< Yeremia 32 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Nebukadneza.
The word that came to Jeremiah from Jehovah in the tenth year of Zedekiah king of Judah, which was the eighteenth year of Nebuchadnezzar.
2 Wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi katika jumba la kifalme la Yuda.
Now at that time the king of Babylon's army was besieging Jerusalem; and Jeremiah the prophet was shut up in the court of the guard, which was in the king of Judah's house.
3 Basi Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga huko akisema, “Kwa nini unatabiri hivyo? Wewe unasema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteka.
For Zedekiah king of Judah had shut him up, saying, "Why do you prophesy, and say, 'Thus says Jehovah, "Look, I will give this city into the hand of the king of Babylon, and he shall take it;
4 Sedekia mfalme wa Yuda hataweza kuponyoka mikononi mwa Wakaldayo, lakini kwa hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atazungumza naye ana kwa ana na kumwona kwa macho yake mwenyewe.
and Zedekiah king of Judah shall not escape out of the hand of the Chaldeans, but shall surely be delivered into the hand of the king of Babylon, and shall speak with him mouth to mouth, and his eyes shall see his eyes;
5 Atamchukua Sedekia hadi Babeli, mahali atakapoishi mpaka nitakapomshughulikia, asema Bwana. Kama utapigana dhidi ya Wakaldayo, hutashinda.’”
and he shall bring Zedekiah to Babylon, and he shall be there until I visit him," says Jehovah: "though you fight with the Chaldeans, you shall not prosper?"'"
6 Yeremia akasema, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
Jeremiah said, "The word of Jehovah came to me, saying,
7 Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako atakuja kwako na kusema, ‘Nunua shamba langu huko Anathothi, kwa sababu wewe kama jamaa ya karibu ni haki na wajibu wako kulinunua.’
'Look, Hanamel the son of Shallum your uncle shall come to you, saying, "Buy my field that is in Anathoth; for the right of redemption is yours to buy it."'
8 “Kisha, kama Bwana alivyosema, binamu yangu Hanameli alinijia katika ua wa walinzi na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini. Kwa kuwa ni haki yako kulikomboa na kulimiliki, jinunulie.’ “Nilijua kwamba hili lilikuwa neno la Bwana.
So Hanamel my uncle's son came to me in the court of the guard according to the word of Jehovah, and said to me, "Please buy my field that is in Anathoth, which is in the land of Benjamin; for the right of inheritance is yours, and the redemption is yours; buy it for yourself.' Then I knew that this was the word of Jehovah.
9 Hivyo nikalinunua shamba hilo lililoko Anathothi kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nami nikampimia shekeli kumi na saba za fedha.
I bought the field that was in Anathoth of Hanamel my uncle's son, and weighed him the money, even seventeen shekels of silver.
10 Nikatia sahihi na kuweka muhuri hati ya kumiliki, nikaweka mashahidi, na kupima ile fedha kwenye mizani.
I subscribed the deed, and sealed it, and called witnesses, and weighed him the money in the balances.
11 Nikachukua ile hati ya kununulia, nakala iliyotiwa muhuri yenye makubaliano na masharti, pia pamoja na ile nakala isiyo na muhuri,
So I took the deed of the purchase, both that which was sealed, containing the terms and conditions, and that which was open;
12 nami nikampa Baruku mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, hati hii mbele ya binamu yangu Hanameli, na mbele ya mashahidi waliokuwa wameweka sahihi kwenye hati hii na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ua wa walinzi.
and I delivered the deed of the purchase to Baruch the son of Neriah, the son of Mahseiah, in the presence of Hanamel my cousin, and in the presence of the witnesses who subscribed the deed of the purchase, before all the Jews who sat in the court of the guard.
13 “Nilimpa Baruku maelezo haya mbele yao:
I commanded Baruch before them, saying,
14 ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Chukua hati hizi, yaani nakala zote zenye muhuri na zisizo na muhuri za hati ya kununulia, na uziweke kwenye gudulia la udongo wa mfinyanzi ili zidumu kwa muda mrefu.
'Thus says Jehovah of hosts, the God of Israel: "Take these deeds, this deed of the purchase which is sealed, and this deed which is open, and put them in an earthen vessel; that they may continue many days."'
15 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nyumba, mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’
For thus says Jehovah of hosts, the God of Israel: 'Houses and fields and vineyards shall yet again be bought in this land.'
