< Yeremia 46 >

1 Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
La parole de l'Éternel, qui fut adressée à Jérémie, le prophète, pour les nations,
2 Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
Touchant l'Égypte, touchant l'armée de Pharaon-Néco, roi d'Égypte, qui était près du fleuve de l'Euphrate, à Carkémish, et qui fut battue par Nébucadnetsar, roi de Babylone, la quatrième année de Jéhojakim, fils de Josias, roi de Juda.
3 “Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
Préparez le bouclier et l'écu, et approchez-vous pour le combat!
4 Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
Attelez les chevaux, et vous, cavaliers, montez! Présentez-vous avec les casques, fourbissez les lances, revêtez les cuirasses!
5 Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
Que vois-je? Ils sont effrayés; ils tournent le dos; leurs hommes forts sont mis en pièces; et ils fuient sans regarder en arrière; la frayeur est de toutes parts, dit l'Éternel.
6 Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
Que le plus léger ne s'enfuie point, et que le fort n'échappe pas! Au nord, sur les bords du fleuve d'Euphrate, ils chancellent et tombent!
7 “Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
Qui est celui qui monte comme le Nil, et dont les eaux s'émeuvent comme les fleuves?
8 Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
C'est l'Égypte. Elle monte comme le Nil; ses eaux s'émeuvent comme les fleuves; elle dit: “Je monterai; je couvrirai la terre; je détruirai les villes et ceux qui y habitent! “
9 Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
Montez, chevaux; chars, précipitez-vous! Et que les hommes vaillants se montrent: ceux de Cush et de Put qui manient le bouclier, et les Ludiens qui manient et bandent l'arc!
10 Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
Ce jour est au Seigneur, à l'Éternel des armées; c'est un jour de vengeance, pour se venger de ses ennemis. L'épée dévore, s'assouvit, s'enivre de leur sang; car il y a un sacrifice au Seigneur, l'Éternel des armées, dans le pays du nord, sur les bords de l'Euphrate.
11 “Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
Monte en Galaad, et prends du baume, vierge, fille de l'Égypte! En vain multiplies-tu les remèdes; point de guérison pour toi!
12 Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
Les nations ont appris ta honte, et ton cri remplit la terre; car les forts ont chancelé l'un sur l'autre, et tous deux sont tombés ensemble.
13 Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
La parole que l'Éternel prononça à Jérémie, le prophète, touchant la venue de Nébucadnetsar, roi de Babylone, pour frapper le pays d'Égypte:
14 “Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
Annoncez-le en Égypte; publiez-le à Migdol, publiez-le à Noph et à Tachphanès! Dites: Lève-toi et tiens-toi prêt; car l'épée dévore autour de toi.
15 Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
Pourquoi tes vaillants hommes sont-ils emportés? Ils n'ont pu tenir ferme, parce que l'Éternel les a renversés.
16 Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
Il en a fait chanceler un grand nombre, et même ils tombent l'un sur l'autre, et ils disent: “Allons, retournons vers notre peuple et au pays de notre naissance, loin de l'épée qui désole. “
17 Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
Là, ils s'écrient: “Pharaon, roi d'Égypte, n'est que du bruit! Il a laissé échapper l'occasion. “
18 “Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
Je suis vivant, dit le roi dont le nom est l'Éternel des armées, comme le Thabor entre les montagnes, comme le Carmel qui s'avance dans la mer, il viendra!
19 Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
Fais ton bagage pour la captivité, habitante, fille de l'Égypte; car Noph deviendra un désert, elle sera brûlée, elle n'aura plus d'habitants.
20 “Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
L'Égypte est comme une très belle génisse; mais la destruction vient, elle vient du nord.
21 Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
Ses mercenaires aussi sont chez elle comme des veaux bien nourris. Mais eux aussi, ils tournent le dos, ils fuient ensemble; ils ne tiennent pas ferme; car le jour de la calamité est venu sur eux, le temps de leur visitation.
22 Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
Sa voix se fait entendre comme celle du serpent; car ils marchent avec une armée, et ils viennent contre elle avec des haches, comme des bûcherons.
23 Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
Ils coupent sa forêt, dit l'Éternel, parce qu'elle est impénétrable. Car ils sont plus nombreux que les sauterelles, on ne pourrait les compter.
24 Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
La fille d'Égypte est honteuse; elle est livrée entre les mains d'un peuple du nord.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
L'Éternel des armées, le Dieu d'Israël a dit: Voici, je vais punir Amon de No, Pharaon, l'Égypte, ses dieux et ses rois, Pharaon et ceux qui se confient en lui.
26 Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
Et je les livrerai entre les mains de ceux qui cherchent leur vie, entre les mains de Nébucadnetsar, roi de Babylone, et entre les mains de ses serviteurs. Mais après cela, elle sera habitée comme aux jours d'autrefois, dit l'Éternel.
27 “Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
Et toi, Jacob, mon serviteur, ne crains point; ne t'épouvante pas, Israël! Car voici, je te délivrerai du pays lointain, et ta postérité de la terre où elle est captive. Alors Jacob reviendra, et sera en repos et à l'aise, et il n'y aura personne qui le trouble.
28 Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”
Toi, Jacob, mon serviteur, ne crains point, dit l'Éternel; car je suis avec toi. Je détruirai entièrement toutes les nations parmi lesquelles je t'ai dispersé; mais toi, je ne te détruirai point entièrement; je te châtierai avec mesure; cependant je ne te tiendrai pas pour innocent.

< Yeremia 46 >