< Ayubu 18 >

1 Bildadi Mshuhi akajibu:
Then answered Bildad the Shuhite, and said,
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
How long [will it be ere] ye make an end of words? mark, and afterwards we will speak.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
Wherefore are we counted as beasts, [and] reputed vile in your sight?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
He teareth himself in his anger: shall the earth be forsaken for thee? and shall the rock be removed out of his place?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
Yea, the light of the wicked shall be put out, and the spark of his fire shall not shine.
6 Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
The light shall be dark in his tabernacle, and his candle shall be put out with him.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
The steps of his strength shall be straitened, and his own counsel shall cast him down.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
For he is cast into a net by his own feet, and he walketh upon a snare.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
The gin shall take [him] by the heel, [and] the robber shall prevail against him.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
The snare [is] laid for him in the ground, and a trap for him in the way.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
Terrors shall make him afraid on every side, and shall drive him to his feet.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
His strength shall be hungerbitten, and destruction [shall be] ready at his side.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
It shall devour the strength of his skin: [even] the firstborn of death shall devour his strength.
14 Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
His confidence shall be rooted out of his tabernacle, and it shall bring him to the king of terrors.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
It shall dwell in his tabernacle, because [it is] none of his: brimstone shall be scattered upon his habitation.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
His roots shall be dried up beneath, and above shall his branch be cut off.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
His remembrance shall perish from the earth, and he shall have no name in the street.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
He shall be driven from light into darkness, and chased out of the world.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
He shall neither have son nor nephew among his people, nor any remaining in his dwellings.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
They that come after [him] shall be astonied at his day, as they that went before were affrighted.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Surely such [are] the dwellings of the wicked, and this [is] the place [of him that] knoweth not God.

< Ayubu 18 >