< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu:
約伯回答說:
2 “Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
你們真是子民哪, 你們死亡,智慧也就滅沒了。
3 Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
但我也有聰明,與你們一樣, 並非不及你們。 你們所說的,誰不知道呢?
4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
我這求告上帝、蒙他應允的人 竟成了朋友所譏笑的; 公義完全人竟受了人的譏笑。
5 Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
安逸的人心裏藐視災禍; 這災禍常常等待滑腳的人。
6 Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
強盜的帳棚興旺, 惹上帝的人穩固, 上帝多將財物送到他們手中。
7 “Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
你且問走獸,走獸必指教你; 又問空中的飛鳥,飛鳥必告訴你;
8 au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
或與地說話,地必指教你; 海中的魚也必向你說明。
9 Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
看這一切, 誰不知道是耶和華的手做成的呢?
10 Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
凡活物的生命和人類的氣息都在他手中。
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
耳朵豈不試驗言語, 正如上膛嘗食物嗎?
12 Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
年老的有智慧; 壽高的有知識。
13 “Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
在上帝有智慧和能力; 他有謀略和知識。
14 Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
他拆毀的,就不能再建造; 他捆住人,便不得開釋。
15 Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
他把水留住,水便枯乾; 他再發出水來,水就翻地。
16 Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
在他有能力和智慧, 被誘惑的與誘惑人的都是屬他。
17 Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
他把謀士剝衣擄去, 又使審判官變成愚人。
18 Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
他放鬆君王的綁, 又用帶子捆他們的腰。
19 Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
他把祭司剝衣擄去, 又使有能的人傾敗。
20 Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
他廢去忠信人的講論, 又奪去老人的聰明。
21 Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
他使君王蒙羞被辱, 放鬆有力之人的腰帶。
22 Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
他將深奧的事從黑暗中彰顯, 使死蔭顯為光明。
23 Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
他使邦國興旺而又毀滅; 他使邦國開廣而又擄去。
24 Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
他將地上民中首領的聰明奪去, 使他們在荒廢無路之地漂流;
25 Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.
他們無光,在黑暗中摸索, 又使他們東倒西歪,像醉酒的人一樣。

< Ayubu 12 >