< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
但如今,比我年少的人戲笑我; 其人之父我曾藐視, 不肯安在看守我羊群的狗中。
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
他們壯年的氣力既已衰敗, 其手之力與我何益呢?
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
他們因窮乏飢餓,身體枯瘦, 在荒廢淒涼的幽暗中齦乾燥之地,
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
在草叢之中採鹹草, 羅騰的根為他們的食物。
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
他們從人中被趕出; 人追喊他們如賊一般,
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
以致他們住在荒谷之間, 在地洞和巖穴中;
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
在草叢中叫喚, 在荊棘下聚集。
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
這都是愚頑下賤人的兒女; 他們被鞭打,趕出境外。
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
現在這些人以我為歌曲, 以我為笑談。
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
他們厭惡我,躲在旁邊站着, 不住地吐唾沫在我臉上。
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
鬆開他們的繩索苦待我, 在我面前脫去轡頭。
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
這等下流人在我右邊起來, 推開我的腳,築成戰路來攻擊我。
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
這些無人幫助的, 毀壞我的道,加增我的災。
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
他們來如同闖進大破口, 在毀壞之間滾在我身上。
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
驚恐臨到我, 驅逐我的尊榮如風; 我的福祿如雲過去。
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
現在我心極其悲傷; 困苦的日子將我抓住。
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
夜間,我裏面的骨頭刺我, 疼痛不止,好像齦我。
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
因上帝的大力,我的外衣污穢不堪, 又如裏衣的領子將我纏住。
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
上帝把我扔在淤泥中, 我就像塵土和爐灰一般。
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
主啊,我呼求你,你不應允我; 我站起來,你就定睛看我。
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
你向我變心,待我殘忍, 又用大能追逼我,
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
把我提在風中,使我駕風而行, 又使我消滅在烈風中。
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
我知道要使我臨到死地, 到那為眾生所定的陰宅。
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
然而,人仆倒豈不伸手? 遇災難豈不求救呢?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
人遭難,我豈不為他哭泣呢? 人窮乏,我豈不為他憂愁呢?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
我仰望得好處,災禍就到了; 我等待光明,黑暗便來了。
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
我心裏煩擾不安, 困苦的日子臨到我身。
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
我沒有日光就哀哭行去; 我在會中站着求救。
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
我與野狗為弟兄, 與鴕鳥為同伴。
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
我的皮膚黑而脫落; 我的骨頭因熱燒焦。
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
所以,我的琴音變為悲音; 我的簫聲變為哭聲。

< Ayubu 30 >