16 “Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria hii hati ya kununulia, nilimwomba Bwana:
Now after I had delivered the deed of the purchase to Baruch the son of Neriah, I prayed to Jehovah, saying,
17 “Ee Bwana Mwenyezi, umeumba mbingu na nchi kwa uwezo wako mkuu na kwa mkono ulionyooshwa. Hakuna jambo lililo gumu usiloliweza.
'Ah, Jehovah. Look, you have made the heavens and the earth by your great power and by your outstretched arm; there is nothing too difficult for you,
18 Wewe huonyesha upendo kwa maelfu, lakini huleta adhabu kwa ajili ya dhambi za baba mapajani mwa watoto wao baada yao. Ee Mungu mkuu na mwenye uweza, ambaye jina lako ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,
who show loving kindness to thousands, and recompense the iniquity of the fathers into the bosom of their children after them; the Great, the Mighty God, Jehovah of hosts is his name;
19 makusudi yako ni makuu, na matendo yako ni yenye uwezo. Macho yako yanaona njia zote za wanadamu, nawe humlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake, na kama yanavyostahili matendo yake.
great in counsel, and mighty in work; whose eyes are open on all the ways of human beings, to give to each person according to his ways, and according to the fruit of his doings.
20 Ulitenda ishara za miujiza na maajabu huko Misri, na umeyaendeleza mpaka leo, katika Israeli na miongoni mwa wanadamu wote, nawe umejulikana na kufahamika hivyo mpaka leo.
You performed signs and wonders in the land of Egypt, and to this day in Israel and among all humankind, and have made a name for yourself to this day.
21 Uliwatoa watu wako Israeli kutoka Misri kwa ishara na maajabu, kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa na kwa matisho makuu.
You brought forth your people Israel out of the land of Egypt with signs, and with wonders, and with a strong hand, and with an outstretched arm, and with great terror;
22 Uliwapa nchi hii uliyokuwa umeapa kuwapa baba zao, nchi inayotiririka maziwa na asali.
and gave them this land, which you swore to their fathers to give them, a land flowing with milk and honey;
23 Waliingia na kuimiliki, lakini hawakukutii wala kuifuata sheria yako. Hawakufanya kile ulichowaamuru kufanya. Hivyo ukaleta maafa haya yote juu yao.
and they came in, and possessed it, but they did not obey your voice, neither walked in your law; they have done nothing of all that you commanded them to do: therefore you have caused all this evil to come on them.
24 “Tazama jinsi tumezungukwa na jeshi ili kuuteka mji huu. Kwa sababu ya upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo ambao wanaushambulia. Ulilosema limetokea kama vile unavyoona sasa.
Look, the mounds, they have come to the city to take it; and the city is given into the hand of the Chaldeans who fight against it, because of the sword, and of the famine, and of the pestilence; and what you have spoken has happened; and look, you see it.
25 Ingawa mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo, wewe, Ee Bwana Mwenyezi, uliniambia, ‘Nunua shamba kwa fedha, na jambo hilo lishuhudiwe.’”
You have said to me, Lord Jehovah, "Buy the field for money, and call witnesses"; whereas the city is given into the hand of the Chaldeans.'"
26 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Then came the word of Jehovah to Jeremiah, saying,
27 “Mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza?
"Look, I am Jehovah, the God of all flesh: is there anything too difficult for me?
28 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa Wakaldayo, na mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ambaye atauteka.
Therefore thus says Jehovah: 'Look, I will give this city into the hand of the Chaldeans, and into the hand of Nebuchadnezzar king of Babylon, and he shall take it:
29 Wakaldayo ambao wanaushambulia mji huu watakuja na kuuchoma moto na kuuteketeza, pamoja na nyumba ambamo watu wamenikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba katika mapaa na kumimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine.
and the Chaldeans, who fight against this city, shall come and set this city on fire, and burn it, with the houses, on whose roofs they have offered incense to Baal, and poured out drink offerings to other gods, to provoke me to anger.
30 “Watu wa Israeli na wa Yuda hawakufanya kitu kingine ila uovu mbele zangu tangu ujana wao. Naam, watu wa Israeli hawakufanya kitu kingine ila kunikasirisha kwa kazi ambazo mikono yao imetengeneza, asema Bwana.
For the children of Israel and the people of Judah have done only that which was evil in my sight from their youth; for the children of Israel have only provoked me to anger with the work of their hands, says Jehovah.
