< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
“Da, srebro ima svoja nalazišta, a zlato mjesta gdje se pročišćava.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Ruda željezna iz zemlje se vadi, a iz rudače rastaljene bakar.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
Ljudi tami postavljaju granice i kopaju do najvećih dubina za kamenom u mraku zakopanim.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Čeljad iz tuđine rovove dube do kojih ljudska ne dopire noga, visi njišuć' se, daleko od ljudi.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
Krilo zemlje iz kojeg kruh nam niče kao od vatre sve je razrovano.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Stijene njene safira su skrovišta, prašina zlatna krije se u njima.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
Tih putova ne znaju grabljivice, jastrebovo ih oko ne opaža.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
Zvijeri divlje njima nisu kročile niti je kada lav njima prošao.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
Ali na kamen diže čovjek ruku te iz korijena prevraća planine.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
U kamenu prokopava prolaze, oko mu sve dragocjeno opaža.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
Žilama vode on tok zaustavlja; stvari skrivene nosi na vidjelo.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Ali otkuda nam Mudrost dolazi? Na kojemu mjestu Razum prebiva?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
Čovjek njezina ne poznaje puta, u zemlji živih nisu je otkrili.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
Bezdan govori: 'U meni je nema!' a more: 'Ne nalazi se kod mene!'
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
Zlatom se čistim kupiti ne može, ni cijenu njenu srebrom odmjeriti;
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
ne mjeri se ona zlatom ofirskim, ni oniksom skupim pa ni safirom.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
Sa zlatom, staklom ne poređuje se, nit' se daje za sud od suha zlata.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
Čemu spominjat' prozirac, koralje, bolje je steći Mudrost no biserje.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
Što je prema njoj topaz etiopski? Ni čistim zlatom ne procjenjuje se.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
Ali otkuda nam Mudrost dolazi? Na kojemu mjestu Razum prebiva?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
Sakrivena je očima svih živih; ona izmiče pticama nebeskim.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
Propast paklena i Smrt izjavljuju: 'Za slavu njenu mi smo samo čuli.' (questioned)
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
Jedino je Bog put njen proniknuo, on jedini znade gdje se nalazi.
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
Jer pogledom granice zemlje hvata i opaža sve pod svodom nebeskim.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
Kad htjede vjetru odredit težinu i mjerilom svu vodu izmjeriti,
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
kad je zakone daždu nametnuo i oblacima gromovnim putove,
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
tad ju je vidio te izmjerio, učvrstio i do dna ispitao.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
A potom je rekao čovjeku: Strah Gospodnji - eto što je mudrost; 'Zla se kloni' - to ti je razumnost.”

< Ayubu 28 >