< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
“But now those who are younger than I have me in derision, whose fathers I considered unworthy to put with my sheep dogs.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Of what use is the strength of their hands to me, men in whom ripe age has perished?
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
They are gaunt from lack and famine. They gnaw the dry ground, in the gloom of waste and desolation.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
They pluck salt herbs by the bushes. The roots of the broom tree are their food.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
They are driven out from among men. They cry after them as after a thief,
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
so that they live in frightful valleys, and in holes of the earth and of the rocks.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
They bray among the bushes. They are gathered together under the nettles.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
They are children of fools, yes, children of wicked men. They were flogged out of the land.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
“Now I have become their song. Yes, I am a byword to them.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
They abhor me, they stand aloof from me, and don’t hesitate to spit in my face.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
For he has untied his cord, and afflicted me; and they have thrown off restraint before me.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
On my right hand rise the rabble. They thrust aside my feet. They cast their ways of destruction up against me.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
They mar my path. They promote my destruction without anyone’s help.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
As through a wide breach they come. They roll themselves in amid the ruin.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Terrors have turned on me. They chase my honor as the wind. My welfare has passed away as a cloud.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
“Now my soul is poured out within me. Days of affliction have taken hold of me.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
In the night season my bones are pierced in me, and the pains that gnaw me take no rest.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
My garment is disfigured by great force. It binds me about as the collar of my tunic.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
He has cast me into the mire. I have become like dust and ashes.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
I cry to you, and you do not answer me. I stand up, and you gaze at me.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
You have turned to be cruel to me. With the might of your hand you persecute me.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
You lift me up to the wind, and drive me with it. You dissolve me in the storm.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
For I know that you will bring me to death, to the house appointed for all living.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
“However doesn’t one stretch out a hand in his fall? Or in his calamity therefore cry for help?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Didn’t I weep for him who was in trouble? Wasn’t my soul grieved for the needy?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
When I looked for good, then evil came. When I waited for light, darkness came.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
My heart is troubled, and doesn’t rest. Days of affliction have come on me.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
I go mourning without the sun. I stand up in the assembly, and cry for help.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
I am a brother to jackals, and a companion to ostriches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
My skin grows black and peels from me. My bones are burned with heat.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Therefore my harp has turned to mourning, and my pipe into the voice of those who weep.

< Ayubu 30 >