< Yeremia 43 >

1 Yeremia alipomaliza kuwaambia watu maneno yote ya Bwana Mungu wao, yaani kila kitu Bwana alichokuwa amemtuma kuwaambia,
Gdy Jeremiasz przestał mówić do całego ludu te wszystkie słowa PANA, ich Boga, z którymi posłał go do nich PAN, ich Bóg, wszystkie te słowa;
2 Azaria mwana wa Hoshaya, na Yohanani mwana wa Karea, na watu wote wenye kiburi wakamwambia Yeremia, “Wewe unasema uongo! Bwana Mungu wetu hajakutuma kusema, ‘Kamwe msiende Misri kukaa huko.’
Azariasz, syn Hoszajasza, i Jochanan, syn Kareacha, oraz wszyscy pyszni mężczyźni powiedzieli do Jeremiasza: Kłamstwo mówisz! Nie posłał cię PAN, nasz Bóg, byś mówił: Nie idźcie do Egiptu, aby tam przebywać;
3 Lakini Baruku mwana wa Neria anakuchochea dhidi yetu ili ututie mikononi mwa Wakaldayo, ili watuue au watuchukue uhamishoni Babeli.”
Ale Baruch, syn Neriasza, podburza cię przeciwko nam, aby nas wydać w ręce Chaldejczyków, żeby nas pobili albo uprowadzili do niewoli do Babilonu.
4 Basi Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi, na watu wote wakakataa kutii amri ya Bwana ya kukaa katika nchi ya Yuda.
Dlatego Jochanan, syn Kareacha, oraz wszyscy dowódcy wojsk, a także cały lud nie słuchali głosu PANA, aby pozostać w ziemi Judy.
5 Badala yake, Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi wakawaongoza mabaki yote ya Yuda waliokuwa wamerudi kuishi katika nchi ya Yuda kutoka mataifa yote ambayo walikuwa wametawanywa.
Lecz Jochanan, syn Kareacha, i wszyscy dowódcy wojsk zabrali całą resztkę Judy, która powróciła ze wszystkich narodów, do których została wygnana, by zamieszkać w ziemi Judy:
6 Pia wakawaongoza wanaume wote, wanawake na watoto, na binti za mfalme ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha na Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, na nabii Yeremia, na Baruku mwana wa Neria.
Mężczyzn, kobiety, dzieci, córki króla oraz każdą duszę, którą pozostawił Nebuzaradan, dowódca gwardii, z Gedaliaszem, synem Achikama, syna Szafana, z prorokiem Jeremiaszem i z Baruchem, synem Neriasza;
7 Kwa hiyo wakaingia Misri kwa kutokumtii Bwana, wakaenda mpaka Tahpanhesi.
I poszli do ziemi Egiptu, bo nie usłuchali głosu PANA. I przybyli do Tachpanches.
8 Huko Tahpanhesi neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
I w Tachpanches doszło do Jeremiasza słowo PANA mówiące:
9 “Wayahudi wakiwa wanaona, chukua baadhi ya mawe makubwa na kuyazika katika udongo wa mfinyanzi katika njia iliyojengwa kwa matofali katika ingilio la jumba la kifalme la Farao huko Tahpanhesi.
Weź do rąk wielkie kamienie i ukryj je w glinie w piecu do wypalania cegieł, który jest przy wejściu do domu faraona w Tachpanches, na oczach mężczyzn Judy;
10 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Nitamtumania mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, nami nitakiweka kiti chake cha enzi juu ya haya mawe niliyoyazika hapa, naye atatandaza hema yake ya ufalme juu yake.
I powiedz im: Tak mówi PAN zastępów, Bóg Izraela: Oto poślę po Nabuchodonozora, króla Babilonu, mego sługę, i sprowadzę [go], i ustawię jego tron na tych kamieniach, które ukryłem; i rozciągnie swój baldachim na nich.
11 Atakuja na kuishambulia Misri, akiwaua wale waliokusudiwa kuuawa, awateke mateka wale waliokusudiwa kutekwa, na upanga kwa wale waliokusudiwa upanga.
Gdy przyjdzie, pobije ziemię Egiptu, a [oddani] na śmierć na śmierć [pójdą], oddani do niewoli do niewoli pójdą, i oddani pod miecz pod miecz pójdą.
12 Atachoma moto mahekalu yao ya miungu ya Misri, atachoma mahekalu yao na kuteka miungu yao. Kama vile mchungaji ajizungushiavyo vazi lake ndivyo atakavyojizungushia Misri na kuondoka mahali hapo bila kudhurika.
Podłożę ogień w domach bogów Egiptu i on je spali, i uprowadzi. Przyozdobi się ziemią Egiptu, jak pasterz zakłada swoją szatę, i wyjdzie stamtąd w pokoju.
13 Humo ndani ya hekalu la jua nchini ya Misri atabomoa nguzo za ibada, na kuteketeza kwa moto mahekalu ya miungu wa Misri.’”
Rozbije posągi w Betszemesz, które [jest] w ziemi Egiptu, oraz ogniem spali domy bogów egipskich.

< Yeremia 43 >