< Yeremia 28 >

1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
Cette même année, au commencement du règne de Sédécias, roi de Juda, la quatrième année, au cinquième mois, Hanania, fils d'Azzur, prophète de Gabaon, me parla dans la maison de l'Éternel, en la présence des sacrificateurs et de tout le peuple, et dit:
2 “Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
Ainsi a dit l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël: J'ai rompu le joug du roi de Babylone.
3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
Encore deux années, et je fais rapporter en ce lieu tous les vases de la maison de l'Éternel que Nébucadnetsar, roi de Babylone, a pris de ce lieu et qu'il a emportés à Babylone.
4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
Et je ferai revenir dans ce lieu, dit l'Éternel, Jéchonias, fils de Jéhojakim, roi de Juda, et tous les captifs de Juda qui sont allés à Babylone; car je romprai le joug du roi de Babylone.
5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
Alors Jérémie, le prophète, parla à Hanania, le prophète, en présence des sacrificateurs et en présence de tout le peuple, qui se tenaient dans la maison de l'Éternel.
6 Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
Et Jérémie, le prophète, dit: Amen! qu'ainsi fasse l'Éternel! Que l'Éternel accomplisse les paroles que tu as prophétisées, et qu'il fasse revenir de Babylone en ce lieu les vases de la maison de l'Éternel et tous les captifs de Babylone.
7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
Toutefois, écoute cette parole que je prononce à tes oreilles et aux oreilles de tout le peuple:
8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
Les prophètes qui ont été avant moi et avant toi, dès longtemps, ont prophétisé contre plusieurs pays et contre de grands royaumes, la guerre, et l'affliction, et la peste.
9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
Si un prophète prophétise la paix, c'est par l'accomplissement de sa parole que ce prophète sera reconnu pour véritablement envoyé de l'Éternel.
10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
Alors Hanania, le prophète, prit le joug de dessus le cou de Jérémie, le prophète, et le rompit.
11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
Puis Hanania parla en présence de tout le peuple, en disant: Ainsi a dit l'Éternel: C'est ainsi que je romprai, dans deux années, le joug de Nébucadnetsar, roi de Babylone, de dessus le cou de toutes les nations. Et Jérémie, le prophète, s'en alla son chemin.
12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
Or la parole de l'Éternel fut adressée à Jérémie en ces mots, après que Hanania, le prophète, eut rompu le joug de dessus le cou de Jérémie, le prophète:
13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
Va et parle à Hanania, et dis-lui: Ainsi a dit l'Éternel: Tu as rompu des jougs de bois; mais, au lieu de ceux-là, tu auras des jougs de fer.
14 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
Car ainsi a dit l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël: J'ai mis un joug de fer sur le cou de toutes ces nations, pour qu'elles soient asservies à Nébucadnetsar, roi de Babylone, et elles lui seront asservies; et même je lui ai donné les bêtes des champs.
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
Puis Jérémie, le prophète, dit à Hanania, le prophète: Écoute, Hanania! l'Éternel ne t'a pas envoyé; mais tu as fait que ce peuple a mis sa confiance dans le mensonge.
16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
C'est pourquoi ainsi a dit l'Éternel: Voici, je te rejette de dessus la terre; tu mourras cette année; car tu as prêché la révolte contre l'Éternel.
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.
Et Hanania, le prophète, mourut cette année-là, au septième mois.

< Yeremia 28 >