31 Tangu siku ulipojengwa hadi sasa, mji huu umenikasirisha na kunighadhibisha kiasi kwamba ni lazima niuondoe machoni pangu.
For this city has been to me a provocation of my anger and of my wrath from the day that they built it even to this day; that I should remove it from before my face,
32 Watu wa Israeli na wa Yuda wamenikasirisha kwa uovu wote waliofanya: wao, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao, watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu.
because of all the evil of the children of Israel and of the people of Judah, which they have done to provoke me to anger, they, their kings, their officials, their priests, and their prophets, and the men of Judah, and the inhabitants of Jerusalem.
33 Walinigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao. Ingawa niliwafundisha tena na tena, hawakupenda kusikiliza wala kuitikia adhabu.
They have turned to me the back, and not the face: and though I taught them, rising up early and teaching them, yet they have not listened to receive instruction.
34 Waliweka miungu yao ya kuchukiza sana katika nyumba iitwayo kwa Jina langu na kuinajisi.
But they set their abominations in the house which is called by my name, to defile it.
35 Wakajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu kwa ajili ya Baali katika Bonde la Ben-Hinomu, ambapo walitoa wana wao na binti zao kafara kwa Moleki, ingawa kamwe sikuamuru, wala halikuingia akilini mwangu, kwamba watafanya chukizo kama hilo na kumfanya Yuda atende dhambi.
They built the high places of Baal, which are in the Valley of Ben Hinnom, to cause their sons and their daughters to pass through fire to Molech; which I did not command them, neither did it come into my mind, that they should do this abomination, to cause Judah to sin.'
36 “Mnasema kuhusu mji huu, ‘Kwa upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babeli,’ lakini hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo:
"Now therefore thus says Jehovah, the God of Israel, concerning this city, about which you say, 'It is given into the hand of the king of Babylon by the sword, and by the famine, and by the pestilence':
37 Hakika nitawakusanya kutoka nchi zote nilizowafukuzia katika hasira yangu kali na ghadhabu yangu kuu, nitawarudisha mahali hapa na kuwaruhusu waishi kwa salama.
'Look, I will gather them out of all the countries, where I have driven them in my anger, and in my wrath, and in great indignation; and I will bring them again to this place, and I will cause them to dwell safely:
38 Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
and they shall be my people, and I will be their God:
39 Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili kwamba waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao.
and I will give them one heart and one way, that they may fear me forever, for their good, and of their children after them:
40 Nitafanya nao agano la milele: Kamwe sitaacha kuwatendea mema, nami nitawavuvia kunicha mimi, ili kamwe wasigeukie mbali nami.
and I will make an everlasting covenant with them, that I will not turn away from following them, to do them good; and I will put my fear in their hearts, that they may not depart from me.
41 Nitafurahia kuwatendea mema, na kwa hakika nitawapanda katika nchi hii kwa moyo wangu wote na roho yangu yote.
Yes, I will rejoice over them to do them good, and I will plant them in this land assuredly with my whole heart and with my whole soul.'
42 “Hili ndilo asemalo Bwana: Kama nilivyoleta maafa haya makubwa kwa watu hawa, ndivyo nitakavyowapa mafanikio niliyowaahidi.
"For thus says Jehovah: 'Just as I have brought all this great disaster on this people, so will I bring on them all the good that I have promised them.
43 Kwa mara nyingine tena mashamba yatanunuliwa katika nchi hii ambayo mlisema, ‘Imekuwa ukiwa, isiyofaa, isiyo na watu wala wanyama, kwa sababu imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.’
Fields shall be bought in this land, about which you say, "It is desolate, without man or animal; it is given into the hand of the Chaldeans."
44 Mashamba yatanunuliwa kwa fedha, na hati zitatiwa sahihi, zitatiwa muhuri na kushuhudiwa katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda na katika miji ya nchi ya vilima, sehemu za magharibi katika miji ya tambarare na katika Negebu, kwa sababu nitarudisha tena mafanikio yao, asema Bwana.”
Men shall buy fields for money, and subscribe the deeds, and seal them, and call witnesses, in the land of Benjamin, and in the places about Jerusalem, and in the cities of Judah, and in the cities of the hill country, and in the cities of the lowland, and in the cities of the Negev: for I will cause their captivity to return,' says Jehovah."

< Yeremia 32 >