< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
After this Job opened his mouth, and cursed his day.
2 Kisha akasema:
And Job spoke, and said,
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
Let the day perish in which I was born, and the night [in which] it was said, There is a man child conceived.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Let that day be darkness; let not God regard it from above, neither let the light shine upon it.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Let darkness and the shades of death stain it; let a cloud dwell upon it; let the blackness of the day terrify it.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
As [for] that night, let darkness seize upon it; let it not be joined to the days of the year, let it not come into the number of the months.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Lo, let that night be solitary, let no joyful voice come therein.
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Let them curse it that curse the day, who are ready to raise up their mourning.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Let the stars of its twilight be dark; let it look for light, but [have] none; neither let it see the dawning of the day:
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
Because it prevented not my birth, nor hid sorrow from my eyes.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
Why died I not from the womb? [why] did I [not] expire at the time of my birth?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Why did the knees receive me? or why the breasts that I should be nursed?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
For now should I have lain still and been quiet, I should have slept: then had I been at rest,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
With kings and counselors of the earth, who built desolate places for themselves;
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
Or with princes that had gold, who filled their houses with silver:
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
Or as a hidden untimely birth I had not been; as infants [which] never saw light.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
There the wicked cease [from] troubling; and there the weary are at rest.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
[There] the prisoners rest together; they hear not the voice of the oppressor.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
The small and great are there; and the servant [is] free from his master.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
Why is light given to him that is in misery, and life to the bitter [in] soul;
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
Who long for death, but it [cometh] not; and dig for it more than for hid treasures;
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
Who rejoice exceedingly, [and] are glad, when they can find the grave?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
[Why is light given] to a man whose way is hid, and whom God hath hedged in?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
For my sighing cometh before I eat, and my roarings are poured out like the waters.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
For the thing which I greatly feared hath come upon me, and that which I dreaded hath come to me.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
I was not in safety, neither had I rest, neither was I quiet; yet trouble came.

< Ayubu 3 >