< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
Truly there is a mine for silver, and a place where gold is washed out.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Iron is taken out of the earth, and stone is changed into brass by the fire.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
Man puts an end to the dark, searching out to the farthest limit the stones of the deep places of the dark.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
He makes a deep mine far away from those living in the light of day; when they go about on the earth, they have no knowledge of those who are under them, who are hanging far from men, twisting from side to side on a cord.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
As for the earth, bread comes out of it; but under its face it is turned up as if by fire.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Its stones are the place of sapphires, and it has dust of gold.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
No bird has knowledge of it, and the hawk's eye has never seen it.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
The great beasts have not gone over it, and the cruel lion has not taken that way.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
Man puts out his hand on the hard rock, overturning mountains by the roots.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
He makes deep ways, cut through the rock, and his eye sees everything of value.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
He keeps back the streams from flowing, and makes the secret things come out into the light.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
But where may wisdom be seen? and where is the resting-place of knowledge?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
Man has not seen the way to it, and it is not in the land of the living.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
The deep waters say, It is not in me: and the sea says, It is not with me.
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
Gold may not be given for it, or a weight of silver in payment for it.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
It may not be valued with the gold of Ophir, with the onyx of great price, or the sapphire.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
Gold and glass are not equal to it in price, and it may not be exchanged for jewels of the best gold.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
There is no need to say anything about coral or crystal; and the value of wisdom is greater than that of pearls.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
The topaz of Ethiopia is not equal to it, and it may not be valued with the best gold.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
From where then does wisdom come, and where is the resting-place of knowledge?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
For it is kept secret from the eyes of all living, unseen by the birds of the air.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
Destruction and Death say, We have only had word of it with our ears.
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
God has knowledge of the way to it, and of its resting-place;
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
For his eyes go to the ends of the earth, and he sees everything under heaven.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
When he made a weight for the wind, measuring out the waters;
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
When he made a law for the rain, and a way for the thunder-flames;
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
Then he saw it, and put it on record; he gave it its fixed form, searching it out completely.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
And he said to man, Truly the fear of the Lord is wisdom, and to keep from evil is the way to knowledge.

< Ayubu 28 >