< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
Certainement l'argent a sa veine, et l'or a un lieu [d'où on le tire] pour l'affiner.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Le fer se tire de la poussière, et la pierre étant fondue rend de l'airain.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
Il a mis un bout aux ténèbres, tellement qu'on découvre le bout de toutes choses, [même] les pierres les plus cachées, et qui sont dans l'ombre de la mort.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Le torrent se débordant d'auprès d'un lieu habité, se jette dans des lieux où l'on ne met plus le pied, [mais ses eaux] se tarissent et s'écoulent par [le travail] des hommes.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
C'est de la terre que sort le pain, et au dessous elle est renversée, [et elle est] en feu.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Ses pierres sont le lieu d'où l'on tire les Saphirs; on y trouve aussi la poudre d'or.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
L'oiseau de proie n'en a point connu le sentier, et l'œil du milan ne l'a point regardé.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
Les fans du lion n'y ont point marché, le vieux lion n'a point passé par là.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
[L'homme] met sa main aux cailloux, et renverse les montagnes jusqu'aux racines.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
Il fait passer les ruisseaux au travers des rochers fendus, et son œil voit tout ce qui [y] est de précieux.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
Il arrête le cours des rivières, et il tire dehors et expose à la lumière ce qui est caché.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Mais d'où recouvrera-t-on la sagesse? et où est le lieu de l'intelligence?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
L'homme ne connaît pas sa valeur, et elle ne se trouve pas dans la terre des vivants.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
L'abîme dit: Elle n'est pas en moi; et la mer dit: Elle n'est pas avec moi.
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
Elle ne se donne point pour du fin or, et elle ne s'achète point au poids de l'argent.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
On ne l'échange point avec l'or d'Ophir, ni avec l'Onyx précieux, ni avec le Saphir.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
L'or ni le diamant n'approchent point de son prix, et on ne la donnera point en échange pour un vase de fin or.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
Il ne se parlera point de corail ni de pierre précieuse; et le prix de la sagesse monte plus haut que celui des perles.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
La topaze d'Ethiopie n'approchera point de son prix, et elle ne sera point échangée contre le pur or.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
D'où vient donc la sagesse? et où est le lieu de l'intelligence?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
Elle est couverte aux yeux de tout homme vivant, et elle est cachée aux oiseaux des cieux.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
Le gouffre et la mort disent: Nous avons entendu de nos oreilles parler d'elle.
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
C'est Dieu qui en sait le chemin, et qui sait où elle est.
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
Car c'est lui qui voit jusqu'aux extrémités du monde, et qui regarde sous tous les cieux.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
Quand il mettait le poids au vent, et qu'il pesait les eaux par mesure;
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
Quand il prescrivait une loi à la pluie, et le chemin à l'éclair des tonnerres;
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
Alors il la vit, et la manifesta; il la prépara, et même il la sonda jusqu'au fond.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
Puis il dit à l'homme: Voilà, la crainte du Seigneur est la sagesse, et se détourner du mal c'est l'intelligence.

< Ayubu 28 >