< Ayubu 29 >

1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
ヨブまた語をつぎて曰く
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
嗚呼過にし年月のごとくならまほし 神の我を護りたまへる日のごとくならまほし
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
かの時には彼の燈火わが首の上に輝やき彼の光明によりて我黑暗を歩めり
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
わが壯なりし日のごとくならまほし 彼時には神の恩惠わが幕屋の上にありき
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
かの時には全能者なほ我とともに在し わが子女われの周圍にありき
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
乳ながれてわが足跡を洗ひ 我が傍なる磐油を灌ぎいだせり
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
かの時には我いでて邑の門に上りゆき わが座を街衢に設けたり
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
少き者は我を見て隱れ 老たる者は起あがりて立ち
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
牧伯たる者も言談ずしてその口に手を當て
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
貴き者も聲ををさめてその舌を上顎に貼たりき
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
我事を耳に聞る者は我を幸福なりと呼び 我を目に見たる者はわがために證據をなしぬ
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
是は我助力を求むる貧しき者を拯ひ 孤子および助くる人なき者を拯ひたればなり
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
亡びんとせし者われを祝せり 我また寡婦の心をして喜び歌はしめたり
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
われ正義を衣また正義の衣る所となれり 我が公義は袍のごとく冠冕のごとし
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
われは盲目の目となり跛者の足となり
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
貧き者の父となり知ざる者の訴訟の由を究め
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
惡き者の牙を折り その齒の間より獲物を取いだせり
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
我すなはち言けらく 我はわが巣に死ん 我が日は砂の如く多からん
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
わが根は水の邊に蔓り 露わが枝に終夜おかん
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
わが榮光はわが身に新なるべくわが弓はわが手に何時も強からんと
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
人々われに聽き默して我が敎を俟ち
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
わが言し後は彼等言を出さず 我説ところは彼等に甘露のごとく
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
かれらは我を望み待つこと雨のごとく 口を開きて仰ぐこと春の雨のごとくなりき
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
われ彼等にむかひて笑ふとも彼等は敢て眞實とおもはず我面の光を彼等は除くことをせざりき
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
われは彼等のために道を擇び その首として座を占め 軍中の王のごとくして居り また哀哭者を慰さむる人のごとくなりき

< Ayubu 29 >