< Yeremia 24 >

1 Baada ya Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na maafisa, mafundi stadi na wahunzi wa Yuda, kuchukuliwa kutoka Yerusalemu kwenda Babeli na Nebukadneza mfalme wa Babeli kwenda uhamishoni huko Babeli, Bwana akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya Hekalu la Bwana.
L'Éternel me fit voir une vision. Et voici, deux paniers de figues étaient posés devant le temple de l'Éternel, après que Nébucadnetsar, roi de Babylone, eut transporté de Jérusalem Jéchonias, fils de Jéhojakim, roi de Juda, et les principaux de Juda, avec les charpentiers et les serruriers, et les eut emmenés à Babylone.
2 Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama zile za mavuno ya kwanza. Kikapu cha pili kilikuwa na tini dhaifu sana, mbovu mno zisizofaa kuliwa.
L'un des paniers avait de fort bonnes figues, comme sont d'ordinaire les figues de la première récolte; et l'autre panier avait de fort mauvaises figues, dont on ne pouvait manger, tant elles étaient mauvaises.
3 Kisha Bwana akaniuliza, “Je, Yeremia, unaona nini?” Nikamjibu, “Ninaona tini zile zilizo nzuri ni nzuri sana, lakini zilizo dhaifu ni mbovu mno zisizofaa kuliwa.”
Et l'Éternel me dit: Que vois-tu, Jérémie? Et je répondis: Des figues; les bonnes figues, fort bonnes; et les mauvaises, fort mauvaises, trop mauvaises pour être mangées.
4 Kisha neno la Bwana likanijia:
Et la parole de l'Éternel me fut adressée, et il me dit:
5 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama zilivyo hizi tini nzuri, ndivyo ninavyowaona kuwa bora watu wa uhamisho kutoka Yuda, niliowaondoa kutoka mahali hapa kwenda katika nchi ya Wakaldayo.
Ainsi a dit l'Éternel, le Dieu d'Israël: Comme tu distingues ces bonnes figues, ainsi je distinguerai, pour leur bien, les captifs de Juda, que j'ai envoyés de ce lieu au pays des Caldéens.
6 Macho yangu yatakuwa juu yao kwa ajili ya kuwapatia mema, nami nitawarudisha tena katika nchi hii. Nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa,
Et je les regarderai d'un œil favorable, et je les ferai retourner en ce pays, et je les rétablirai et ne les détruirai plus; je les planterai et ne les arracherai plus.
7 nitawapa moyo wa kunifahamu mimi, kwamba mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.
Et je leur donnerai un cœur pour connaître que je suis l'Éternel; ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu; car ils reviendront à moi de tout leur cœur.
8 “‘Lakini kama zilivyo zile tini dhaifu, ambazo ni mbovu mno zisizofaa kuliwa,’ asema Bwana, ‘ndivyo nitakavyomtendea Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na mabaki wengine kutoka Yerusalemu, wawe wamebaki katika nchi hii, au wanaishi Misri.
Et comme ces mauvaises figues, qu'on ne peut manger, tant elles sont mauvaises, a dit l'Éternel, tels je rendrai Sédécias, roi de Juda, et ses princes, et le reste de Jérusalem, ceux qui sont restés dans ce pays, et ceux qui habitent dans le pays d'Égypte.
9 Nitawafanya kuwa chukizo kabisa na kitu cha kulaumiwa katika mataifa yote ya dunia, watakuwa aibu na kitu cha kudharauliwa, chombo cha dhihaka na kulaaniwa, popote nitakapowafukuzia.
Et je les livrerai pour être agités et maltraités par tous les royaumes de la terre, et pour être en opprobre, en proverbe, en risée, et en malédiction, dans tous les lieux où je les aurai chassés.
10 Nitautuma upanga, njaa na tauni dhidi yao hadi wawe wameangamia kutoka nchi niliyowapa wao na baba zao.’”
Et j'enverrai sur eux l'épée, la famine et la peste, jusqu'à ce qu'ils soient consumés de dessus la terre que je leur avais donnée, à eux et à leurs pères.

< Yeremia 24 >