrą bez poznania.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
Lecz [ludzie] obłudnego serca gromadzą gniew, nie wołają, kiedy ich wiąże.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Umierają w młodości, swoje życie spędzają wśród rozpustników.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Wyrywa ubogiego z utrapienia i otwiera ich uszy w ucisku.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Również ciebie wyrwałby z ciasnego miejsca na [miejsce] przestronne, gdzie nie ma ucisku, a [zastawiłby] twój stół pełnią tłuszczu.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Ale ty zasłużyłeś na sąd niegodziwego, [dlatego] prawo i sąd będą cię trzymać.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Gniew [wisi], więc uważaj, by nie poraził cię karą, gdyż nie wybawił cię żaden okup.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Czy będzie zważał na twoje bogactwa? [Nie], ani [na] złoto, ani [na] jakiekolwiek siły [lub] potęgi.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Nie tęsknij za nocą, kiedy ludzie są porwani ze swojego miejsca.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Strzeż się, abyś nie zważał na nieprawość; gdyż wybrałeś to sobie zamiast utrapienia.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Oto Bóg jest najwyższy w swojej potędze, któż może tak nauczyć jak on?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Kto mu wytyczył jego drogę? Albo kto mu powie: Popełniłeś nieprawość?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Pamiętaj, abyś wysławiał jego dzieło, któremu przypatrują się ludzie.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Wszyscy ludzie je widzą, człowiek przypatruje się nim z daleka.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Oto Bóg [jest] wielki, a poznać [go] nie możemy, a liczba jego lat jest niezbadana.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
On wyciąga bowiem krople wód, które padają z pary [jako] deszcz;
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
Który spuszczają chmury i [który] obficie spływa na ludzi.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
(A kto zrozumie rozmieszczenie chmur i grzmot jego namiotu?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Oto rozciąga nad nim swoją światłość i okrywa głębiny morskie.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Przez te rzeczy bowiem sądzi narody i daje pokarm w obfitości.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Chmurami okrywa światłość i rozkazuje [jej ukrywać] się za wyznaczoną [chmurą]).
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
Grzmot daje o nim znać, a także bydło – o parze unoszącej się w górę.

< Ayubu 36 >