< Yeremia 6 >

1 “Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
"Flee for safety, you people of Benjamin, out of the midst of Jerusalem, and blow the trumpet in Tekoa, and raise up a signal on Beth Haccherem; for evil looks forth from the north, and a great destruction.
2 Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
The comely and delicate one, the daughter of Zion, will I cut off.
3 Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
Shepherds with their flocks shall come to her; they shall pitch their tents against her all around; they shall feed everyone in his place."
4 “Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
"Prepare war against her; arise, and let us go up at noon. Woe to us. For the day declines, for the shadows of the evening are stretched out.
5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku, na kuharibu ngome zake!”
Arise, and let us go up by night, and let us destroy her palaces."
6 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma kuzunguka Yerusalemu. Mji huu ni lazima uadhibiwe, umejazwa na uonevu.
For Jehovah of hosts said, "Cut down trees, and cast up a mound against Jerusalem. She is the city to be punished; she is full of oppression in the midst of her.
7 Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake, ndivyo anavyomwaga uovu wake. Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake, ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.
As a well casts forth its waters, so she casts forth her wickedness: violence and destruction is heard in her; before me continually is sickness and wounds.
8 Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”
Be instructed, Jerusalem, lest my soul be alienated from you; lest I make you a desolation, a land not inhabited."
9 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli kwa uangalifu kama kwenye mzabibu; pitisha mkono wako kwenye matawi tena, kama yeye avunaye zabibu.”
Thus says Jehovah of hosts, "They shall thoroughly glean the remnant of Israel like a vine. Pass your hand again as a grape gatherer into the baskets."
10 Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.
To whom shall I speak and testify, that they may hear? Look, their ear is uncircumcised, and they can't listen. Look, the word of Jehovah has become a reproach to them. They have no delight in it.
11 Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana, nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani, na juu ya vijana waume waliokusanyika; mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake, hata nao wazee waliolemewa na miaka.
Therefore I am full of the wrath of Jehovah. I am weary with holding in. "Pour it out on the children in the street, and on the assembly of young men together; for even the husband with the wife shall be taken, the aged with him who is full of days.
12 Nyumba zao zitapewa watu wengine, pamoja na mashamba yao na wake zao, nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya wale waishio katika nchi,” asema Bwana.
Their houses shall be turned to others, their fields and their wives together; for I will stretch out my hand on the inhabitants of the land," says Jehovah.
13 “Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata faida zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
"For from their least even to their greatest, everyone is given to covetousness; and from the prophet even to the priest, everyone deals falsely.
14 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, ‘Amani, amani,’ wakati hakuna amani.
They have healed also the hurt of my people superficially, saying, 'Peace, peace.' when there is no peace.
15 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo; hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini nitakapowaadhibu,” asema Bwana.
Were they ashamed when they had committed abomination? No, they were not at all ashamed, neither could they blush. Therefore they shall fall among those who fall; at the time that I visit them, they shall be cast down," says Jehovah.
16 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Simama kwenye njia panda utazame, ulizia mapito ya zamani, ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’
Thus says Jehovah, "Stand in the ways and see, and ask for the old paths, 'Where is the good way?' and walk in it, and you will find rest for your souls." But they said, "We will not walk in it."
17 Niliweka walinzi juu yenu na kusema, ‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’ Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’
"I set watchmen over you, saying, 'Listen to the sound of the trumpet.'" But they said, "We will not listen."
18 Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa, angalieni, enyi mashahidi, lile litakalowatokea.
"Therefore hear, you nations, and know, congregation, what will happen to them.
19 Sikia, ee nchi: Ninaleta maafa juu ya watu hawa, matunda ya mipango yao, kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu na wameikataa sheria yangu.
Hear, earth. 'Look, I will bring disaster on this people, even the fruit of their thoughts, because they have not listened to my words; and as for my law, they have rejected it.
20 Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba, au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali? Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki, dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”
To what purpose comes there to me frankincense from Sheba, and the sweet cane from a far country? Your burnt offerings are not acceptable, nor your sacrifices pleasing to me.'
21 Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa. Baba na wana wao watajikwaa juu yake, majirani na marafiki wataangamia.”
Therefore thus says Jehovah, 'Look, I will lay stumbling blocks before this people. The fathers and the sons together shall stumble against them. The neighbor and his friend shall perish.'
22 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Tazama, jeshi linakuja kutoka nchi ya kaskazini, taifa kubwa linaamshwa kutoka miisho ya dunia.
"Thus says Jehovah, 'Look, a people comes from the north country. A great nation shall be stirred up from the uttermost parts of the earth.
23 Wamejifunga pinde na mkuki, ni wakatili na hawana huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao. Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”
They take hold of bow and spear. They are cruel, and have no mercy. Their voice roars like the sea, and they ride on horses, everyone set in array, as a man to the battle, against you, daughter of Zion.'"
24 Tumesikia taarifa zao, nayo mikono yetu imelegea. Uchungu umetushika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
"We have heard its report; our hands become feeble: anguish has taken hold of us, and pains as of a woman in labor.
25 Usitoke kwenda mashambani au kutembea barabarani, kwa kuwa adui ana upanga, na kuna vitisho kila upande.
Do not go forth into the field, nor walk by the way; for the sword of the enemy and terror, are on every side."
26 Enyi watu wangu, vaeni magunia mjivingirishe kwenye majivu, ombolezeni kwa kilio cha uchungu kama amliliaye mwana pekee, kwa maana ghafula mharabu atatujia.
"Daughter of my people, clothe yourself with sackcloth, and wallow in ashes. Mourn, as for an only son, most bitter lamentation; for the destroyer shall suddenly come on us."
27 “Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma, nao watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.
"I have made you a tester of metals and a fortress among my people; that you may know and try their way."
28 Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.
"They are all grievous rebels, going about with slanders; they are bronze and iron: they all of them deal corruptly.
29 Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure; waovu hawaondolewi.
The bellows blow fiercely; the lead is consumed of the fire: in vain do they go on refining; for the wicked are not plucked away.
30 Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu Bwana amewakataa.”
Men will call them 'rejected silver,' because Jehovah has rejected them."

< Yeremia 6 >