< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
Men no er eg til spott for deim som yngre er av år enn eg; eg deira feder ikkje fann verdige plass hjå gjætarhunden.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Magtlause er og deira hender, og deira saft og kraft er burte;
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Dei magre er av naud og svolt, dei gneg i turre øydemarki som alt i går var reine audni,
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
og plukkar melde millom kjørri og hev til føda einerot.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
Frå folket vert dei jaga burt, fær tjuvemann slengt etter seg.
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
Dei gøymer seg i fæle gil, i holor uti jord og fjell;
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
og millom buskor skrålar dei og samlast under netlerunnar;
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
ei ætt av dårar og namnlause som ein helst piskar ut or landet.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
No er eg slengjestev for deim, eit ordtak hev for deim eg vorte.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Dei styggjest ved meg, held seg burte og sparer ei å sputta på meg.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Utan all blygd dei krenkjer meg, hiv av kvart band framfor mi åsyn.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Eit utjo reiser seg til høgre, dei spenner mine føter burt, og legg ulukke-vegar mot meg.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Og stigen min den bryt dei upp og hjelper til med mi ulukka, dei som er hjelpelause sjølv.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Som gjenom vide murbrot kjem dei, velter seg fram med bråk og brak.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Imot meg vender rædslor seg, mi æra elter dei som stormen, mi velferd kvarv som lette sky.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
No jamrar seg mi sjæl i meg; usæle dagar held meg fast.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
Natti gneg mine knokar av meg, min verk, mi pina aldri søv.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Ved allmagt vert min klædnad vanstelt, heng tett som skjortekragen kring meg.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Han kasta meg i skarnet ned; og eg ser ut som mold og oska.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Eg skrik til deg, du svarar ikkje, eg stend der, og du stirer på meg.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Hard hev du vorte imot meg, du stri’r mot meg med veldug hand.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Du let meg fara burt i stormen, du let meg tynast i hans brus.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Eg veit du fører meg til dauden, der alt som liver samlast lyt.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Kven kavar ikkje når han søkk? Kven ropar ikkje ut i fåren?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Gret eg’kje sjølv med den fortrykte, og syrgde yver fatigmann?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
Eg vona godt, men det kom vondt, eg venta ljos, men myrker kom.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Det kokar allstødt i mitt indre, ulukkedagen møter meg.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Svart gjeng eg kring, men ikkje solbrend, eg ris i flokken, skrik um hjelp.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Bror åt sjakalar hev eg vorte, til strussar eg ein frende er.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Mi hud er svart og flaknar av; det brenn i mine bein av hite.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Min cither hev eg bytt i sorg, og fløyta mi med gråtar-mål.

< Ayubu 30 >