< Yeremia 4 >

1 “Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
"If you will return, Israel," says Jehovah, "if you will return to me, and if you will put away your abominations out of my sight; then you shall not be removed;
2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
and you shall swear, 'As Jehovah lives,' in truth, in justice, and in righteousness. The nations shall bless themselves in him, and in him shall they glory."
3 Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
For thus says Jehovah to the men of Judah and to Jerusalem, "Break up your fallow ground, and do not sow among thorns.
4 Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
Circumcise yourselves to Jehovah, and take away the foreskins of your heart, you men of Judah and inhabitants of Jerusalem; lest my wrath go forth like fire, and burn so that none can quench it, because of the evil of your doings.
5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
Declare in Judah, and publish in Jerusalem; and say, 'Blow the trumpet in the land.' Cry aloud and say, 'Assemble yourselves. Let us go into the fortified cities.'
6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
Set up a standard toward Zion. Flee for safety. Do not wait; for I will bring evil from the north, and a great destruction."
7 Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
A lion is gone up from his thicket, and a destroyer of nations; he is on his way, he is gone forth from his place, to make your land desolate, that your cities be laid waste, without inhabitant.
8 Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
For this clothe yourself with sackcloth, lament and wail; for the fierce anger of Jehovah hasn't turned back from us.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
"It shall happen at that day," says Jehovah, "that the heart of the king shall perish, and the heart of the officials; and the priests shall be astonished, and the prophets shall wonder."
10 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
Then I said, "Ah, Lord Jehovah. Surely you have greatly deceived this people and Jerusalem, saying, 'You shall have peace;' whereas the sword reaches to the heart."
11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
At that time shall it be said to this people and to Jerusalem, "A hot wind from the bare heights in the wilderness toward the daughter of my people, not to winnow, nor to cleanse;
12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
a full wind from these shall come for me. Now I will also utter judgments against them."
13 Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
Look, he shall come up as clouds, and his chariots shall be as the whirlwind: his horses are swifter than eagles. Woe to us. For we are ruined.
14 Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
Jerusalem, wash your heart from wickedness, that you may be saved. How long shall your evil thoughts lodge within you?
15 Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
For a voice declares from Dan, and publishes evil from the hills of Ephraim:
16 “Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
"Tell the nations; look, publish against Jerusalem, 'Besiegers come from a far country, and raise their voice against the cities of Judah.
17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
As keepers of a field, they are against her all around, because she has been rebellious against me,'" says Jehovah.
18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
"Your way and your doings have brought these things to you. This is your wickedness; for it is bitter, for it reaches to your heart."
19 Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
My anguish, my anguish. I am pained at my very heart; my heart is disquieted in me; I can't hold my peace; because you have heard, O my soul, the sound of the trumpet, the alarm of war.
20 Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
Destruction on destruction is proclaimed; for the whole land is laid waste: suddenly are my tents destroyed, and my curtains in a moment.
21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
How long shall I see the standard, and hear the sound of the trumpet?
22 “Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
"For my people are foolish, they do not know me. They are foolish children, and they have no understanding. They are skillful in doing evil, but to do good they have no knowledge."
23 Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
I saw the earth, and, look, it was waste and void; and the heavens, and they had no light.
24 Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
I saw the mountains, and look, they trembled, and all the hills moved back and forth.
25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
I saw, and look, there was no man, and all the birds of the sky had fled.
26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
I saw, and look, the fruitful field was a wilderness, and all its cities were broken down at the presence of Jehovah; before his fierce anger they were destroyed.
27 Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
For thus says Jehovah, "The whole land shall be a desolation; yet I will not make a full end.
28 Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
For this the earth will mourn, and the heavens above be black; because I have spoken it, I have purposed it, and I have not relented, neither will I turn back from it."
29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
Every city flees for the noise of the horsemen and archers; they go into caves, and they hide themselves in the thickets, and climb up on the rocks; every city is forsaken, and not a man dwells in it.
30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
You, when you are made desolate, what will you do? Though you clothe yourself with scarlet, though you dress yourselves with ornaments of gold, though you enlarge your eyes with paint, in vain do you make yourself beautiful; your lovers despise you, they seek your life.
31 Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”
For I have heard a voice as of a woman in travail, the anguish as of her who brings forth her first child, the voice of the daughter of Zion, who gasps for breath, who spreads her hands, saying, "Woe is me now. For my soul faints before the murderers."

< Yeremia 4 >