< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
I made a covenant with mine eyes, and I will not think upon a virgin.
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Now what portion has God given from above? and is there an inheritance [given] of the Mighty One from the highest?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
Alas! destruction to the unrighteous, and rejection to them that do iniquity.
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Will he not see my way, and number all my steps?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
But if I had gone with scorners, and if too my foot has hasted to deceit:
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
(for I am weighed in a just balance, and the Lord knows my innocence: )
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
if my foot has turned aside out of the way, or if mine heart has followed mine eye, and if too I have touched gifts with my hands;
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
then let me sow, and let others eat; and let me be uprooted on the earth.
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
If my heart has gone forth after another man's wife, and if I laid wait at her doors;
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
then let my wife also please another, and let my children be brought low.
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
For the rage of anger is not to be controlled, [in the case] of defiling [another] man's wife.
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
For it is a fire burning on every side, and whoever it attacks, it utterly destroys.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
And if too I despised the judgment of my servant or [my] handmaid, when they pleaded with me;
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
what then shall I do if the Lord should try me? and if also he should at all visit me, can I make an answer?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Were not they too formed as I also was formed in the womb? yes, we were formed in the same womb.
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
But the helpless missed not whatever need they had, and I did not cause the eye of the widow to fail.
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
And if too I ate my morsel alone, and did not impart [of it] to the orphan;
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
(for I nourished [them] as a father from my youth and guided [them] from my mother's womb.)
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
And if too I overlooked the naked as he was perishing, and did not clothe him;
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
and if the poor did not bless me, and their shoulders were [not] warmed with the fleece of my lambs;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
if I lifted my hand against an orphan, trusting that my strength was far superior [to his]:
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
let them my shoulder start from the blade-bone, and my arm be crushed off from the elbow.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
For the fear of the Lord constrained me, and I can’t bear up by reason of his burden.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
If I made gold my treasure, and if too I trusted the precious stone;
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
and if too I rejoiced when my wealth was abundant, and if too I laid my hand on innumerable [treasures]:
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
(do we not see the shining sun eclipsed, and the moon waning? for they have not [power to continue]: )
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
and if my heart was secretly deceived, and if I have laid my hand upon my mouth and kissed it:
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
let this also then be reckoned to me as the greatest iniquity: for I [should] have lied against the Lord Most High.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
And if too I was glad at the fall of mine enemies, and mine heart said, Aha!
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
let then mine ear hear my curse, and let me be a byword among my people in my affliction.
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
And if too my handmaids have often said, Oh that we might be satisfied with his flesh; (whereas I was very kind:
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
for the stranger did not lodge without, and my door was opened to every one that came: )
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
or if too having sinned unintentionally, I hid my sin;
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
(for I did not stand in awe of a great multitude, so as not to declare boldly before them: ) and if too I permitted a poor man to go out of my door with an empty bosom:
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
(Oh that I had a hearer, ) and if I had not feared the hand of the Lord; and [as to] the written charge which I had against any one,
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
I would place [it] as a chaplet on my shoulders, and read it.
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
And if I did not read it and return it, having taken nothing from the debtor:
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
If at any time the land groaned against me, and if its furrows mourned together;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
and if I ate its strength alone without price, and if I too grieved the heart of the owner of the soil, by taking [anything] from [him]:
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
then let the nettle come up to me instead of wheat, and a bramble instead of barley. And Job ceased speaking.

< Ayubu 31 >